MKURUGENZI MADABA AKIFUNGUA KITUO CHA TIBA ASILI

MKURUGENZI mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Madaba mkoani Ruvuma Shafi Mpenda, amekifungia kituo cha kitengo cha utafiti wa say...


MKURUGENZI mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Madaba mkoani Ruvuma Shafi Mpenda, amekifungia kituo cha kitengo cha utafiti wa sayansi ya tiba asili na tiba mbadala kinachojishughulisha na kupima afya za binadamu na kutibu magonjwa mbalimbali cha The King Solomon of Sanitarium clinik hadi hapo wataalam wa afya watakapojiridhisha uhalali wake.

Mbali na kukifungia kituo hicho,Mpenda amesema atawachukulia hatua kali baadhi ya wataalam wake wa idara ya afya walioshiriki kutoa vibali feki vilivyohalalisha kituo hicho kufanya kazi ambayo imeonekana kama kuwatapeli wananchi.
Kwa mujibu wa Mpenda ni kwamba, kituo hicho kupitia kwa mmiliki wake Selemani Nzaganya kimekuwa kikifanya shughuli zake kinyume na taratibu ambapo hata leseni kutoka kwa baraza la tiba asili kimekwisha muda wake tangu tarehe 1 januari mwaka huu,hata hivyo bado akifanya shughuli zake bila kupata leseni mpya jambo ambalo ni kosa kinyume cha sheria.
Alisema, amelazimika kufunga kituo hicho kwa ajili ya kuokoa maisha ya wansanchi kwani hata mtu aliyekutwa akihudumia wananchi hana taaluma yoyote inayomwezesha kuhudumia wagonjwa jambo linaloonekana ni hatari kwa afya za watu.
Kwa mujibu wa Mpenda hii ni mara ya pili kufunga kituo kama hicho na ni kampeni ya kudumu kwa wale wote wanaofanya shughuli za kuwatapeli wananchi wa Madaba ambapo ametoa onyo kwa watu wengine wenye tama ya kupata fedha kwa njia ya ujanja ujanja kutafuta maeneo mengine ya kufanya shughuli zao.
Hata hivyo kwa mujibu wa majirani ambao hawakutaka kutaja majina yao,wameipongeza serikali kwa uamuzi wa kukifungia kituo hicho kwani wamiliki wake walikuwa wakiwaibia wananchi.
Walisema, kituo hicho kimekuwa sehemu ya tatizo kwa sababu hata wananchi wanaohitajika kupata ushauri na matibabu hospitalini wamekuwa wakifika katika kituo hicho kwa kuamini kwamba watapata suluhu ya matatizo yao kumbe wanazidisha ukubwa wa matizo waliyonayo.

Kwa upande wake mtu aliyekutwa akitoa huduma katika kituo hicho Ezakiel Mwakatumbula alisema, wamekuwa wanatoa huduma za matibabu kwa wa magonjwa mbalimbali hasa magonjwa sugu kwa kutumkia dawa za mimea,chakula na matunda.

Hata hivyo alikanusha kufanya shughuli zao kitapeli na kusisitiza kuwa huduma wanazotoa zimekuwa zikiwasaidia sana wananchi kuokoa maisha yao.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MKURUGENZI MADABA AKIFUNGUA KITUO CHA TIBA ASILI
MKURUGENZI MADABA AKIFUNGUA KITUO CHA TIBA ASILI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgFXpC5GDhBSuvYjBwvh4E4newr2f7jjj_IXq-vAIl70Hmuq4af6mx3e9y-fHit6ExsW4GQp-Dqs0YCKVBkZqQdlJTM9F4mG8cbqXVAYndP-hwFpunMtWlNO_sebGqlzwzqq1dpeuMX3Eg/s400/DSC00388.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgFXpC5GDhBSuvYjBwvh4E4newr2f7jjj_IXq-vAIl70Hmuq4af6mx3e9y-fHit6ExsW4GQp-Dqs0YCKVBkZqQdlJTM9F4mG8cbqXVAYndP-hwFpunMtWlNO_sebGqlzwzqq1dpeuMX3Eg/s72-c/DSC00388.JPG
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/07/mkurugenzi-madaba-akifungua-kituo-cha.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/07/mkurugenzi-madaba-akifungua-kituo-cha.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy