NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR. UMOJA wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi Tanzania (UWT) umewataka wanawake kuchangamkia fursa za ...
NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.
UMOJA
wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi Tanzania (UWT) umewataka wanawake
kuchangamkia fursa za Uongozi wa ngazi mbali mbali kupitia uchaguzi
unaondelea hivi sasa ndani ya Chama na jumuiya zake.
Wito
huo umetolewa Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja huo Zanzibar Bi.Tunu Juma
Kondo katika mwendelezo wa ziara ya UWT ya kuzungumza na Viongozi
wapya wa ngazi za matawi wa umoja huo uko Jimbo la Kijini Wilaya ya
Kaskazini "A" kichama Unguja.
Awambia
Akina Mama hao kuwa Uchaguzi wa ngazi mbali mbali unaoendelea katika
taasisi hiyo ndio fursa moja wapo ya wanawake kupata nafasi za uongozi
ili waweze kufikia malengo ya kupata uwakilishi wa viongozi wenye idadi
sawa na wanaume ndani ya Chama hicho.
Alifafanua
kuwa wanawake wanatakiwa kuondokana na dhana ya kuendelea kuongozwa
kwa kila nafasi za uongozi ndani ya CCM bali wanatakiwa kujiongeza kwa
kuwania wenyewe uongozi ndani ya chama hicho ili kuleta maendeleo
endelevu ndani ya chama na jumuiya zake.
Pia
alisisitiza viongozi hao kuwa pamoja na majukumu ya kiuongozi
waliyonayo ni lazima wawahamasishe kwa wingi wanawake kuwania nafasi
za uongozi ili kupata viongozi makini na wenye uwezo wa kwenda na kasi
za kiutendaji za chama hicho.
"Wanawake
wenzangu tutumieni fursa ya Uchaguzi wa Chama kuwania nafasi mbali
mbali za uongozi , tusisubiri nafasi za uteuzi bali tusimame wenyewe
kupambana kwa kuhakikisha nasi tunakuwa na nyadhifa za uongozi kama
walivyo wanaume kwani tunaweza wenyewe bila ya kuwezeshwa’’,. Alisema
Bi.Tunu.
Akizungumza
katika ziara hiyo Katibu Msaidizi Idara ya Organazesheni UWT Zanzibar,
Bi. Mgeni Ottow Alisema CCM atadumu madarakani endapo viongozi mbali
mbali wanaopatikana kupitia uchaguzi wa chama hicho watakuwa na uzalendo
wa kweli katika kulinda maslahi ya taasisi hiyo kwa vitendo.
Bi.
Mgeni aliwasihi Akina Mama wa Umoja huo kuhakikisha wanachagua
viongozi waadilifu na wenye uwezo wa kubuni fursa mbali mbali za
maendeleo zitakazowanufaisha wanawake wenzao na chama kwa ujumla.
“
Wanawake ndio tegemeo la Chama chetu na jumuiya kwa ujumla hivyo lazima
tuwe wa kwanza kujitokeza kwa kila tukio linalohusu uimarishaji wa
chama chetu hasa michakato ya uchaguzi na tukiwa wengi katika nafasi za
uongozi ndipo tutakapopata nguvu za pamoja kutetea haki zetu na kupinga
kisheria udhalilishaji wa Wanawake”,. Aliseleza Bi. Mgeni.
Kwa
Upande wake Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Kaskazini Unguja, Bi. Miza Ali
Kombo amesema zoezi la Uchaguzi kwa ngazi ya Wadi linaendelea vizuri
kwani wagombea tayari wamejaza fomu na kinachosubiriwa kwa sasa ni
upigaji wa kura ili kupata viongozi watakaoongoza ngazi hiyo kwa miaka
mitano.
Naye
Katibu wa UWT Tawi la Muange, Bi. Waja Mnadhani Ali alieleza maratajio
yake baada ya kupata nafasi hiyo atafanya kazi za jumuiya na chama kwa
umakini na uadilifu ili kuwawakilisha vyema wanawake waliomuamini na
kumpa ridhaa ya uongozi huo.
Kaimu
Naibu Mkuu wa UWT Zanzibar, Bi. Tunu Juma Kondo akizungumza na
viongozi wa Matawi ya Jimbo Kijini Wilaya ya Kaskazini “A” kichama
Unguja.
Katibu Msaidizi wa Idara ya Organazesheni UWT Zanzibar, Bi. Mgeni
Ottow akitoa nasaha kwa viongozi wa Matawi ya Jimbo Kijini Wilaya ya
Kaskazini “A” kichama Unguja.
Baadhi
ya viongozi wa UWT wa Matawi jimbo la kijini Wilaya ya Kaskazini “A”
kichama Unguja wakisikiliza kwa makini nasaha zinazotolewa na viongozi
wa UWT Zanzibar uko Tawi la CCM Muange.
COMMENTS