UKOMO WA KUSHUGHULIKIA MAOMBI YA MUDA MREFU YA KUUNGANISHA UMEME NI AGOSTI 30. WAZIRI KALEMANI

Na Teresia Mhagama Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani ameeleza kuwa ukomo wa kuunganishia umeme wateja walioom...

Na Teresia Mhagama

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani ameeleza kuwa ukomo wa kuunganishia umeme wateja walioomba kuunganishiwa huduma hiyo kwa muda mrefu ni Agosti 30, 2017 na Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) atakayeshindwa kutimiza agizo hilo atashushwa cheo.

Dkt. Kalemani aliyasema hayo kwa nyakati tofauti akiwa katika ziara ya kuzindua mradi wa Usambazaji Umeme Vijijini wa Awamu ya Tatu katika mikoa ya Rukwa, Ruvuma na Mtwara.

"Unakuta kuna wateja wameomba kuunganishiwa umeme miezi kadhaa iliyopita lakini mpaka sasa hawajaunganishwa wakati vifaa vipo, kwa hili lazima tuchukue hatua kwa Meneja kama ni wa wilaya, mkoa, Kanda au Mkurugenzi atayechelewa kuunganishia wateja Umeme," alisema Dkt. Kalemani.

Dkt. Kalemani alisema kuwa muda wa kumuunganishia mteja Umeme mara anapolipia huduma hiyo ni Siku Saba na si vinginevyo."Natambua kuna maeneo ambayo TANESCO mnafanya kazi vizuri lakini katika hili tutawajibishana," alisisitiza Dkt. Kalemani.

Wakati huohuo. Dkt. Kalemani aliwaagiza watendaji wa TANESCO kuhakikisha kuwa watu wote wanaofanya kazi ya kutandaza nyaya za umeme ndani ya nyumba wawe wanatambulika na Shirika hilo ili kuondoa tatizo la vishoka kufanya kazi hiyo pasipo ufanisi na baadaye kuleta madhafa kama ya moto.

Vilevile aliwataka watendaji hao kutokukaa maofisini na badala yake wawafuate wananchi sehemu walipo, suala ambalo litafanya Shirika hilo kuongeza idadi ya wateja na kuwaondolea wananchi kero ya kutembea kwa umbali mrefu kufuata huduma TANESCO.

Kuhusu usimamizi wa mradi wa usambazaji Umeme Vijijini Awamu ya Tatu ambao umeshaanza kutekelezwa nchini, Dkt Kalemani aliwataka watendaji wa TANESCO kuhakikisha kuwa wanawasimamia wakandarasi wanaofanya kazi hiyo usiku na mchana ili mradi ukamilike ndani muda uliopangwa.

Aidha Dkt. Kalemani alitoa maagizo mbalimbali ambayo yanapaswa kutekelezwa na wakandarasi wote waliopewa kazi ya kusambaza umeme vijijini katika Mradi wa Awamu ya Tatu.

Naibu Waziri aliwaagiza Wakandarasi hao kutoajiri wakandarasi wasaidizi wanaotoka nje ya eneo lao la kazi ili wananchi wanaotoka katika maeneo hayo wapate ajira na kutoa huduma mbalimbali kwa wakandarasi hao na hivyo kujiongezea kipato.

Pia aliwataka wakandarasi hao kutokuruka kijiji, kitongoji, sehemu zinazotoa huduma muhimu kama mitambo ya maji, Shule, vituo vya afya na sehemu za biashara, na nyumba ambazo tayari zimeshafanyiwa malipo ya kuunganishwa na huduma ya umeme.

" nisingependa kusikia Kituo cha Afya, Shule au Mitambo ya Maji imerukwa na haijawekewa Umeme hivyo nichukue nafasi hii kuwashauri watendaji wa Halmashauri nchini kutenga fedha kwenye Bajeti zao kwa ajili ya kutandaza nyaya za Umeme kwenye sehemu hizo ili wakandarasi waweze kuingiza Umeme," alisema Dkt. Kalemani.

Vilevile, Dkt. Kalemani aliwataka wakandarasi hao kutoa malipo kwa wakandarasi wadogo ndani ya wakati ili kuepusha mradi huo kusuasua na kuwacheleweshea huduma wananchi.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani akizungumza na wananchi (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa mradi wa kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu katika mkoa wa Ruvuma.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: UKOMO WA KUSHUGHULIKIA MAOMBI YA MUDA MREFU YA KUUNGANISHA UMEME NI AGOSTI 30. WAZIRI KALEMANI
UKOMO WA KUSHUGHULIKIA MAOMBI YA MUDA MREFU YA KUUNGANISHA UMEME NI AGOSTI 30. WAZIRI KALEMANI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiQ2lAwZG7v7FVD2Fua4QRLin8h7X7tgwS2Lwfqu8S8njdo03Wy0Auqu_uHTNPmycSa1rc3fk7Hmlax7pJ9IBE51bcHinz721g_jh2w8ETYOEm5z4q9EJItbSS-hJuf8R9_n9cbwdvIzwdv/s640/pic+saba.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiQ2lAwZG7v7FVD2Fua4QRLin8h7X7tgwS2Lwfqu8S8njdo03Wy0Auqu_uHTNPmycSa1rc3fk7Hmlax7pJ9IBE51bcHinz721g_jh2w8ETYOEm5z4q9EJItbSS-hJuf8R9_n9cbwdvIzwdv/s72-c/pic+saba.JPG
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/08/ukomo-wa-kushughulikia-maombi-ya-muda.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/08/ukomo-wa-kushughulikia-maombi-ya-muda.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy