Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), linatangaza kufungua dirisha la usajili kwa wachezaji wa Ligi Kuu...
Shirikisho la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF), linatangaza kufungua dirisha la usajili kwa wachezaji wa
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja
la Pili ikiwa ni ufunguzi wa msimu mpya wa mashindano wa 2017/2018.
Dirisha hilo linafunguliwa Juni
15, mwaka huu na litafungwa Agosti 6, mwaka huu hivyo kila timu
inayoshiriki michuano tajawa hapo juu, inaarifiwa kufuata kalenda hiyo
ambayo imetangazwa sasa.
Tahadhali, hakutakuwa na muda wa
nyongeza kwa timu ambazo hazitakamilisha usajili kama ilivyotokea msimu
uliopita kwa baadhi ya timu kushindwa kufanya kusajili kwa wakati na
dirisha likafungwa.
COMMENTS