WAZIRI LUKUVI KUPEWA TUZO YA UWAJIBIKAJI NA UTENDAJ BORA

Na Jonas Kamaleki- MAELEZO. Viongozi wa Dini wanajiandaa kumpa tuzo Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Will...


Na Jonas Kamaleki- MAELEZO.

Viongozi wa Dini wanajiandaa kumpa tuzo Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi kwa utendaji mzuri uliojaa ubunifu na uwajibikaji.

Hayo yameelezwa katika mahojiano maalum jijini Dar es salaam na Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Maadili na Haki za Binadamu kwa Jamii ya Dini zote Tanzania, Askofu William Mwamalanga.

Askofu Mwamalanga amesema kuwa Waziri Lukuvi amekuwa kiongozi imara katika kufuatilia masuala yanayohusu ardhi ikiwemo utatuzi wa migogoro ambayo imedumu kwa muda mrefu.
“Lukuvi ameing’arisha Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuendana na kasi ya Rais John Pombe Magufuli, hakika amevaa viatu vya Magufuli, hivyo tumeamua kumpa tuzo maalum kwa ajili utendaji wake”, alisema Askofu Mwamalanga.
Ameeleza kuwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imefanya jambo zuri kwa kutoa elimu ya ardhi kiasi kwamba karibu kila mtu amefahamu matumizi ya ardhi na umuhimu wake.
Askofu Mwamalanga amesema kuwa ardhi imefanywa kuwa lulu na kufanya sura mpya ya ardhi kuonekana ambapo takriban asilimia 85 ya Watanzania wameiona kuwa ni mali.
Mhe. Lukuvi amewapa nafasi ya kwanza wananchi kuliko Sheria jambo ambalo limewafanya Watanzania kujisikia kuwa wanathaminiwa na Serikali yao, aliongeza Askofu Mwamalanga.
Kiongozi huyo wa Dini amesema kuwa Mhe. Lukuvi ni mfano wa kuigwa na mawaziri na viongozi wenzake kwa uchapakazi wake. Amesema kuwa ni Waziri ambaye anawashirikisha watendaji waliochini yake katika maamuzi mbali mbali, hivyo anastahili kupewa tuzo.
“Tumepanga kumpa tuzo Waziri Lukuvi kwa kuzingatia yafuatayo: Kuiweka ardhi mikononi mwa watanzania, kuonyesha kuwa ardhi ni chanzo kikuu cha uchumi wa watu na utatuzi wa migogoro ya ardhi hasa iliyodumu kwa muda mrefu”, alisema Askofu Mwamalanga. 
Migogoro hiyo ni kama vile mgogoro wa kijiji cha Mabwegere, Mkoani Morogoro, mgogoro wa Chasimba, jijini Dar es Salaam na migogoro mingine mingi katika mikoa ya Arusha, Mbeya, Kigoma, Tanga na Mwanza.
Askofu Mwamalanga amesema Kamati yake imewasiliana na Taasisi mbalimbali za Serikali na binafsi ili watoe mapendekezo ya tuzo ambayo anastahili kupewa Mhe. Lukuvi kwa utendaji kazi wake mzuri. 
Amezitaja baadhi ya Taasisi hizo kuwa ni Vyuo Vikuu vya Umma na Binafsi, Marais wastaafu na mawaziri wakuu wastaafu, Vyama vyote vya siasa ambavyo kwa ujumla wake vimeonyesha kutambua mchango wa waziri Lukuvi.
Baada ya kupokea mapendekezo na kuyafanyia kazi ndipo itatangazwa siku ya kutoa tuzo hiyo kwa Mhe. Lukuvi, alisema Askofu Mwamalanga.

Tangu Waziri Lukuvi aiongoze Wizara ya ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi mwisho mwa uongozi wa awamu ya Nne hadi sasa, 
mabadiliko yenye tija katika wizara hiyo yameonekana. Migogoro mingi ya ardhi imetatuliwa, utoaji wa hati za viwanja umerahisishwa na huduma kwa wateja imeboreshwa.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAZIRI LUKUVI KUPEWA TUZO YA UWAJIBIKAJI NA UTENDAJ BORA
WAZIRI LUKUVI KUPEWA TUZO YA UWAJIBIKAJI NA UTENDAJ BORA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjdxcS2b52QOX5wogd-BcGbGOCbYpP2pFKAYKBLaiZ7RpR5j9lr-Q-a4uTHLprc2ZE3MhYeBUtvMmoAf-_44DMf00agvKkxVSv6ycoLsXz64gSXVcR7m-5FNRmCwpd8zEteQjIKeYvQamo/s400/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjdxcS2b52QOX5wogd-BcGbGOCbYpP2pFKAYKBLaiZ7RpR5j9lr-Q-a4uTHLprc2ZE3MhYeBUtvMmoAf-_44DMf00agvKkxVSv6ycoLsXz64gSXVcR7m-5FNRmCwpd8zEteQjIKeYvQamo/s72-c/1.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/waziri-lukuvi-kupewa-tuzo-ya.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/waziri-lukuvi-kupewa-tuzo-ya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy