YUSUF MANJI AUNGANA NA FAMILIA YAKE, NI BAADA YA KESI YA UHUJUMU UCHUMI KUFUTWA

Mfanyabiashara Yusuf Manji, akiwa huru wakati anatoka mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, leo Septemba 14, 2017. NA K-VI...





Mfanyabiashara Yusuf Manji, akiwa huru wakati anatoka mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, leo Septemba 14, 2017.




NA K-VIS BLOG
OFISI ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali, (DPP), imeiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu jijini Dar es Salaam kuwa haina nia ya kuendelea na Kesi ya Uhujumu Uchumi iliyomfungulia Mfanyabiashara maarufu nchini, Bw. Yusuf Manji na kwa maana hiyo Mahakama ikaamua kuifuta kesi hiyo na kumuachia huru Mfanyabiashara huyo.


Pamoja na Manji, pia washtakwia wenzake wawili, nao wameachiliwa huru.


Mkurugenzi wa ashtaka aliwasilisha hati ya kuomba kuondolewa kwa mashitaka dhidi yao kwa kuwa hana nia ya kuendelea kuwashitaki.
Baada ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi, kueleza nia hiyo ya DPP, Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama hiyo, Bw. Huruma Shaidi, aliyekuwa akisikiliza shauri hilo aliliondoa na kuwaachia huru washitakiwa hao.
Baada ya kusota rumande kwa miezi kadhaa, leo hii Manji amepata fursa ya kuungana na familia yake na jamaa zake na kabla ya kuachiwa huru, Manji na wenzake waliletwa Mahakamani hapo wakitokea Mahabusu ya gereza la Keko.

Manji alishtakiwa kwa kosa la uhujumu uchumi baada ya kukutwa na vitambaa vya sare za jeshi vyenye thamani ya shilingi milioni 200 pamoaja na mihuri ya jeshi.


“Kama tulivyomzoea Yusuf Manji, ni mfanyabiashara na atarudi na kusimamia shughuli zake za kila siku, uhuru wake ni muhuimu na tunaimani atanednelea na biashara zake.” Alisema wakili wake, Bw. Hudson Ndusyepo.
Mfanyabiashara huyo bado anakabiliwa na kesi nyingine ya matumizi ya madawa ya kulevya ambapo kesi hyo imefikia hatua ya utetezi.
Manji akiwa na wakili wake Bw. Hudson Ndusyepo.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: YUSUF MANJI AUNGANA NA FAMILIA YAKE, NI BAADA YA KESI YA UHUJUMU UCHUMI KUFUTWA
YUSUF MANJI AUNGANA NA FAMILIA YAKE, NI BAADA YA KESI YA UHUJUMU UCHUMI KUFUTWA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEifCWEA8YO4ei23b8WYFKnTIgqbi7X29BKLIAPup6tlYxbBTryZjLcLzwb2Zfe49corYWZiTLdeIO0Ch15J3iwNsC9lPrrUfSxoGXoOUMZdhueGdfjFoUmSkYl893-6qc6tCiAcbIrStK0l/s640/IMG-20170914-WA0082.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEifCWEA8YO4ei23b8WYFKnTIgqbi7X29BKLIAPup6tlYxbBTryZjLcLzwb2Zfe49corYWZiTLdeIO0Ch15J3iwNsC9lPrrUfSxoGXoOUMZdhueGdfjFoUmSkYl893-6qc6tCiAcbIrStK0l/s72-c/IMG-20170914-WA0082.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/09/yusuf-manji-aungana-na-familia-yake-ni.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/09/yusuf-manji-aungana-na-familia-yake-ni.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy