MEYA WA JIJI LA DAR MWITA AWATAKA WANANCHI KUWA WAMOJA BILA KUJALI TOFAUTI ZA ITIKADI ZA VYAMA VYAO

NA CHRISTINA MWAGALA ,OFISI YA MEYA WA JIJI MSTAHIKI Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita amesema watanzania hawajafikia hat...


NA CHRISTINA MWAGALA ,OFISI YA MEYA WA JIJI

MSTAHIKI Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita amesema watanzania hawajafikia hatua ya kubaguana kwa kiitikadi ya vyama, Dini, Kabila badala yake wote wanapaswa kutangaza hali ya Umoja, Upendo na Mshikamano katika nchi yao.

Meya Mwita alitoa kauli hiyo jijini hapa jana, wakati wa harambee ya uchangiaji wa ujenzi wa Kanisa la kisasa la Tanzania Assemblies Of God (TAG) lililopo Kivule ,Halmashauri ya Manispaa ya Ilala jijini hapa ambapo pamoja na mambo mengine alisema kuwa watanzania wanapaswa kuwa wamoja ili nchi iendelee kuwa na amani.

Alisema yapo mambo mbalimbali ambayo yanajitokeza ndani ya nchi ambapo kama watanzania , kwakushirikiana na viongozi wa dini kwa pamaoja wanapaswa kusimama na kuliombea Taifa ili kuendelea kudumisha amani iliyopo.

" Tangu nimezaliwa sijawahi kushuhudia vita, machafuko katika nchi yetu, kikubwa huwa naona amani iliyotawala, Upendo, na umoja , sasa nawasishi sana ndugu zangu tuendelee kuwa wamoja tusibaguane, kwa namna yoyote ile , ili nchi yetu iendelee kuwa na amani" alisema Meya Mwita.

"Baba wataifa Hayati Mwalim Julius Nyerere enzi ya uhali wake alikuwa akisisitiza sana kulinda amani ya nchi yetu, na sisi ambao tupo hai hadi sasa , mambo ya vyama, Udini, Ukabila tuweke pembeni tusimame kama Taifa moja.

Awali akijibu risala iliyoandaliwa na uongozi wa kanisa hilo, Meya Mwita aliahidi kuchangia katika ujenzi huo mifuko 100 ya Simenti na kiasi cha Fedha shilingi 500,000 huku aliwataka waumini wa kanisa hilo kujitolea ili kufanikisha ujenzi huo.

Risala hiyo ilieleza kujenga kanisa la kisasa lenye uwezo wa kuchukua waumini 600 ambapo jumla ya shilingi milioni 95 zinahitajika ili kukamilisha ujenzi huo.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MEYA WA JIJI LA DAR MWITA AWATAKA WANANCHI KUWA WAMOJA BILA KUJALI TOFAUTI ZA ITIKADI ZA VYAMA VYAO
MEYA WA JIJI LA DAR MWITA AWATAKA WANANCHI KUWA WAMOJA BILA KUJALI TOFAUTI ZA ITIKADI ZA VYAMA VYAO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhgix14aiJ8kTK1PdV5K0KGnXrz40pcH4j7TmoHAvfXXZKelQx2Qg8qrNhscCOgJ_gqwevAwRyKD4Qi4cax9wXrEd6d9BJ7u3AILBM-fxWffFu1B8ohbPekLivRbtHs1nUh24PvfARG_KQ/s400/MEYA+CHARLES.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhgix14aiJ8kTK1PdV5K0KGnXrz40pcH4j7TmoHAvfXXZKelQx2Qg8qrNhscCOgJ_gqwevAwRyKD4Qi4cax9wXrEd6d9BJ7u3AILBM-fxWffFu1B8ohbPekLivRbtHs1nUh24PvfARG_KQ/s72-c/MEYA+CHARLES.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/07/meya-wa-jiji-la-dar-mwita-awataka.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/07/meya-wa-jiji-la-dar-mwita-awataka.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy