Na Mwandishi wetu – JKCI Viongozi wa mashirika ya Umma na Binafsi wametakiwa kujenga mazoea ya kupima afya zao mara kwa mara i...
Na Mwandishi wetu – JKCI
Viongozi
wa mashirika ya Umma na Binafsi wametakiwa kujenga mazoea ya kupima
afya zao mara kwa mara ili kufahamu kama wana magonjwa yanayowasumbua
au la na kwa kufanya hivyo wataweza kupata matibabu kwa wakati.
Rai
hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi wakati akiongea na viongozi wa
Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) waliofika katika Taasisi hiyo kwa ajili
ya upimaji wa Afya zao.
Prof.
Janabi alisema baadhi ya viongozi hawana mazoea ya kupima afya zao
japo mara moja kwa mwaka na inapotokea wamegundulika kuwa na tatizo la
ugonjwa huwa ni kubwa na limeshaleta madhara mwilini, na wakati
mwingine huwa ni vigumu kutibika lakini tatizo kama hilo likigundulika
mapema katika hatua ya awali huwa ni rahisi kutibika.
Akizungumzia
kuhusu magonjwa ya Moyo Mkurugenzi Mtendaji huyo alisema ni muhimu
mgonjwa afuate maelekezo ya jinsi ya kutumia dawa aliyopewa na daktari
wake kwani kuna baadhi ya wagonjwa wamekuwa na tabia ya kuacha kutumia
dawa pindi wanapojiona wamepata naafuu jambo ambalo siyo sahihi.
Akielezea
jinsi ya kujikinga na magonjwa ya Moyo kwa upande wa chakula Afisa
Lishe kutoka JKCI Louisa Shem alisema ni muhimu kupunguza utumiaji wa
vyakula vya mafuta kupita kiasi hasa mafuta yatokananyo na wanyama,
kutumia vyakula vya nafaka zisizokobolewa.
Kupunguza
unywaji wa pombe na uvutaji wa bidhaa zitokanazo na tumbaku ikiwemo
sigara, kufanya mazoezi ya mwili angalau nusu saa kwa siku na kupunguza
matumizi ya vyakula vyenye chumvi nyingi.
Kwa
upande wake Mkuu wa Idara ya Afya na Usalama Kazini kutoka NHC Dkt.
Yothan Mackenzie alisema hivi karibuni walikuwa na mkutano wa Baraza la
Wafanyakazi katika mkutano huo kulikuwa na mada ya ulaji na afya
wakaona ni vyema mada hiyo iende sambamba na upimaji wa magonjwa
mbalimbali ikiwemo ugonjwa wa Moyo.
Dkt.
Mackenzie alisema wanawapima viongozi hao kwa awamu hadi sasa jumla ya
wakurugenzi na wakuu wa vitengo 14 wamepima na kujuwa afya zao na
viongozi wengine wataendelea kupima kwani Shirika lao linaamini kuwa
mfanyakazi akiwa na afya njema ataweza kufanya kazi zake vizuri.
Baadhi ya magonjwa waliyopima viongozi hao ni pamoja na Moyo, tezi dume, figo na sukari.
COMMENTS