Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro akisikiliza maelekezo ya jinsi inavyotumika moja ya magari manne waliyokabidhiwa...
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini
(IGP), Simon Sirro akisikiliza maelekezo ya jinsi inavyotumika moja ya
magari manne waliyokabidhiwa na Kampuni ya utengenezaji magari ya
Haval kutoka China, ambaye ni Meneja wa Kampuni ya Kifaru, Mario Gaspari.Hafla
hiyo imefanyika Julai 5, 2017 katika ukumbi wa mikutano wa Polisi Oysterbay ijini
Dar es Salaam.
Mkuuwa Jeshi la Polisi nchini
(IGP), Simon Sirro na Meneja Mkuu wa kampuni ya utengenezaji magari ya
Haval kutroka China, Bw.Jianguo Liu wakikata utepe kuashiria kukabidhiwa magari manne
yaliyotolewa na kampuni hiyo ikiwa ni juhudi zake katika kulisaidia
Jeshi la Polisi kupambana na uhalifu nchini.Hafla hiyo imefanyika
katika Ukumbi wa Mikutano wa Polisi, Oysterbay jijini Dar es Salaam
Mkuuwa Jeshi la Polisi nchini
(IGP), Simon
Sirro akikagua moja ya magari hayo.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini
(IGP), Simon
Sirro akitoa hotuba yake.
Meneja
wa Kampuni ya utengenezaji magari ya Haval, Jianguo
Liu, akizungumza wakati wa Hafla ya makabidhiano ya magari manne
yaliyotolewa na kampuni hiyo ambapo aliahidi kushirikiana na Jeshi
la Polisi katika vita
ya kupambana na uhalifu nchini.Kushoto aliyesimama ni mkalimani wa lugha
ya Kichina. Hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa mikutano wa
Polisi, Oysterbay, jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini
(IGP), Simon
Sirro akipita mbele ya magari manne yaliyotolewa na Kampuni ya utengenezaji magari ya Haval,
ambapo aliishukuru kampuni hiyo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi katika
vita ya kupambana na uhalifu.Hafla hiyo imefanyika Julai 5, 2017 katika ukumbi wa mikutano wa
Polisi, Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini
(IGP), Simon Sirro(wanne kulia),
akiwa katika picha ya pamoja na Meneja wa Kampuni ya utengenezaji magari
ya Haval, Jianguo
Liu,(watatu kushoto),baada ya makabidhiano ya magari manne kutoka
kwakampuni hiyo ikiwa ni mchango wao katika kulisaidia Jeshi
la Polisi katika
kupambana na uhalifu nchini.Wengine ni viongozi wa juu wa jeshi na
viongozi wa kampuni ya Haval kutoka China. Hafla hiyo imefanyika Julai 5, 2017 katika ukumbi wa Mikutano wa Polisi, Oysterbay, jijini
Dar es Salaam. (Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)
COMMENTS