Spika Mstaafu na Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Anne Makinda akiwahamasisha Madiwani wanawake wa Jiji la D...
Spika
Mstaafu na Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Anne
Makinda akiwahamasisha Madiwani wanawake wa Jiji la Dar es Salaam
walioudhuria mafunzo ya uongozi, jinsia na bajeti yenye mlengo wa
kijinsia pamoja na kutoa uzoefu wake kwenye maswala ya uongozi kwa
wanawake hasa ngazi za juu leo kwenye ukumbi wa TGNP Mtandano jijini Dar
es Salaam.
Mkurugenzi
wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Bi Lilian Liundi akizungumza na
Madiwani Wanawake kuhusu nguvu ya mwanamke kwenye jamii pamoja na
kuwapa miongozo kuhusu nafasi zao kwenye uongozi ili kufikia lengo la
hamsini kwa hamsini.
Mwanachama
wa TGNP Mtandao na mkufunzi wa Mafunzo ya Madiwani wanawake wa Jiji la
Dar Es Salaam Profesa Ruth Meena akiwasilisha mada kuhusu kujitambua
kwa mwanamke kwenye jamii, kujua thamani yake pamoja na mchango wake
kwenye jamii katika mafunzo yaliyofanyika kwenye ukumbiwa TGNP Mtandao
jijini Dar es Salaam.
Mkuu
wa Idara ya Ijenzi wa Nguvu Pamoja wa TGNP Mtandao, Grace Kisetu
akizungumza jambo kwenye mafunzo ya madiwani wanawake wa Jiji la Dar es
Salaam leo
Madiwani
wanawake wa Jiji la Dar es Salaam wakiwa kwenye mafunzo ya uongozi,
jinsia na bajeti yenye mlengo wa kijinsia leo kwenye ukumbi wa TGNP
Mtandano.
Mkutano ukiendelea
Mwenyekiti
wa Muda wa Umoja wa Madiwani Wanawake wa Jiji la Dar es Salaam, Bi.
Saada Mandwanga akitoa shukrani kwa TGNP Mtandao kutoa mafunzo ya
uongozi, jinsia na bajeti yenye mlengo wa kijinsia ambayo kwao yamekuwa
ni chachu kwenye jamii inayowazunguka.
Baadhi ya wafanyakazi wa TGNP Mtandao wakiwa kwenye mafunzo ya Madiwani wanawake yanayofanyika kwa siku tatu
Madiwani
wanawake wa vyama mbalimbali vya siasa katika Mkoa wa Dar es Salaam
wamesema suala la kubadili mtazamo katika ushirikishwaji wa wanawake
kwenye maendeleo ni la msingi na linapaswa kutekelezwa kuanzia ngazi za
chini.
Wakizungumza
katika warsha ya siku tatu ya Uongozi wa Kijinsia iliyoandaliwa na
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP Mtandao), madiwani hao wamesema haki za
wanawake bado zinakandamizwa katika jamii huku vitendo vya unyanyasaji
wa kijinsia vikishika kasi.
Akizungumza katika mafunzo ya siku tatu Spika
Mstaafu na Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Anne
Makinda amesema wanawake wanapaswa kuungana kwa pamoja wanapokuwa
wanapigania haki zao za msingi. Amewasisitiza kuachana na masuala ya
vyama kwenye jambo linalowahusu wanawake wote. Wakifanya hivyo wataweza
kupunguza tabaka kubwa kwenye utawala na hata kwenye uzalishaji mali.
Kwa
upande wa Mkurugenzi wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Bi Lilian
Liundi amesema watoto wa kike wanakosa vipindi vya masomo kutokana na
ukosefu wa elimu ya kujihifadhi hasa wanapokuwa katika hedhi.
“Elimu ya hedhi bado duni sana, hasa vijijini kwa sababu watoto wengi wa
kike wanapokuwa katika hedhi huhisi kwamba ni wagonjwa, hivyo hushindwa
kuhudhuria vipindi ipasavyo lazima elimu hii itolewe kwa jamii ili
kuwawezesha watoto hawa wapate elimu kama ilivyo kwa wale wa kiume,”
alisema Lilian Liundi.
COMMENTS