VIONGOZI WA DINI WATAKIWA KUTUMIA TAALUMA ZAO KUMSAIDIA RAIS DK. JOHN MAGUFULI KATIKA KULILETEA TAIFA MAENDELEO

  M uhubiri wa kimataifa 'Mama Afrika' Dk.Nicku Kyungu  akihubiri katika kongamano la kitaifa la viongozi wa dini lililofanyika...




 Muhubiri wa kimataifa 'Mama Afrika' Dk.Nicku Kyungu  akihubiri katika kongamano la kitaifa la viongozi wa dini lililofanyika Kanisa la Naoith Pentekoste Church Makuburi  Ubungo jijini Dar es Salaam leo.


 Mchungaji Dk. William Kopwe wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania  (KKKT) Dodoma, akifundisha katika kongamano hilo.

 Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya maombi hayo, Askofu Mkuu wa Naoith Pentekoste Church, Dk.David Mwasota akizungumza katika kongamano hilo.
 Mchungaji Timoth Joseph kutoka Nigeria alifundisha somo la watu kuwa waaminifu katika kila jambo.
 Mafundisho yakiendelea.


 Usikivu katika kongamano hilo
 Maombi yakifanyika.
 Maombi yakiendelea.
 Maaskofu wakiwa katika maombi.
 Maombi yakiendelea.


 Maombi yakifanyika.
  Mchungaji Timoth Joseph kutoka Nigeria akitoa zawadi ya vitabu kwa maaskofu.
Maaskofu wakiwa kwenye kongamano hilo.

Na Dotto Mwaibale

VIONGOZI wa dini wametakiwa kutumia taaluma waliyonayo kumsaidia Rais Dk. John Magufuli kuliletea taifa maendeleo na kuondokana na umaskini nchini.

Mwito huo umetolewa na muhubiri wa kimataifa 'Mama Afrika' Dk.Nicku Kyungu wakati akihubiri katika kongamano la kimataifa la viongozi wa dini lililofanyika Kanisa la Naoith Pentekoste Church Makuburi jijini Dar es Salaam leo.

Alisema viongozi wa dini waliopo katika makanisa wanataaluma mbalimbali hivyo mbali ya kuhubiri neno la mungu wanapaswa kutumia taaluma walizonazo kumsaidia Rais katika maendeleo ya nchi jambo litakalosaidia nchi kuondokana na umaskini na adui ujinga.

Dk.Kyungu alisema katika imani Tanzania sasa imetoka katika uchanga na sasa inakwenda mbele na hilo ni jambo la kujivunia.

Alisema nchi ya Tanzania imebarikiwa tangu uongozi wa baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamini Mkapa, Jakaya Kikwete na sasa Dk. John Magufuli.

"Ili ni jambo la kujivunia kwa nchi kuwa na amani tangu wakati huo hadi leo hii na ndio maana tumeona ni vizuri tukafanya maombi ya shukrani ya kuliombea taifa na Rais wetu yatakayofanyika Jumamosi Uwanja wa Uhurua jijini Dar es Salaam kuanzia asubuhi" alisema Dk. Kyungu.

Dk.Kyungu alisema kauli alioianzisha Rais Magufuli ya Hapa Kazi Tu ipo katika biblia  hivyo ni wajibu wa kila mtu kufanya kazi kama mungu alivyomuagiza adamu pale bustani ya hedeni.

Katika kongamano hilo ambalo litakwisha kesho viongozi mbalimbali wa dini na maaskofu kutoka ndani na nje ya nchi walipata fursa ya kuhubiri ambapo Mchungaji Timoth Joseph kutoka Nigeria alifundisha somo la watu kuwa waaminifu katika kila jambo.

Mchungaji Dk. William Kopwe wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania kutoka mkoani Dodoma alisema kanisa hivi sasa limeingiliwa na magonjwa likiwemo la waumini kuwanenea mabaya viongozi wao.


Maombi hayo ya shukrani kitaifa yatakayofanyika Jumamosi yameandaliwa Igo Africa for Jesus na Makanisa na Huduma za Tanzania

(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712727062)



COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: VIONGOZI WA DINI WATAKIWA KUTUMIA TAALUMA ZAO KUMSAIDIA RAIS DK. JOHN MAGUFULI KATIKA KULILETEA TAIFA MAENDELEO
VIONGOZI WA DINI WATAKIWA KUTUMIA TAALUMA ZAO KUMSAIDIA RAIS DK. JOHN MAGUFULI KATIKA KULILETEA TAIFA MAENDELEO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiL37bGK8XI1pvcBEDTa5bgpXkWDZ01zByQocD-McHCe5_y4wG2g8qzmImSUoEzDZOTSPdhXF5zjMniSYQQPFuzjFjuslEWJxXGDzUMHxjJ6GkmmYjtcxhOgSJybqCifuOlKWUTl9Nzs3bS/s640/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiL37bGK8XI1pvcBEDTa5bgpXkWDZ01zByQocD-McHCe5_y4wG2g8qzmImSUoEzDZOTSPdhXF5zjMniSYQQPFuzjFjuslEWJxXGDzUMHxjJ6GkmmYjtcxhOgSJybqCifuOlKWUTl9Nzs3bS/s72-c/1.JPG
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/07/viongozi-wa-dini-watakiwa-kutumia.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/07/viongozi-wa-dini-watakiwa-kutumia.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy