Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad M...
Mwenyekiti
wa Taifa wa Baraza la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akiongoza
maandamano ya Mabalozi wa Usalama Barabarani kuingia Uwanja wa Mashujaa,
wakiadhimisha siku yao iliyofanyika kitaifa mkoani Dodoma. Kulia ni
Katibu Mtendaji wa baraza hilo,Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani
nchini, DCP Mohamed Mpinga. (Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)
Mwenyekiti
wa Taifa wa Baraza la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni,akizungumza
wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mabalozi wa Usalama Barabarani ambapo
aliwaasa madereva kufuata sheria ili kuweza kupunguza tatizo la ajali za
barabarani ambazo zimekuwa zikisababisha vifo na kuacha idadi kubwa ya
wahanga wa ajali hizo.Wapili kushoto ni Katibu Mtendaji wa baraza
hilo,Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, DCP Mohamed Mpinga na
anayefuatia ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa.
Maadhimisho hayo yamefanyika kitaifa Uwanja wa Mashujaa, leo mkoani
Dodoma.
Katibu
Mtendaji wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ambae pia ni Mkuu wa
Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,DCP Mohamed Mpinga, akizungumza
wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mabalozi wa Usalama Barabarani ambapo
aliwaasa askari wa usalama barabarani kusimamia sheria ili kuweza
kupunguza tatizo la ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikisababisha
vifo na kuacha idadi kubwa ya wahanga wa ajali hizo.Kulia ni Mwenyekiti
wa Taifa wa Baraza la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni na kulia ni
Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma,Lazaro Mambosasa. Maadhimisho hayo
yamefanyika kitaifa Uwanja wa Mashujaa,leo mkoani Dodoma.
Kamanda
wa Polisi mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambo sasa akizungumza wakati wa
Maadhimisho ya Siku ya Mabalozi wa Usalama Barabarani ambapo
aliwashukuru mabalozi hao kuchagua mkoa wa Dodoma kufanyia maadhimisho
hayo na kuahidi kuelimisha watumiaji wa vyombo vya moto sheria na kanuni
za usalama barabarani ikiwa anaongoza mkoa ambao ni Makao Makuu ya nchi
.Wakwanza kushoto ni Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Usalama
Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,
Mhandisi Hamad Masauni na kulia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la
Usalama Barabarani ambae pia ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani
nchini, DCP Mohamed Mpinga. Maadhimisho hayo yamefanyika kitaifa Uwanja wa
Mashujaa, leo mkoani Dodoma.
Mabalozi
wa Usalama wa Barabarani wakifuatilia hotuba ya Mwenyekiti wa Taifa wa
Baraza la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo
ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani) wakati wa
Maadhimisho ya Siku ya Mabalozi wa Usalama Barabarani ambapo aliwaasa
madereva kufuata sheria ili kuweza kupunguza tatizo la ajali za
barabarani ambazo zimekuwa zikisababisha vifo na kuacha idadi kubwa ya
wahanga wa ajali hizo. Maadhimisho hayo yamefanyika kitaifa Uwanja wa
Mashujaa, leo mkoani Dodoma.
Msanii
Faustine Matina ambae ni Balozi wa Usalama Barabarani, akiimba wimbo wa
kuhimiza masuala ya kuzingatia sheria za usalama barabarani wakati wa
Siku ya Maadhimisho ya Mabalozi wa Usalama Barabarani, iliyofanyika
kitaifa leo katika Uwanja wa Mashujaa, mkoani Dodoma.
Mhanga
wa ajali anayefahamika kwa jina la Mpemba Asilia, akizungumza na
Mabalozi wa Usalama Barabarani, alipofika katikaMaadhimisho ya Mabalozi
wa Usalama Barabarani yaliyofanyika kitaifa leo katika Uwanja wa
Mashujaa,mkoani Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Mwenyekiti
wa Taifa wa Baraza la Usalama Barabarani ambaye pia ni Naibu Waziri
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (watano
kulia),akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Mabalozi wa Usalama
Barabarani wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mabalozi wa Usalama
Barabarani yaliyofanyika kitaifa Uwanja wa Mashujaa,leo mkoani
Dodoma.Wasita kulia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Usalama
Barabarani ambae pia ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, DCP
Mohamed Mpinga
COMMENTS