JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA KURUGENZI YA HABARI NA UHUSIANO Simu ya Upepo : “ N G O M E ” Makao Makuu ya Jesh...
JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA
KURUGENZI YA HABARI NA UHUSIANO
Simu ya Upepo : “N G O M E” Makao Makuu ya Jeshi,
Simu ya Mdomo : DSM 22150463 Sanduku la Posta 9203,
Telex : 41051 DAR ES SALAAM, 02 June 2017
Tele Fax : 2153426
Tovuti : www.tpdf.mil.tz
Wito wa Vyombo vya Habari
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania linapenda kutoa wito kwa vyombo vya Habari ili kufanya coverage ya kufungwaji wa mashindano ya kombe la Mkuu wa Majeshi (CDF CUP) ambayo yanatarajiwa kufungwa rasmi tarehe 04 Juni 2017 katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Venance Mabeyo, kuanzia Saa nne (4:00) kamili asubuhi.
Lengo la mashindano hayo lilikuwa kudumisha mshikamano, kuvumbua na kukuza vipaji na kupata timu itakayo wakilisha Jeshi na Taifa kwa ujumla katika mashindano ya michezo ya Majeshi na Utamaduni kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka huu mashindano yanayotarajiwa kufanyika nchini Burundi mwezi wa nane 2017.Ukiwa mdau wa habari inaombwa chombo chako kufanya ‘coverage’ katika tukio hili muhimu.
Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P 9203, Dar es Salaam, Tanzania.
COMMENTS