Mkuu wa Itifaki mstaafu Balozi Cisco Mtiro (pichani) ambaye amefariki dunia leo asubuhi katika hospitali ya Aga Khan jijini Dar ...
Mkuu
wa Itifaki mstaafu Balozi Cisco Mtiro (pichani) ambaye amefariki dunia
leo asubuhi katika hospitali ya Aga Khan jijini Dar es salaam alikokuwa
amelazwa kwa matibabu, anatarajiwa kuzikwa siku ya JUMATANO, kwa mujibu wa msemaji wa familia, Bw. Shaaban Kessy Mtambo
Jioni
hii Bw. Mtambo ameiambia Globu ya Jamii kwamba mazishi ya
mwanadiplomasia huyo yamepangwa kufanyika siku ya JUMATANO saa saba
adhuhuri katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam.
Hiyo
ni baada ya kuwasili watoto wake walioko Marekani ambao wanategemewa
kuwasili Jumanne usiku, pamoja na mjane wa marehemu anayetegemewa
kuwasili Jumanne mchana akitokea Bangui, Afrika ya Kati.
Amesema
mwili wa marehemu unatarajiwa kuwasili nyumbani kwa marehemu saa tano
asubuhi siku hiyo ya JUMATANO ambapo utafanyiwa kisomo na kuswaliwa
kabla ya kuelekea makaburini kwa mazishi.
Msiba
upo nyumbani kwa marehemu mikocheni B jijini Dar es salaam ambako
ndugu, jamaa marafiki, majirani na waliofanya kazi na marehemu wamekuwa
wakimiminika kutoa mkono wa pole kutwa nzima ya leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametuma salamu za rambirambi kufuatia msiba huu.
Mola aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi - AMINA
COMMENTS