RAIS DKT MAGUFULI APOKEWA KWA SHANGWE NA NDEREMO MKOANI TANGA

 Msafara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ukielekea mkoani Tanga ambako katika ziara yake ya sik...




 Msafara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ukielekea mkoani Tanga ambako katika ziara yake ya siku tano ataungana na mgeni wake Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda kesho Jumamosi katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la kuanza kwa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima hadi bandari ya Tanga
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Tanga pamoja na maelfu ya wananchi wa Mkata wakati akiwasili mkoani Tanga
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Tanga pamoja na maelfu ya wananchi wa Mkata wakati akiwasili mkoani Tanga.



Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amefuta umiliki wa mashamba matano yenye jumla ya hekari 14,000 yaliyoshindwa kuendelezwa na wamiliki wake katika Wilaya ya Muheza mkoani Tanga.
Hatua hiyo imechukuliwa na Rais Magufuli wakati akiwahutubia wananchi wa Wilaya hiyo alipokuwa anapita kuelekea Tanga kwa ajili ya shughuli ya uwekaji wa jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa bomba la kusafirishia mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Tanga,Tanzania.
Rais amefuta umiliki huo baada ya baadhi ya wananchi wa wilaya hiyo waliopewa mashamba hayo kwa ajili ya kuwekeza katika miradi mbalimbali ya kilimo ambacho kingeiingizia Serikali mapato, kuyaacha maeneo hayo bila kufanya uwekezaji tarajiwa.
“Tayari nimeshafuta umiliki wa mashamba matano yaliyokuwa yamechukuliwa bila kuendelezwa, nimeyarudisha kwa uongozi wa Mkoa ili wayapange maeneo hayo kwa ajili ya shughuli za Serikali pamoja na kuyagawa kwa wananchi. Nasisitiza wananchi wagaiwe mashamba hayo bure,” alisema Rais Magufuli.
Rais Magufuli ameongeza kuwa ardhi ya mkoa wa Tanga haikupangwa kwa ajili ya wawekezaji bali ni ardhi kwa ajili ya wananchi wote hivyo wana haki ya kupewa bure ardhi hiyo iliyoshindwa kuendelezwa.
Katika safari hiyo ya kuelekea Tanga mabapo alisimama maeneo mbalimbali kuwahutubia wananchi, Rais Magufuli alimpongeza Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Mhandisi Robert Gabriel kwa kutumia vizuri fedha za Serikali kuhamasisha vikundi vya wananchi kujenga madarasa kwa gharama ndogo na kuwataka viongozi wengine kuiga mfano wake.
Alipopewa nafasi ya kuwasalimia wananchi, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alisema kuwa utekelezaji wa maagizo mbalimbali ya Rais Magufuli unaonesha wazi dhamira yake ya kutaka kuifanya Tanzania kuwa mpya hivyo ni jukumu la kila Mtanzania kuhakikisha hamkatishi tamaa Rais Magufuli kwa kufanya kazi kwa bidii.
“Tunampongeza Rais Magufuli kwa juhudi zake za kuibadilisha Tanzania, katika bajeti ya sekta ya afya ya mwaka huu, tumepewa shilingi milioni 650 kwa ajili ya kuimarisha kituo cha afya cha Mkuzi, kikubwa ninaomba mtusaidie kuwaibua wanaouza dawa za Serikali ili tukomeshe tabia hii,” alisisitiza Waziri Ummy.
Baadhi ya maeneo ambayo Rais alisimama kuongea na wananchi wakati akielekea Tanga ni pamoja na Mkata, Michungwani, Hale, Muheza na Mkanyageni.
Rais Magufuli pamoja na Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda wanatarajiwa kuweka Jiwe la Msingi katika mradi mkubwa wa ujenzi wa bomba la mafuta la kutoka Hoima nchini Uganda mpaka Tanga, Tanzania. Jiwe hilo la msingi litawekwa eneo la Chongoleani lililopo Barabara ya Horohoro kuelekea Mombasa nje kidogo ya jiji la Tanga.

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimia  maelfu ya wananchi wa Mkata  akiwasili mkoani Tanga
 Sehemu ya umati wa wananchi wa Mkata wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
 Sehemu ya umati wa wananchi wa Mkata wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
 Sehemu ya umati wa wananchi wa Mkata wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
 Sehemu ya umati wa wananchi wa Mkata wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
 Sehemu ya umati wa wananchi wa Mkata wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
 Sehemu ya umati wa wananchi wa Mkata wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
 Sehemu ya umati wa wananchi wa Mkata wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
 Sehemu ya umati wa wananchi wa Mkata wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na wananchi Mkata
 Sehemu ya umati wa wananchi wa Mkata wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiaga baada ya kuongea na wananchi wa Mkata
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa aliposimama kuongea na wananchi eneo la Komkonga
  Sehemu ya wananchi wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliposimama kuongea nao eneo la Komkonga
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na wananchi aliposimama eneo la Komkonga
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na wananchi aliposimama eneo la Komkonga
 Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe. Godwin Gondwe akimshangilia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati akiongea na wananchi aliposimama eneo la Komkonga
 Wananchi wakiwa na furaha kumuona Rais wao


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza kwa kazi nzuri na ya mfano  katika kuendeleza elimu Mkuu wa wilaya ya Korogwe Mhe. Robet Gabriel 


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza kwa kazi nzuri na ya mfano  katika kuendeleza elimu Mkuu wa wilaya ya Korogwe Mhe. Robet Gabriel 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea
Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe. Godwin Gondwe akiongea jambo na  Mkuu wa wilaya ya Korogwe Mhe. Robet Gabriel 
 Wananchi wa Hale wakimsikiliza Rais
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na wananchi wa Michungwani


 Wananchi wakimshangilia Rais Magufuli
 Rais akisalimiana na wananchi wa Kabuku 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia vazi la mwananchi
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia vazi la mwananchi 
 Msafara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ukisimamishwa na maelfu ya wananchi kila alipopita 
 Wenyeji kwa wageni wakifurahia ujio wa Rais Magufuli
 Msafara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ukisimamishwa na maelfu ya wananchi kila alipopita 
 Msafara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ukisimamishwa na maelfu ya wananchi kila alipopita 
 Rais Magufuli akiongea na wananchi eneo la Hale
 Wananchi wenye furaha wakimsikiliza Rais Magufuli
 Wengi walitumia simu zao za mkononi kumrekodi Rais Magufuli
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira Mhe January Makamba akiongea 
 Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akilakiwa na Mkuu wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Hajat Mhandisi Mwanasha Tumbo alipowasili wilayani humo
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Mbunge wa Muheza Mhe. Adadi Rajabu
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa kwa shangwe na wananchi wa Muheza
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisoma mabango alipowasili wailayani Muheza
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndg. Abdulrahmana Kinana akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Mhe. Henry Shekifu wakati wa mkutano wa hadhara wilayani Muheza
  Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndg. Abdulrahmana Kinana akiongea katika  mkutano wa hadhara wilayani Muheza
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akitambulishwa kwa wananchi wakati wa mkutano wa hadhara wilayani Muheza
  Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimia  wananchi wakati wa mkutano wa hadhara wilayani Muheza
  Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwa meza kuu na Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martine Shigella wakati wa mkutano wa hadhara wilayani Muheza


 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndg. Abdulrahmana Kinana katika  mkutano wa hadhara wilayani Muheza
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndg. Abdulrahmana Kinana akiongea na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira Mhe January Makamba  katika  mkutano wa hadhara wilayani Muheza


  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na wananchi wa Muheza
 Wananchi wa Muheza wakimsikiliza  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli 
 Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini Mhe. Stephen Ngonyani aka 'Profesa Maji Marefu' akisalimia wananchi
 Mbunge wa Pangani Jumaa Aweso akisalimia wananchi
  Mbunge wa Korogwe Mjini Mhe. Mary Chatanda akisalimia wananchi
 Mbunge akisalimia wananchi
 Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini Mhe Omari Kigoda akisalimia wananchi
 Mbunge wa Muheza Mhe. Adadi Rajabu akisalimia wananchi
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipata picha na baadhi ya viongozi wa Muheza
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Profesa Maji Marefu
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipata picha na baadhi ya watoto waliokuwepo kwenye mkutano wake wa hadhara Muheza
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza diwani wa Pongwe Mhe. Mbaraka Saadi Mbaraka akimuelezea changamoto za eneo lake


    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza  diwani wa Pongwe Mhe. Mbaraka Saadi Mbaraka aliyemuelezea kwa ufasaha changamoto za eneo lake 
    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsifia  diwani wa Pongwe Mhe. Mbaraka Saadi Mbaraka kwa kumuelezea changamoto za eneo lake. 


 Wananchi na diwani wa Pongwe Mhe. Mbaraka Saadi Mbaraka wakifurahia umauzi wa Rais wa kujengwa kituo cha mabasi eneo lao 
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akielekeza eneo la Pongwe lijengwe kituo cha mabasi na kuitwa jina la diwani wa Pongwe Mhe. Mbaraka Saadi Mbaraka baada ya  kufurahishwa na jinsi alivyomuelezea kwa ufasaha  changamoto mbalimbali za eneo lake. (Picha zote na IKULU)

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: RAIS DKT MAGUFULI APOKEWA KWA SHANGWE NA NDEREMO MKOANI TANGA
RAIS DKT MAGUFULI APOKEWA KWA SHANGWE NA NDEREMO MKOANI TANGA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgR7Ca8-dnGjUFN09jRU0kzcm_EyemhaZ5ve8X2mOFsy2sMwgox3gQDLhySeUe9DRl5rmuEwPCulWE5cWHNBe7kwu4BfJC435rACzGM3bS8dbKVIC04ZQCM_NXxhPhu6PPXGHRCMg8mzCE/s640/IMGS0014.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgR7Ca8-dnGjUFN09jRU0kzcm_EyemhaZ5ve8X2mOFsy2sMwgox3gQDLhySeUe9DRl5rmuEwPCulWE5cWHNBe7kwu4BfJC435rACzGM3bS8dbKVIC04ZQCM_NXxhPhu6PPXGHRCMg8mzCE/s72-c/IMGS0014.JPG
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/08/rais-dkt-magufuli-apokewa-kwa-shangwe.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/08/rais-dkt-magufuli-apokewa-kwa-shangwe.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy