MKURUGENZI mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Madaba mkoani Ruvuma Shafi Mpenda, amekifungia kituo cha kitengo cha utafiti wa say...
MKURUGENZI
mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Madaba mkoani Ruvuma Shafi Mpenda,
amekifungia kituo cha kitengo cha utafiti wa sayansi ya tiba asili na
tiba mbadala kinachojishughulisha na kupima afya za binadamu na kutibu
magonjwa mbalimbali cha The King Solomon of Sanitarium clinik hadi hapo
wataalam wa afya watakapojiridhisha uhalali wake.
Mbali
na kukifungia kituo hicho,Mpenda amesema atawachukulia hatua kali
baadhi ya wataalam wake wa idara ya afya walioshiriki kutoa vibali feki
vilivyohalalisha kituo hicho kufanya kazi ambayo imeonekana kama
kuwatapeli wananchi.
Kwa
mujibu wa Mpenda ni kwamba, kituo hicho kupitia kwa mmiliki wake
Selemani Nzaganya kimekuwa kikifanya shughuli zake kinyume na taratibu
ambapo hata leseni kutoka kwa baraza la tiba asili kimekwisha muda wake
tangu tarehe 1 januari mwaka huu,hata hivyo bado akifanya shughuli zake
bila kupata leseni mpya jambo ambalo ni kosa kinyume cha sheria.
Alisema,
amelazimika kufunga kituo hicho kwa ajili ya kuokoa maisha ya wansanchi
kwani hata mtu aliyekutwa akihudumia wananchi hana taaluma yoyote
inayomwezesha kuhudumia wagonjwa jambo linaloonekana ni hatari kwa afya
za watu.
Kwa
mujibu wa Mpenda hii ni mara ya pili kufunga kituo kama hicho na ni
kampeni ya kudumu kwa wale wote wanaofanya shughuli za kuwatapeli
wananchi wa Madaba ambapo ametoa onyo kwa watu wengine wenye tama ya
kupata fedha kwa njia ya ujanja ujanja kutafuta maeneo mengine ya
kufanya shughuli zao.
Hata
hivyo kwa mujibu wa majirani ambao hawakutaka kutaja majina
yao,wameipongeza serikali kwa uamuzi wa kukifungia kituo hicho kwani
wamiliki wake walikuwa wakiwaibia wananchi.
Walisema,
kituo hicho kimekuwa sehemu ya tatizo kwa sababu hata wananchi
wanaohitajika kupata ushauri na matibabu hospitalini wamekuwa wakifika
katika kituo hicho kwa kuamini kwamba watapata suluhu ya matatizo yao
kumbe wanazidisha ukubwa wa matizo waliyonayo.
Kwa
upande wake mtu aliyekutwa akitoa huduma katika kituo hicho Ezakiel
Mwakatumbula alisema, wamekuwa wanatoa huduma za matibabu kwa wa
magonjwa mbalimbali hasa magonjwa sugu kwa kutumkia dawa za
mimea,chakula na matunda.
Hata
hivyo alikanusha kufanya shughuli zao kitapeli na kusisitiza kuwa huduma
wanazotoa zimekuwa zikiwasaidia sana wananchi kuokoa maisha yao.
COMMENTS