PROF. MBARAWA ATOA MIEZI 10 KWA MKANDARASI CICO

Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mkoa wa Tabora Eng. Damian Ndibalinze, akimuonesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawa...







Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mkoa wa Tabora Eng. Damian Ndibalinze, akimuonesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, maendeleo yaliyofikiwa katika ujenzi wa barabara ya Tabora –Nyahua KM 85, wakati alipokagua ujenzi wake, Mkoani humo jana.
Muonekano wa sehemu ya KM 6 ya barabara ya Tabora–Nyahua yenye jumla ya urefu wa KM 85, inayojengwa kwa kiwango cha lami, Mkoani humo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kushoto), akitazama mchoro wa ujenzi wa kalvati itakayojengwa katika barabara ya Tabora-Sikonge yenye urefu wa KM 30, Mkoani humo jana. 


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kushoto), akitoa maelekezo kwa Mhandisi Mkazi anayesimamia ujenzi wa barabara ya Tabora-Sikonge yenye urefu wa KM 30 Eng. Golam Shahid, kumaliza mradi huo kwa viwango na ubora unaostahili, Mkoani humo jana.
Mkuu wa Wilaya ya Kaliua Bw. Abeli Busalama, akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, wakati alipokuwa akikagua barabara ya Kaliua-Kazilambwa yenye urefu wa KM 56 iliyokamilika kujengwa kwa kiwango cha lami, Mkoani humo jana.

……………………………………………………………………….

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amempa muda wa miezi kumi Mkandarasi wa Kampuni ya CICO anayejenga barabara ya Tabora-Sikonge yenye urefu wa KM 30 kwa kiwango cha lami kukamilisha kazi hiyo.

Prof. Mbarawa ameyasema hayo mkoani Tabora mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara hiyo na kuelezea kutoridhishwa na kasi ya ujenzi wake.

“Nakupa miezi kumi tangu sasa hadi mwezi Mei mwakani uwe umeikabidhi Serikali barabara hii”, amesisitiza Waziri Prof. Mbarawa.

Ameongeza kuwa ukamilishaji wa barabara hiyo uendane na viwango na ubora vinavyoendana na thamani ya fedha waliyopewa ili barabara hiyo iweze kudumu kwa muda uliopangwa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mwalimu Queen Mlozi, amemshukuru Waziri Prof. Mbarawa kwa kuufuatilia kwa karibu mradi huo ambao utachochea kasi ya maendeleo mkoani humo.

Naye, Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), mkoa wa Tabora Eng. Damian Ndabalinze, amemhakikishia Waziri Prof. Mbarawa kuwa atamsimamia mkandarasi huyo kikamilifu ili barabara hiyo ikamilike katika kipindi cha miezi kumi.

Pia, Waziri Prof. Mbarawa amekagua ujenzi wa barabara ya Tabora-Nyahua yenye urefu wa KM 85 na kumtaka mkandarasi CICO anayejenga barabara hiyo kukamilisha KM 6 zilizobaki ifikapo mwezi Oktoba mwaka huu.

Katika hatua nyingine, Prof. Mbarawa amempongeza Mkandarasi CHICO anayejenga barabara ya Kaliua-Kazilambwa yenye urefu wa KM 56 iliyokamilika kwa kiwango cha lami na kusisitiza wananchi kuilinda na kuitunza barabara hiyo kwa kutoiharibu miundombinu yake.

Ametoa nafasi nyingine kwa mkandarasi huyo kuomba kazi nyingine za ujenzi wa barabara katika maeneo mengine mbalimbali ya nchi kwani utendaji wao ni wa viwango na wanamaliza kwa wakati.

Mkuu wa Wilaya ya Kaliua Bw. Abel Busalama, ameipongeza Serikali kwa jitahada zake za kufungua Mikoa na Wilaya nchini kwa kujenga barabara za lami kwani barabara hiyo imefungua shughuli za kiuchumi na kimaendeleo wilayani kwake.

Waziri Prof. Mbarawa yupo katika ziara ya kikazi ya siku mbili ya kukagua miradi ya miundombinu iliyopo mkoani Tabora.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: PROF. MBARAWA ATOA MIEZI 10 KWA MKANDARASI CICO
PROF. MBARAWA ATOA MIEZI 10 KWA MKANDARASI CICO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgiU-aYaSRcC9OrAJaIqgnD0xjQL9JkGMnThiif24ug7C3a9qzFnuASjR7zQzIwYUkzMTCqLDkSwrY7YJJvxmtEvAGvfIyWPmhS4TCH-h7ZRO5LuCrk9Z8IvDF2HkeSMSkhTAao6tETNXI/s640/1-100.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgiU-aYaSRcC9OrAJaIqgnD0xjQL9JkGMnThiif24ug7C3a9qzFnuASjR7zQzIwYUkzMTCqLDkSwrY7YJJvxmtEvAGvfIyWPmhS4TCH-h7ZRO5LuCrk9Z8IvDF2HkeSMSkhTAao6tETNXI/s72-c/1-100.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/07/prof-mbarawa-atoa-miezi-10-kwa.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/07/prof-mbarawa-atoa-miezi-10-kwa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy