· Jumla ya wateja Milioni 7 wananufaika na gawio hilo nchi nzima · Gawio hilo unaendana na matakwa ya Benki kuu ya Ta...
·
Jumla ya wateja Milioni 7 wananufaika na gawio hilo nchi nzima
·
Gawio hilo unaendana na matakwa ya Benki kuu ya Tanzania (BoT)
Na Mwandishi Wetu
Dar es Salaam,
Wateja wa Vodacom Tanzania PLC ambao ni watumiaji wa huduma ya kifedha
ya
M-Pesa wameanza kunufaika na gawio la shilingi bilioni 7.9.Gawio hilo
limeanza kuwanufaisha jumla ya watumiaji milioni saba wa huduma ya
M-Pesa nchi nzima.
Utoaji
wa gawio unaendana na matakwa ya Benki kuu ya Tanzania. Hadi sasa
Vodacom tayari imeshatoa jumla ya shilingi bilioni 80 kama gawio ambalo
huhifadhiwa kwenye akaunti
maalum ya M-Pesa Trust iliyopo kwenye benki za biashara hapa nchini.
Kabla
ya gawio la sasa, jumla ya Tsh bilioni 72 zilishagawiwa katika awamu
tofauti tangu kampuni hii ianze utaratibu wa kutoa gawio Mwezi Disemba
2016. Utoaji wa gawio
hufanyika kila baada ya miezi mitatu na gawio la sasa ni kwa ajili ya
robo ya kwanza ya mwaka 2017.
Akiongea
na waandishi wa habari Mkurugenzi wa biashara ya mtandao wa kampuni
hiyo,Sitoyo Lopokoiyit alisema “M-Pesa inamwezesha kila mteja kupata
huduma ya kifedha. Tunapojitahidi
kumfikia kila Mtanzania, tunaendelea kutoa huduma bora na za kisasa
zinazoziwezesha Serikali na biashara kufanya kazi pamoja na huku tukitoa
faida nono kwa mawakala na wabia wetu,” alisema
Mkurugenzi
huyo aliwaasa wateja ambao tayari wameanza kunufaika na gawio hili
kutumia fedha hizo kununua Ukarimu bando ili waweze kunufaika zaidi
kimawasiliano kwa wakati
huu wa mwezi mtukufu wa Ramadhani pamoja na kufanya malipo ya moja kwa
moja kutoka kwenye simu zao wanaponunua bidhaa na huduma mbali mbali na
kusititiza kwamba kwa sasa kuna mamia ya wakala wanaopokea malipo kwa
njia ya M-Pesa na APP mpya ya M-Pesa imefanya
malipo kuwa rahisi zaidi.
Lopokoiyit alifafanua kuwa, kiasi ambacho mteja anapokea kama gawio hutegemeana na matumizi yake
kupitia huduma ya M-Pesa kama kutuma pesa, kununua muda wa maongezi, kulipa huduma na bidhaa pamoja na nyingine.
Alisema
Vodacom itaendelea na jitihada za kuboresha maisha ya wateja wake
kupitia huduma mbali mbali mbali na kuwataka wateja wa Vodacom kuendelea
kutumia huduma ya M-Pesa ili waweze
kunufaika na mambo mbali mbali ikiwamo gawio.
COMMENTS