Meneja Miradi kutoka Social Action Trust Fund (SATF) Rogasian Massue akimkabidhi leo mfano wa hundi ya shilingi milioni 10 Mkurug...
Meneja
Miradi kutoka Social Action Trust Fund (SATF) Rogasian Massue
akimkabidhi leo mfano wa hundi ya shilingi milioni 10 Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi
fedha ambazo zitatumika kwa ajili ya kulipia gharama za upasuaji wa moyo
kwa watoto watano.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi
akimshukuru Meneja Miradi kutoka Social Action Trust Fund (SATF)
Rogasian Massue mara baada ya kumkabidhi leo mfano wa hundi ya shilingi
milioni 10 fedha ambazo zitatumika kwa ajili ya kulipia gharama za
upasuaji wa moyo kwa watoto watano.
Meneja
Miradi kutoka Social Action Trust Fund (SATF) Rogasian Massue
akimsalimia mtoto Goodluck Msele ambaye amefanyiwa upasuaji wa moyo hivi
karibuni katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na hali yake
inaendelea vizuri. SATF imechangia shilingi milioni 10 fedha ambazo
zitatumika kwa ajili ya kulipia gharama za upasuaji wa moyo kwa watoto
watano.
Daktari
Bingwa wa upasuaji wa Moyo kwa Watoto na Mkuu wa Idara ya Upasuaji wa
Moyo kwa Watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Godwin Sharau
(katikati) akimwelezea Meneja Miradi kutoka Social Action Trust Fund
(SATF) Rogasian Massue (kushoto) kuhusu aina mbalimbali za magonjwa ya
moyo yanayowasumbua watoto wanaotibiwa katika Taasisi hiyo. Kulia ni
Msimamizi wa Wodi ya watoto Afisa Muuguzi Rogers Kibula.
Meneja
Miradi kutoka Social Action Trust Fund (SATF) Rogasian Massue
akimsikiliza Daktari Bingwa wa upasuaji wa Moyo kwa Watoto na Mkuu wa
Idara ya Upasuaji wa Moyo kwa Watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
(JKCI) Godwin Sharau wakati akimuelezea jinsi upasuaji wa moyo
unavyofanyika katika Taasisi hiyo. (Picha na JKCI)
COMMENTS