Jenerali Joseph Ole Nkaissery enzi za Uhai wake. Waziri huyo amefariki dunia saa chache baada yake kulazwa katika hospitali ...
Jenerali Joseph Ole Nkaissery enzi za Uhai wake.
Waziri
huyo amefariki dunia saa chache baada yake kulazwa katika hospitali ya
kibinafsi ya Karen kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu.
Taarifa za kifo chake zimetangazwa na mkuu wa utumishi wa umma Bw Joseph Kinyua mwendo wa saa kumi na moja alfajiri.
“Ni kwa huzuni kubwa na mshangao kwamba tunatangaza kifo cha ghafla cha Waziri wa Usalama wa Ndani Jenerali Mstaafu Joseph Nkaissery,” taarifa ya Bw Kinyua imesema.
“Taifa litaendelea kupashwa habari zaidi punde maelezo yatakapopatikana.”
Jenerali Nkaissery amefariki siku chache baada ya mwanasiasa mkongwe G.G Gitahi aliyekuwa seneta wa jimbo la Laikipia kufariki dunia.
Waziri
wa elimu nchini Kenya Dkt Fred Matiang'i (pichani) ameteuliwa kuwa
kaimu waziri wa usalama wa ndani kufuatia kifo cha aliyekuwa waziri Meja
Jenerali Mstaafu Joseph Nkaissery.
COMMENTS