SPIKA NDUGAI AKUTANA NA RAIS MSTAAFU WA IRELAND NA MAMA GRACA MACHEL LEO OFISINI KWAKE MJINI DODOMA

Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akisalimiana na Mjumbe wa  “The Elders” Taasisi inayoshughulika na Amani, Haki...

IMGL7797


Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akisalimiana na Mjumbe wa  “The Elders” Taasisi inayoshughulika na Amani, Haki za Binadamu na Huduma za Afya,  Ndg. Graca Machel (kulia) katika tukio lililofanyika leo katika viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.
IMGL7800
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akisalimiana na Rais Mstaafu wa Ireland (kulia) ambae pia ni Mjumbe wa  “The Elders” Taasisi inayoshughulika na Amani, Haki za Binadamu na Huduma za Afya, Mhe. Mary Robinson katika tukio lililofanyika leo katika viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.
IMGL7813
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia)akizungumza wakati ugeni kutoka “The Elders” Taasisi inayoshughulika na Amani, Haki za Binadamu na Huduma za Afya ilipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma, katikati ni Rais Mstaafu wa Ireland ambae pia ni Mjumbe kutoka Taasisi hiyo Mhe. Mary Robinson na kushoto ni Mjumbe wa Taasisi hiyo Ndg. Graca Michel
……………………………………………………………………….
SPIKA wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai amesema Bunge litaendelea kuungana mkono jitihada za Serikali za kuboresha afya ya jamii ikiwemo uzazi salama, afya ya mama na mtoto na afya ya wazee.
Spika alitoa kauli hiyo Ofisini kwake Mjini Dodoma alipotembelewa na Rais Mstaafu wa Ireland Mheshimiwa Mary Robnson na Mama Graca Machel pamoja na ujumbe wao kutoka Taasisi ya ‘The Elderes’ ya Uingereza inayoshughulikia masuala ya Amani, Haki za Binadamu na Huduma za Afya.
Alisema siku zote Bunge limekuwa likipigania masuala mbalimbali yahusuyo afya ya jamii na kwamba ipo kamati maalamu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii ambayo inashughulikia masuala mbalimbali ikiwemo Huduma za Afya.
Alisema pia wapo wabunge mmoja mmoja ambao huyasemea masuala ya afya ya jamii na kwamba wamekuwa wakiuliza maswali mbalimbali kwa mawaziri na kujibiwa.
Kwa upande wake, Mama Machel alisema wanatambua mchango wa Tanzania katika kuboresha huduma za afya na kuishauri iendelee kufanya vizuri zaidi kwa kuongeza kipaumbele ka kile kilichowekwa  katika elimu kwa kutoa elimu bure  hadi kidato cha nne kifanyike hivyo hivyo katika sekta ya afya.
Alisisitiza pia Wabunge kuhakikisha wanatenga bajeti ya kutosha katika sekta ya afya pamoja nakupitisha sheria zitakazosaidia kuobresha sekta hiyo.
Naye Mheshimiwa Robson alisema anatambua nguvu ya Bunge katika kuhakikisha afya ya jamii inaboreshwa na kusifu juhudi za Tanzania za kuboresha elimu na sekta ya afya pia.
Mheshimiwa Robson na Mama Machel ni wajumbe wa Taasisi ya ‘The Elderes’ ya Uingereza inayoshughulikia masuala ya amani, haki za binadamu na huduma za afya.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: SPIKA NDUGAI AKUTANA NA RAIS MSTAAFU WA IRELAND NA MAMA GRACA MACHEL LEO OFISINI KWAKE MJINI DODOMA
SPIKA NDUGAI AKUTANA NA RAIS MSTAAFU WA IRELAND NA MAMA GRACA MACHEL LEO OFISINI KWAKE MJINI DODOMA
http://fullshangweblog.com/home/wp-content/uploads/2017/07/IMGL7797.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/07/spika-ndugai-akutana-na-rais-mstaafu-wa.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/07/spika-ndugai-akutana-na-rais-mstaafu-wa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy