WAZIRI MAGHEMBE AZINDUWA MRADI WA UHIFADHI NA IKLOJIA YA SECAD

Na Hamza Temba Wizara ya Maliasili na Utalii Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe kwa kushirikiana na balozi wa Ujer...

Na Hamza Temba Wizara ya Maliasili na Utalii


Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe kwa kushirikiana na balozi wa Ujerumani hapa nchini, Egon Konchanke amezindua Mradi wa Uhifadhi na Maendeleo ya Ikolojia ya Pori la akiba la Selous SECAD (Selous Ecosytem Conservation and Development Program) ambao umefadhiliwa na Serikali ya Ujerumani kwa ushirikiano na Serikali ya Tanzania, mradi huo utatekelezwa na Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA, WWF (World Wildlife Fund) na FZS (Frankfurt Zoological Society).

Akizungumza katika hafla iliyofanyika jana, Matembwe Selous, Mkoani Morogoro, Waziri Maghembe alisema Serikali ya Ujerumani kupitia benki ya  ya KFW imechangia Euro Mil. 18 (sawa na Shilingi Bil. 45.124) katika mradi huo utakaodumu kwa miaka mitano huku mashirika ya WWF (World Wildlife Fund) na FZS (Frankfurt Zoological Society) yakichangia Euro laki 4 kila moja (sawa na Shilingi bil. 1.8). Pamoja na uzinduzi huo alizindua pia Mpango Kazi wa Dharura wa miaka mitano wa kuendeleza pori hilo.

"Mradi huu ni muhimu sana kwakua utasaidia kuongeza nguvu kwenye jitihada zetu za kuendeleza na kuimarisha hifadhi ya pori hili la Selous ikiwemo upatikanaji wa vitendea kazi pamoja na kutuongezea nguvu kwenye mapambano dhidi ya ujangili", alisema Prof. Maghembe.

Alisema jitihada ambazo Serikali imeshazifanya katika pori hilo ni pamoja na kuimarisha doria za ndege zenye rubani na zisizo na rubani (drones), kutoa mafunzo ya jeshi usu kwa askari, kuongeza maaskari pamoja na vitendea kazi ambapo katika mwaka ujao wa fedha Serikali itatoa magari mengine 15 kusaidia pori hilo.

"Pamoja na jitihada hizo tuna mpango wa kuwekeza dola za kimarekani Milioni 156 (sawa na Shilingi bilioni 352.560) kwa ajili ya kuboresha pori hili (Selous), Ruaha, Mikumi, Ruangwa na Kitulo kuhakikisha watalii wanatembelea maeneo haya na kuondoa kile kikwazo cha wao kutotembelea hifadhi za kusini, hiyo inaenda sambamba na kuimarishwa kwa shirika la ndege la Serikali la Air Tanzania kuondoa changamoto iliyokuwepo ya usafiri wa anga", alisema Prof. Maghembe. 

Akizungumzia changamoto ya ujangili katika pori hilo alisema Serikali imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kupambana na tatizo hilo ambapo majangili wengi wameshakamatwa katika maeneo ya Tunduru, Namtumbo na maeneo ya katikati ya Selous. Alisema changamoto hiyo bado ipo katika maeneo ya Mkoa wa Ruvuma ambapo imeripotiwa na kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa huo kuwa kuna upatikanaji wa silaha za kivita kutoka nchini Msumbiji ambazo zinapatikana kwa watu kubadilishana na magunia ya mchele changamoto ambayo inaendelea kufanyiwa kazi.

Wakati huo huo, Prof. Maghembe akijibu swali aliloulizwa na wanahabari kuhusu hatua iliyofikiwa juu ya  kauli aliyoitoa bungeni hivi karibuni ya kuunganisha taasisi zote za uhifadhi nchini alisema, tayari ameshaunda kamati ya watu sita ikiongozwa na Mkuu wa Chuo cha Wanyamapori Mweka, Prof. Kidegesho  kwa ajili kuangalia namna bora ya kutekeleza azma hiyo. "Tayari kamati hiyo imeshaanza kazi na itaonana na wadau mbalimbali kupata maoni yao na katika kipindi cha mwezi na nusu watatuletea ripoti", alisema.

Kwa upande wake Balozi Konchanke alimuahakikishia Prof. Maghembe kuwa Serikali ya Ujerumani itaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoikabili hifadhi hiyo ikiwemo ubovu wa miundombinu na uvamizi  pori hilo kwa faida ya jamii kwa ujumla. Aidha, alitoa wito kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA kubuni mbinu mpya  za kukabiliana na changamoto zilizopo.

Meja Jenerali Gaudence Milanzi ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, yeye alisema "Serikali kwa kushirikiana na wadau wa uhifadhi imefanya kazi kubwa kuhakikisha Selous haiondolewi katika orodha ya maeneo ya urithi wa dunia yaliyopo hatarini kutoweka,  hiyo ni pamoja na kunzishwa kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyanapori Tanzania TAWA, kuanzishwa kwa mkakati wa kitaifa wa kukabiliana na ujangili na miradi mbali ukiwemo huu wa SECAD uliozinduliwa leo ambayo kwa kiasi kikubwa imeasaidia katika kuendesha hifadhi zetu pamoja na kusaidia kwenye mapambano dhidi ya ujangili".

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania, TAWA, Martin Loibooki aliishukuru Serikali ya Ujerumani kwa mradi huo na kusema kuwa utasaidia kwa kiasi kikubwa kukabiliana na changamoto mbalimbali katika pori hilo ikiwemo ya uhaba wa vitendea kazi na ujangili na hivyo kuifanya hifadhi hiyo iendelee kuwa miongoni mwa maeneo ya urithi wa dunia.

Pori la Akiba la Selous ni hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania ikiwa ukubwa wa Kilomita za mraba 50,000. Hifadhi hiyo ambayo ipo katika mikoa ya Morogoro, Pwani, Lindi, Mtwara na Ruvuma ina vivutio vingi vya utalii na inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo miundombinu ya barabara za kuingia katika hifadhi hiyo, ujangili, rasilimali watu na vitendea kazi. 


Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akimkabidhi Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori wa Wizara hiyo, Prof. Alexander Songorwa Mpango Kazi wa Dharura wa Kuendeleza Pori la Akiba la Selous baada ya kuuzindua sambamba na mradi wa Kuendeleza Uhifadhi wa Ikolojia ya Pori la Akiba la Selous (SECAD) wenye thamani ya Euro Mil. 18 sawa na Shilingi Bil. 45.124 ambao umefadhiliwa na Serkali ya Ujerumani kwa ushirikiano na Serikali ya Tanzania  katika hafla iliyofanyika tarehe 17 Juni, 2017 Matambwe, Selous Mkoani Morogoro. Kulia kwake ni Balozi wa Ujerumani, Egon Konchanke, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Gaudence Milanzi, Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Prof. Faustin Kamuzora na Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania, Martin Loibooki. (Picha na Hamza Temba - WMU).


Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kulia) akizindua Mradi wa Kuendeleza Uhifadhi wa Ikolojia ya Pori la Akiba la Selous (SECAD) wenye thamani ya Euro Mil. 18 sawa na Shilingi Bil. 45.124 ambao umefadhiliwa na Serikali ya Ujerumani kwa ushirikiano na Serikali ya Tanzania katika hafla iliyofanyika tarehe 17 Juni, 2017 Matambwe, Selous Mkoani Morogoro. Wanaoshudia kulia kwake ni Balozi wa Ujerumani, Egon Konchanke, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili, Meja Jenerali Gaudence Milanzi na Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, Prof. Faustin Kamuzora.


Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kushoto) na  Balozi wa Ujerumani hapa nchini, Egon Konchanke wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa magari sita aina ya Land Cruiser ambayo ni sehemu ya Mradi uliozinduliwa wa Kuendeleza Uhifadhi wa Ikolojia ya Pori la Akiba la Selous (SECAD) wenye thamani ya Euro Mil. 18 sawa na Shilingi Bil. 45.124 ambao umefadhiliwa na Serikali ya Ujerumani kwa ushirikiano na Serikali ya Tanzania katika hafla iliyofanyika tarehe 17 Juni, 2017 Matambwe, Selous Mkoani Morogoro.


Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe akijaribu moja ya gari baada ya uzinduzi wa magari sita aina ya Land Cruiser ambayo ni sehemu ya Mradi uliozinduliwa wa Kuendeleza Uhifadhi wa Ikolojia ya Pori la Akiba la Selous (SECAD) wenye thamani ya Euro Mil. 18 sawa na Shilingi Bil. 45.124 ambao umefadhiliwa na Serikali ya Ujerumani kwa ushirikiano na Serikali ya Tanzania katika hafla iliyofanyika tarehe 17 Juni, 2017 Matambwe, Selous Mkoani Morogoro.

 

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAZIRI MAGHEMBE AZINDUWA MRADI WA UHIFADHI NA IKLOJIA YA SECAD
WAZIRI MAGHEMBE AZINDUWA MRADI WA UHIFADHI NA IKLOJIA YA SECAD
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhA-2TNnvocxrbDutJ3I23ukKFRTTp-M-dP9DefOCpKjzkgjueE3U5BS-XQhyphenhyphenpu6-VNiQf_Y7BHlofMZDnwFPbGuhyZDgzxn50NnGS23v4I8wI1nDT1-_tEzRY9GlsU03SbILY0C3wmN5I/s640/1%252813%2529.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhA-2TNnvocxrbDutJ3I23ukKFRTTp-M-dP9DefOCpKjzkgjueE3U5BS-XQhyphenhyphenpu6-VNiQf_Y7BHlofMZDnwFPbGuhyZDgzxn50NnGS23v4I8wI1nDT1-_tEzRY9GlsU03SbILY0C3wmN5I/s72-c/1%252813%2529.JPG
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/waziri-maghembe-azinduwa-mradi-wa.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/waziri-maghembe-azinduwa-mradi-wa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy