Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, akitazama taarifa ya makadirio ya gharama za ujenzi wa sehemu ...
Naibu
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani,
akitazama taarifa ya makadirio ya gharama za ujenzi wa sehemu ya
barabara ya Mboga kuelekea kiwanda cha Matunda cha Sayona, wilayani
Bagamoyo, leo. Kulia ni Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS),
Mkoa wa Pwani Eng. Rehana Yahya.
Naibu
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani,
akielekeza jambo kwa Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Bw. Magid Mwanga
kuhusu makadirio ya gharama za ujenzi wa sehemu ya barabara ya Mboga
kuelekea kiwanda cha Matunda cha Sayona, wilayani Bagamoyo, leo.
Mkandarasi
wa kampuni ya Motsum Builders, Bw. Kante Bay akitoa maelezo kwa Naibu
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, kuhusu
sehemu ya barabara ya Mboga inayoelekea katika kiwanda cha Matunda cha
Sayona, wilayani Bagamoyo, leo.
Naibu
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani
(katikati), akitazama ramani ya mji inayoonesha maingilio ya barabara
katika kiwanda cha Matunda cha Sayona, wilayani Bagamoyo, mkoani Pwani
leo.
Naibu
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani
(katikati), akifafanua jambo kwa Meneja Mradi wa Kiwanda cha Marumaru na
Masinki cha Twyford Ceramics Bw. Howard Li, kilichopo Chalinze mara
baada ya kukagua kiwanda hicho, mkoani Pwani leo.
……………………………………………………………………………………….
Serikali
imesema kuwa itashirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo katika
kutoa wataalam, kuandaa michoro na kusimamia ujenzi wa barabara zote
zinazoingia katika viwanda vinavyojengwa mkoani Pwani.
Akizungumza
leo mkoani humo, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng.
Edwin Ngonyani, amesema kuwa hatua hiyo imefikiwa mara baada ya uongozi
wa Halmashauri ya wilaya hiyo kuandika barua kwa Wizara hiyo kuomba
msaada wa kujengewa barabara ya Km 1 inayoingia kwenye kiwanda kipya cha
Matunda cha Sayona kutoka kwenye barabara kuu ya Chalinze – Arusha na
ile iliyopo katika kiwanda cha kutengeneza marumaru na masinki cha
Twyford.
“Barabara
hii ni ya kwenu Halmashauri, angalieni namna ya kukaa na mwenye kiwanda
kuona namna ya kusaidia miundombinu yake, Wizara yangu kupitia Wakala
wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Pwani, itasaidia huduma za kitaalamu na
usimamizi”, amesema Naibu Waziri.
Aidha,
Naibu Waziri huyo ameutaka uongozi wa Halmashauri hiyo kutumia fedha za
Bodi ya Mfuko wa Barabara (RFB), kuona namna ya kujenga barabara hizo
na kuhakikisha ubora wa barabara hizo unaendana na thamani ya fedha
zinazotolewa.
Kuhusu
ujenzi wa barabara inayoingia kwenye kiwanda cha kutengeneza marumaru
na masinki kilichopo wilayani hapo, Naibu Waziri Ngonyani, ameuagiza
uongozi wa TANROADS mkoani humo kupima na kufanya tathmini ya gharama za
ujenzi wa barabara hiyo ili kupata taarifa sahihi.
Kwa
upande wake Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Bw. Magid Mwanga, ameipongeza
Serikali ya Awamu ya Tano kwa kufanya kazi kwa vitendo kwa kuchukua
hatua za haraka za kutembelea maeneo hayo na kuboresha miundombinu ya
barabara katika viwanda ili kuhamasisha na kuchochea wawekezaji wa
viwanda nchini.
Dhamira
ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kujenga miundombinu bora kwa wananchi
wake na Taifa kwa ujumla ili kuhamasisha uwekezaji wa viwanda na huduma
za usafirishaji ili kufikia uchumi wa kati ifikapo 2025.
COMMENTS