JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI IDARA YA UHAMIAJI ...
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
IDARA YA UHAMIAJI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
IDARA YA UHAMIAJI
KUISHA KWA MUDA WA ZOEZI LA UHAKIKI WA
VIBALI VYA UKAAZI KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (e-VERIFICATION)
Idara
ya Uhamiaji inapenda kuwakumbusha Waajiri, Wakurugenzi wa Makampuni, Taasisi
mbalimbali na Wageni wote kuhakikisha wamehakiki vibali vyao kupitia Mfumo wa
Uhakiki ambao unapatikana kupitia Tovuti ya Idara ya www.immigration.go.tz kabla
ya zoezi la uhakiki kuisha tarehe 19/07/2017.
Kwa
wale ambao kumbukumbu za vibali vyao hazitaonekana katika mfumo wa uhakiki au
kuwa na tatizo lolote wanashauriwa kuripoti katika Ofisi za Uhamiaji za Mikoa au
kwa Mamlaka husika ndani ya muda uliotolewa.
Baada
ya kuisha kwa muda uliotolewa, Idara itafanya ukaguzi nchi nzima na
kuwachukulia hatua za kisheria Wageni binafsi, Waajiri, Wakurugenzi wa
Makampuni na Taasisi mbalimbali ambazo wageni wao watabainika kuwa na vibali
vya kughushi au vilivyopatikana nje ya utaratibu wa utoaji vibali.
Idara
ya Uhamiaji ilitoa muda wa siku 90 kwa wale wote wenye vibali vya ukaazi kuhakiki
vibali vyao; tangu tarehe ya kuzindua mfumo huo tarehe 19 Aprili, 2017.
Imetolewa na;
KITENGO CHA UHUSIANO,
MAKAO MAKUU, IDARA YA UHAMIAJI,
14 JULAI, 2017.
COMMENTS