Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi ajikuta akikesha ofisini kwake pamoja na wananchi takriban 189 wen...
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi ajikuta akikesha ofisini kwake pamoja na wananchi takriban 189 wenye Matatizo na Kero za ardhi.
Mhe.
Waziri ametumia takriban saa 20 kusikiliza kero za wananchi ambao
waligoma kuondoka ofisini kwake hadi kero zao zitakapopatiwa ufumbuzi.
Kazi hiyo ilianza majira ya saa 2 asubuhi hadi saa 9 usiku.
Hata hivyo wananchi walilazimika kulala Wizarani wakisubiri kuonana na Waziri kutokana na uwepo wa idadi kubwa ya wananchi hao.
Wananachi
wengi wenye matatizo na Kero za ardhi kutoka maeneo ya Bagamoyo,
Kibaha, Mkuranga, Kibiti na Dar es salaam kwa ujumla wametumia fursa hii
ya kipekee ya kuonana na Waziri mwenye dhamana ya Ardhi na kumuelezea
kero zao na hatimaye kupatiwa ufumbuzi papo hapo.
Wananchi
hao wamesifu hatua hii ya Waziri Lukuvi kukutana nao ana kwa ana na
kuzitatua kero zao za ardhi kwa kuwa haijawahi kutokea. Nae Bwana
Francis Kamara mkazi wa Ilala jijini Dar es salaam amemuomba Waziri
aweze kuwaajibisha watumishi ambao wanakwamisha jitihada zake hadi
kupelekea yeye kukutana na wananchi moja kwa moja.
Mwanzoni
mwa mwezi Juni 2017 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe.
William Lukuvi alitoa Tangazo la kuwataka wakazi wa kanda ya Dar es
Salaam na Pwani ambao wangependa kumuona, wafike katika ofisi yake ya
kanda ya Dar es Salaam iliyopo ghorofa ya pili, jengo la Wizara ya Ardhi
– Magogoni, Kivukoni ili kujiandikisha majina yao, anuani na namba zao
za simu.
Aidha,
Mhe. Waziri atafanya ziara kama hii katika kanda nyingine mara baada ya
kukamilisha zoezi hilo katika Kanda ya Dar es Salaam na Pwani.
Baadhi
ya wananchi wa Pwani na Dar es Salaam wakiwa ofisi za Wizara ya ardhi
mida ya saa 9 usiku kusubiri kusikilizwa kero zao za ardhi na Waziri wa
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mh. William Lukuvi.
Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mh. William Lukuvi akitatua
kero za ardhi za wananchi wa Pwani na Dar es Salaam waliofika ofisini
kwake.
Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mh. William Lukuvi akitatua
kero za ardhi za wananchi wa Pwani na Dar es Salaam waliofika ofisini
kwake.
Mkazi
wa Goba jijini Dar es salaam Bibi Fatuma Shami akipata ufafanuzi kutoka
kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mh. William Lukuvi
kuhusu eneo lake kuvamiwa na kupata miliki pandikizi.
Mkazi
wa Kibaha Mkoa wa Pwani Bibi Mariam Hamis akipata ufafanuzi kutoka kwa
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mh. William Lukuvi
kuhusu eneo lake lililo na Mgogoro.
Baadhi
ya wananchi kutoka Wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani wakimueleza Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mh. William Lukuvi kuhusu
mgogoro wao wa ardhi katika ofisi za Wizara ya ardhi.
Watumishi
wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani waliokesha na Waziri Waziri wa Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi, Mh. William Lukuvi wakati wa kutatua migogoro ya
ardhi kutoka kwa wananchi.
COMMENTS