WAAJIRI NCHINI WATAKIWA KUFANYA UHAKIKI WA KINA KWA AJIRA MPYA ZITAKAZOTOLEWA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki akiwasili katika Halmashauri ya W...



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki akiwasili katika Halmashauri ya Wilaya ya Kinondoni leo wakati wa ziara yake ya kikazi katika Wilaya hiyo kuzungumza na Watumishi wa Umma. Katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Ally S. Happi akimkaribisha Waziri Kairuki, na kushoto ni Mkurugenzi wa Wilaya ya Kinondoni, Aron Kagurumjuli.


Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Ally S. Happi akizungumza na watumishi wa umma wa wilaya ya Kinondoni leo (hawapo pichani) wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) katika Wilaya hiyo kuzungumza na Watumishi wa Umma, Jijini Dar es Salaam. 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akizungumza na watumishi wa Wilaya ya Kinondoni (hawapo pichani) wakati wa ziara yake ya kikazi katika wilaya hiyo leo Jijini Dar es Salaam. 


Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Kinondoni, Sixtha Kevin Komba akiwasilisha hoja wakati wa kikao kazi kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) alipofanya ziara ya kikazi katika wilaya ya Kinondoni leo Jijini Dar es Salaam. 



Afisa Utumishi Mwandamizi kutoka Idara ya Ukuzaji Maadili Ofisi ya Rais- Utumishi, Leyla Mavika akitoa ufafanuzi kuhusu masuala ya maadili katika Utumishi wa Umma wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) katika Wilaya ya Kinondoni leo Jijini Dar es Salaam. 




Mstahiki Meya Manispaa ya Kinondoni Mhe. Benjamini Sitta (kulia) akitoa neno la shukrani kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) baada ya kupokea hoja za watumishi wa Umma wa Wilaya ya Kinondoni leo Jijini Dar es Salaam. Pichani- Katikati ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) na kushoto ni Mkurugenzi Manispaa ya Kinondoni Bw. Aron Kagurumjuli. (Picha na Genofeva Matemu - MAELEZO)


Waajiri nchini wametakiwa kufanya uhakiki wa kina wa vyeti vya elimu kwa ajira mpya zitakazotolewa ili kuwa na watumishi wa umma wenye sifa zinazostahili katika utumishi wa umma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) amesema hayo leo katika kikao kazi na Watumishi wa Umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam.


Mhe. Kairuki amesema uhakiki wa kina utasaidia sana kuepukana na kutojirudia tena kwa suala la watumishi wa umma wanaoghushi vyeti.

“Jana tumetoa vibali vya ajira 10,184 kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa, Sekretarieti za Mikoa, Wakala za Serikali, pamoja na Taasisi na Mashirika ya Umma ili kujaza nafasi zilizoachwa na watumishi wa umma waliobainika kughushi vyeti vya elimu, hivyo napenda niwasisitize sana waajiri wote kufanya uhakiki wa kina ili tusiwe tena na watumishi wa umma wasiostahili katika orodha ya malipo” Mhe. Kairuki amesema.

Waziri Kairuki amesisitiza kuwa zoezi la uhakiki ni endelevu ambapo lazima lifanyika pale mtumishi wa umma atakaporudi katika kituo cha kazi kutoka masomoni na watakaorejea katika utumishi wa umma baada ya likizo bila malipo au sababu nyingine.

“Tunafanya hivi sio kwa nia mbaya, bali tunataka tuwe na watumishi wanaostahili kuwepo katika utumishi wa umma kwa sababu wanaoghushi wanaziba nafasi za wale wanaostahili kuwepo na wenye sifa katika utumishi wa umma” Mhe. Kairuki aliongeza

Pia amewataka Waajiri kusafisha taarifa wa watumishi wa umma mara kwa mara katika Mfumo Shirikishi wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara (HCMIS).

“Kuna watumishi ambao muda wao wa kuwepo kazini umemalizika (wamestaafu) lakini bado wanaendelea kuwepo, Mfumo wa HCMIS sasa kila ifikapo saa 06:01 usiku utakuwa unawaondoa wale wote ambao muda wao wa kuwepo kazini umefika lakini bado wanaendelea kuwepo kwenye Mfumo.



Mhe, Kairuki yuko katika ziara ya kikazi katika mkoa wa Dar es Salaam, ambapo leo ni siku yake ya nne aliyoitumia kukutana na Watendaji na watumishi wa umma wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, baada ya kuzungumza na watumishi wa umma wa Temeke na Mbagala.

Lengo la ziara ni kukutana na watumishi wa umma na kusikiliza malalamiko, ushauri na changamoto zinazowakabili katika maeneo yao ya kazi ili kuweza kuzifanyia kazi na kuleta mabadiliko katika Utumishi wa Umma nchini.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Ofisi ya Rais-UTUMISHI

13.07.2017

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAAJIRI NCHINI WATAKIWA KUFANYA UHAKIKI WA KINA KWA AJIRA MPYA ZITAKAZOTOLEWA
WAAJIRI NCHINI WATAKIWA KUFANYA UHAKIKI WA KINA KWA AJIRA MPYA ZITAKAZOTOLEWA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiPiAlprQZaC0j7fjbtUrj4VkZ1YAFZHwkWFCgX8j_ekm8aNfKov2QWKtYwYQeTAMw65gP0_-tJk_MAXYKpCiWCI_p3UulFzKJmUs5WWqBYQPEmCs0Jk8-Emr7M9Cm_n_ZfcZSAnjSNSPmn/s1600/Pix+1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiPiAlprQZaC0j7fjbtUrj4VkZ1YAFZHwkWFCgX8j_ekm8aNfKov2QWKtYwYQeTAMw65gP0_-tJk_MAXYKpCiWCI_p3UulFzKJmUs5WWqBYQPEmCs0Jk8-Emr7M9Cm_n_ZfcZSAnjSNSPmn/s72-c/Pix+1.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/07/waajiri-nchini-watakiwa-kufanya-uhakiki.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/07/waajiri-nchini-watakiwa-kufanya-uhakiki.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy