WATUMISHI WA MAHAKAMA WAASWA KUSHUGHULIKIA VITENDO VYA RUSHWA

WAZIRI wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi amewaasa watumishi wa mahakama kushughulikia vitendo vya rushwa kwani vin...


WAZIRI wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi amewaasa watumishi wa mahakama kushughulikia vitendo vya rushwa kwani vinaipatia mahakama taswira hasi na kuzitaka tume za  mahakama na maadili kuchunguza vitendo vya ukiukwaji wa maadili na kuchukua hatua stahiki.

Waziri Kabudi, amesema hayo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na watumishi wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani juu ya mustakabali wa taasisi hiyo, ikiwa ni mara yake ya  kwanza kufanya ziara tangu alipoteuliwa kuwa Waziri.

Amesema, majaji na mahakimu mara nyingi, wamekuwa wakihusishwa na vitendo vya rushwa hivyo, na kuchangia kuwepo kwa kutokuwa na imani kwa wananchi wanaokuwa na shida, mbali mbali katika taasisi hizo, hasa wale wenye kesi.

 ‘’Pamoja na mabadiliko makubwa katika mahakama bado kumekuwa na changamoto ya uadilifu hususan vitendo vya rushwa na uwajibikaji ambavyo vimeleta taswira hasi kwa wananchi wanaotafuta haki na kusababisha ushiriki mdogo,’’alisema Profesa Kabudi.

Ameongeza, watendaji wanapaswa kubuni mbinu mbali mbali za kuweza kubadili taswira hiyo kwa kuwachukulia hatua za kinidhamu wanaokiuka maadili na kusogeza huduma kwa wananchi.Kwa mujibu wa Profesa Kabudi, mahakama inanafasi kubwa ya kuchangia maendeleo ya nchi na kwamba jambo wanalopaswa kufanya ni kuimarisha utendaji kazi na kutokomeza rushwa.

Kwa upande wake, Kaimu Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma alisema kuwa wataendelea kutumia sheria kwa ajili ya kuwainua wananchi wengi kwa lengo la kukuza uchumi.

Profesa Juma alisema majaji na mahakimu ni sehemu ya jamii ambao wanapaswa kushiriki kustawisha wanaqnchi ili kutokomeza umasikini.
Akiwasilisha ripoti kuhusu mahakama, Mtendaji Mkuu wa mahakama, Hussein Katanga alisema kuwa idadi ya majaji imeshuka kutoka 100 hadi 80 huku uhitaji wake ukiwa ni kati ya 100 hadi 120.

Katanga alisema majaji 20 wameacha kazi kwa sababu mbalimbali ikiwemo kustaafu na kwamba uhitaji huo unachangia kasi ya kuongezeka kwa ufunguaji mashauri.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WATUMISHI WA MAHAKAMA WAASWA KUSHUGHULIKIA VITENDO VYA RUSHWA
WATUMISHI WA MAHAKAMA WAASWA KUSHUGHULIKIA VITENDO VYA RUSHWA
https://1.bp.blogspot.com/-M9P_AKNm4dM/WWjGZtgm0YI/AAAAAAAB6X4/9rlGyqDAXvsMNLcG4Bji0EHrHvtbDUr5wCLcBGAs/s640/J37B1186_700x600.JPG
https://1.bp.blogspot.com/-M9P_AKNm4dM/WWjGZtgm0YI/AAAAAAAB6X4/9rlGyqDAXvsMNLcG4Bji0EHrHvtbDUr5wCLcBGAs/s72-c/J37B1186_700x600.JPG
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/07/watumishi-wa-mahakama-waaswa.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/07/watumishi-wa-mahakama-waaswa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy