MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda akizingumza na Wakurugenzi wa Manispaa za Jiji la Dar es Salaam alipotembelea Kitu...
MKUU
wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda akizingumza na Wakurugenzi
wa Manispaa za Jiji la Dar es Salaam alipotembelea Kituo cha Taifa cha
Kuhifadhi Kumbukumbu (National Internet Data Center) kilichopo
Kijitonyama. (Picha Zote na Mathias Canal)
Mkurugenzi
wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo (kushoto) akimsikiliza
kwa makini Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul Makonda
alipotembelea Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi Kumbukumbu (National
Internet Data Center) kilichopo Kijitonyama. Mwingine ni Katibu Tawala
wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando.
Wakurugenzi,
Na Maofisa Biashara wa Manispaa za Jiji la Dar es Salaam wakimsikiliza
kwa makini Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda wakati wa
kikao cha pamoja katika Ukumbi wa Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi
Kumbukumbu (National Internet Data Center) kilichopo Kijitonyama.
Mkuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe Paul Makonda akizingumza na Wakurugenzi
wa Manispaa za Jiji la Dar es Salaam alipotembelea Kituo cha Taifa cha
Kuhifadhi Kumbukumbu (National Internet Data Center) kilichopo
Kijitonyama.
Mkurugenzi
wa Manispaa ya Ubungo, John Kayombo (Kulia) akimsikiliza kwa
makini Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda alipotembelea
Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi Kumbukumbu (National Internet Data Center)
kilichopo Kijitonyama. Mwingine ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni,Aron Kagoromjuli
Na Mathias Canal, Dar es Salaam
MKUU
wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda amewaagiza Wakurugenzi wa
Manispaa Jijini Dar es Salaam kujiunga katika mfumo mpya wa Mamlaka ya
Mapato Tanzania (TRA) wa ukusanyaji mapato kwa njia ya kielektroniki
(e-RCS) ili serikali iweze kupata kodi stahiki kwa mujibu wa sheria.
RC
Makonda ametoa agizo hilo leo June 20, 2017 Jijini Dar es Salaam
alipotembelea Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi Kumbukumbu (National
Internet Data Center) kilichopo Kijitonyama, dhifa iliyohudhuriwa pia
na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Wakurugenzi wa Manispaa
sambamba na Maofisa Biashara wa Manispaa zote za Jiji.
Mhe
Makonda alisema kuwa kujiunga katika mfumo huo Manispaa zote zitapata
urahisi katika kuwahudumia wananchi sawia na kurahisisha kuboresha
vyanzo vya mapato.
Alisema
kuwa mfumo huo utaongeza Mapato katika Manispaa, Kuondoa usumbufu kwa
wananchi ikiwemo kuepuka Rushwa, sambamba na Kuimarisha huduma kwa
wananchi.
"Najua
Kuna watu Jambo hili litawakwaza Sana hususani wale wapiga dili lakini
niwahakikishie kuwa kuna umuhimu mkubwa Sana kujiunga na Mfumo huu wa
kisasa wa kuhifadhi kumbukumbu kwani ni njia rahisi ya kutoa taarifa pia
ni Mfumo mzuri kwa usalama wa Taifa" Alisisitiza Mhe Makonda
Wakurugenzi
hao wameagizwa kutumia wiki moja kujadili namna gani ya kujiunga na
Mfumo huo huku akielekeza Hadi kufikia Agosti Mosi mwaka huu Manispaa
zote ziwe zimejiunga na Mfumo huo.
Aidha,
Alisema kuwa Kujiunga na Mfumo huo wa serikali wa ukusanyaji Mapato kwa
njia ya Kielektroniki itarahisisha umakini wa huduma hivyo kuachana na
Mfumo wa zamani wa kutuma watu kutambua watu ambao leseni zao zimemaliza
muda wa matumizi.
Alisema
kuwa Jiji la Dar es Salaam Lina vituo vya Daladala zaidi ya 800 hivyo
endapo kama ukiwekwa mfumo mzuri wa ukusanyaji wa Mapato katika vituo
hivyo itakuwa ni chanzo Cha upatikanaji wa mapato ya serikali.
Mfumo
wa Serikali wa Ukusanyaji Mapato kwa Njia ya kielektroniki ulizinduliwa
June Mosi Mwaka huu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt
John pombe Magufuli ambaye aliambatana na Rais wa serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein
na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu
Hassan na viongozi wengine.
COMMENTS