WATUMISHI OFISI YA WAZIRI MKUU WAASWA KUFANYA KAZI KWA UADILIFU

Na Mwandishi Wetu Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wameaswa kufanya kazi kwa uadilifu kwa kuzingatia maadili na utendaji katika Utumis...


Na Mwandishi Wetu
Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wameaswa kufanya kazi kwa uadilifu kwa kuzingatia maadili na utendaji katika Utumishi wa Umma wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma.
Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera na Uratibu Dkt. Hamisi Mwinyimvua alipokutana na wafanyakazi wa ofisi yake Dodoma kwa lengo la kuiadhimisha Wiki hiyo inayofanyika kila mwaka kuanzia Juni 16-23 Barani Afrika ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni “Kuimarisha Ushirikishwaji wa Jamii katika Utoaji Huduma: Vijana washirikishwe kuleta Mabadiliko Barani Afrika”.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Dkt. Hamisi Mwinyimvua akifafanua jambo kwa watumishi wa ofisi yake (hawapo pichani) wakati wa maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma yenye kauli mbiu “Kuimarisha Ushirikishwaji wa Jamii katika Utoaji Huduma: Vijana washirikishwe kuleta Mabadiliko Barani Afrika” Waliyoadhimishi Dodoma Juni 22, 2017 kulia aliyekaa ni Katibu Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge), Maimuna Tarishi.
“Kila mtumishi wa umma anapaswa kuwa mwadilifu na mchapakazi hivyo niwaombe watumishi wote muwe mfano kwa kuwa waadilifu katika utendaji wenu kwa kuzingatia sheria zote za utumishi wa umma ili kuisaidia Serikali na kuwafikia wananchi kiujumla.”alieleza Dkt.Mwinyimvua
Katika kuiadhimisha wiki hii ya utumishi wa Umma ni wakati pekee wa kujitathimini eneo la kiutendaji na kuona maeneo yenye mapungufu ili yafanyiwe maboresho kwa haraka lengo likiwa kuondokana na mazoea yaliyokuwepo na kuendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu, Issa Nchansi amewataka watumishi  kuzingatia mambo nane muhimu yaliyoainishwa katika Kanuni za Maadili ya Utendaji katika Utumishi wa Umma ikiwemo; Utoaji wa huduma bora, Utii kwa Serikali, bidii ya kazi, kutoa huduma bila upendeleo, uwajibikaji kwa umma,kuheshimu sheria, matumizi sahihi ya taarifa na uadilifu sehemu ya kazi.
Naye, Katibu Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge) Bi. Maimuna Tarishi aliwaomba watumishi wote kuzingatia kauli mbiu ya mwaka huu kwa kuwawezesha vijana kielimu, kiuchumi na kijamii ili waweze kuzalisha na kuwa tegemeo la taifa.
“Niwaombe watumishi wote kuiangalia hili kundi la vijana wanaoajiriwa na Serikali kwa kuwatia moyo na kuwaunga mkono katika utekelezaji wa kazi zao” alisisitiza Tarishi
Sambamba na hili, Katibu Mkuu, Tarishi alisema  kuwa ili kuwe na utendaji wenye matokeo lazima kuitumia wiki hii kukumbushana majukumu na nafasi zetu katika kuitumikia serikali.
“Tuwe na utendaji wenye matokeo na si kuhesabu siku, miezi hadi mwaka bali tuwajibike kwa uadilifu kila muda tuwapo Serikalini.”
Baadhi ya watumishi Ofisi ya Waziri Mkuu wakimsikiliza Katibu Mkuu (Sera na Uratibu) Dkt. Hamisi Mwinyimvua (hayupo pichani) wakati wa mkutano uliofanyika Ukumbi wa Mikutano ofisi hiyo Dodoma ili kuadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma inayoendelea Barani Afrika.

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu Ofisi ya Waziri Mkuu Bw.Issa Nchansi akieleza kanuni za maadili kiutendaji kwa watumishi wa ofisi hiyo wakati wa kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma walipokutana na watumishi wote Dodoma ili kujadili masuala ya kiutumishi Juni 22, 2017.

Mchumi Idara ya Uratibu wa Shughuli za Serikali Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Novatus Tesha akisoma Kanuni za Maadili ya Utendaji Katika Utumishi wa Umma wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambapo ofisi hiyo imeadhimisha kwa kukutana na watumishi wake kujadili masuala ya msingi ya kiutumishi Juni 22, 2017.

Msaidizi wa Waziri Mkuu (Hotuba) Bw. Abdalah Mtibora akiuliza swali kwa Mwenyekiti wa mkutano (hayupo pichani) wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma tarehe 22Juni, 2017.

Mhasibu Ofisi ya Waziri Mkuu Bi.Kissa Mwakipesile akieleza hoja yake kwa Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu ofisi hiyo, Issa Nchansi (hayupo pichani) wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika Juni 22, 2017 Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi hiyo Dodoma.

Afisa Tehama Ofisi ya Waziri Mkuu, Innocent Mboya akifafanua jambo kwa washiriki wa mkutano wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika Juni 22, 2017 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi hiyo Dodoma.


Katibu Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge) Maimuna Tarishi akifunga mkutano wa wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma wakati wa kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma inayoadhimishwa kila mwaka kuanzia tarehe 16-23 Juni Barani Afrika.
(PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU-DODOMA)






COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WATUMISHI OFISI YA WAZIRI MKUU WAASWA KUFANYA KAZI KWA UADILIFU
WATUMISHI OFISI YA WAZIRI MKUU WAASWA KUFANYA KAZI KWA UADILIFU
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiAQ75UwHjaDRauZ-q9ifbOapwh7zn6BxrPe1CAqoGpqnk_unlLdpqMwywtPgnEt4WwNMgOf0lpIOMhYDjRDEYDaAUa6k93lo7Mcul2FzRDCgvM15xm4ieehSGFaUnMpr6rOwUrDQ3r1Gk/s640/N1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiAQ75UwHjaDRauZ-q9ifbOapwh7zn6BxrPe1CAqoGpqnk_unlLdpqMwywtPgnEt4WwNMgOf0lpIOMhYDjRDEYDaAUa6k93lo7Mcul2FzRDCgvM15xm4ieehSGFaUnMpr6rOwUrDQ3r1Gk/s72-c/N1.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/watumishi-ofisi-ya-waziri-mkuu-waaswa.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/watumishi-ofisi-ya-waziri-mkuu-waaswa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy