TAMKO LA SERIKALI KUHUSU UTARATIBU WA UTOAJI WA LESENI ZA MACHAPISHO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA IDARA YA HABARI-MAELEZO          TAARIFA KWA UMMA KUANZA UTOAJI WA LESENI KWA MAGAZETI N...


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

IDARA YA HABARI-MAELEZO

        




TAARIFA KWA UMMA
KUANZA UTOAJI WA LESENI KWA MAGAZETI NA MAJARIDA
Dar es Salaam, Agosti 23, 2017:

SERIKALI kupitia Idara ya Habari (MAELEZO) inapenda kuutaarifu umma kuwa katika utekelezaji wa matakwa ya kifungu cha 5(e) cha Sheria ya Huduma za Habari, 2016, itaanza kutoa leseni za machapisho mbalimbali ikiwemo magazeti na majarida yote nchini.

Utoaji wa leseni hizo pia ni kwa mujibu wa Kanuni ya 7 ya Kanuni za Sheria ya Huduma za Habari za mwaka 2017 zilizochapishwa kwa mujibu wa Tangazo la Serikali Na 18 la Februari 3, 2017.

Kwa mujibu wa sheria, utaratibu wa sasa unafuta mfumo wa awali wa utoaji wa Hati za Usajili wa magazeti na majarida uliokuwa ukitumika kwa mujibu wa Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976 ambayo kwa sasa imefutwa.

Aidha utaratibu huu mpya utawahusu wamiliki wote wa magazeti (newspapers), majarida (journals, magazines na newsletters) na wamiliki wapya ambao hawakuwa wameyasajili machapisho yao. Aidha leseni hizi zitahuishwa kila mwaka kwa mujibu wa Kanuni za 8(3) na 12(1)(2) za Kanuni za Sheria ya Huduma za Habari, 2017.

Fomu za maombi pamoja, akaunti ya kulipia na orodha ya nyaraka zinazohitajika kwa ajili ya usajili vinapatikana kuanzia leo katika ofisi za MAELEZO Dar es Salaam na Dodoma au katika sehemu ya “Huduma Zetu” katika tovuti yetu: www.maelezo.go.tz.

Kwa wamiliki wa magazeti na majarida ambao wana usajili wa zamani, Serikali inatoa fursa  kuanzia leo mpaka Oktoba 15, 2017 wawe wamekamilisha taratibu na kupatiwa leseni mpya za uendeshaji na uchapishaji wa majarida na magazeti na baada ya muda huo hawataruhusiwa kuyachapisha kwani watakuwa wametenda kosa kisheria.
Kwa ufafanuzi zaidi kuhusu utaratibu wa usajili, wasiliana nasi katika namba 0622 664606 na 0717 312417, tembelea tovuti yetu au wasiliana nasi kupitia: maelezo@habari.go.tz
Imetolewa na:




Dkt. Hassan Abbasi,
Mkurugenzi Mkuu, Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali.




  




COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: TAMKO LA SERIKALI KUHUSU UTARATIBU WA UTOAJI WA LESENI ZA MACHAPISHO
TAMKO LA SERIKALI KUHUSU UTARATIBU WA UTOAJI WA LESENI ZA MACHAPISHO
https://lh6.googleusercontent.com/ZCn83Gfk5PDRNzyJjuAuBLVW27D3bBYa1n-b6fYj0INjwn66BKvxyzNXZIZDIP4OSdsUXlwOhdTe6eqAwCJ9pJahyEcEHuZxJm0pkOcAOjHK8dbFBeUiell5fBSWlWTQBgFcWyXLTmN-cvY4rA
https://lh6.googleusercontent.com/ZCn83Gfk5PDRNzyJjuAuBLVW27D3bBYa1n-b6fYj0INjwn66BKvxyzNXZIZDIP4OSdsUXlwOhdTe6eqAwCJ9pJahyEcEHuZxJm0pkOcAOjHK8dbFBeUiell5fBSWlWTQBgFcWyXLTmN-cvY4rA=s72-c
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/08/tamko-la-serikali-kuhusu-utaratibu-wa_65.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/08/tamko-la-serikali-kuhusu-utaratibu-wa_65.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy