Wanamichezo Watakiwa Kuzingatia Nidhamu Na Lorietha Laurence Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyem...
Wanamichezo Watakiwa Kuzingatia Nidhamu
Na Lorietha Laurence
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe amewataka wadau wa michezo nchini kuzingatia nidhamu na uvumilivu ili kufikia malengo ya klabu zao.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt. Harisson Mwakyembe leo Jijini Dar es Salaam alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kufuatia ujio wa klabu ya Everton nchini chini ya uratibu wa Kampuni ya SportPesa.
Katika mkutano huo, Waziri Mwakyembe ameeleza kuwa ujio wa uongozi wa timu ya Everton ni fursa kubwa kwa vilabu vya mpira wa miguu nchini katika kujifunza mbinu mbalimbali za kuendeleza na kukuza vipaji vya wachezaji wake.
“Ujio huu ni muhimu na elimu tosha kwa vilabu vyetu nchini katika kuhakikisha vipaji vya wanamichezo vinakuzwa na kuendelezwa ili kufanikisha maendeleo ya sekta ya michezo “alisema Dkt.Mwakyembe.
Alisema mbali na elimu itakayopatikana kutoka kwa timu na uongozi wa Everton, ni fursa nzuri katika sekta ya Utalii kwa kuwa wageni hao wataweza kutembelea Mbuga za Wanyama,Mlima Kilimanjaro na vivutio vingine mbalimbali vya kimichezo.
Naye Mtendaji Mkuu wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Everton, Robert Elstone amesema kuwa lengo kuu la kuwepo Tanzania ni kujenga uhusiano mzuri katika michezo husani mpira wa miguu kwa kuweka msingi mzuri wa kusaidia klabu za michezo na kukuza vipaji kwa vijana.
Kwa upande wake mchezaji wa zamani wa Everton, Leon Osman amesema kuwa ni muhimu kuendeleza vipaji vya vijana ili kuweza kupata wachezaji mahiri.
Mchezaji wa Zamani wa timu ya Everton ya Nchini Uingereza Leon
Osman azindua programu ya timu za vijana nchini itakayosimamiwa na timu
hiyo uzinduzi uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.
Osman aliyekuwa ameambatana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa
na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe walizindua programu hiyo kwa vijana
wadogo ambapo itakuwa endelevu hapa nchini.
Akizungumza na watoto kutoka katika vituo mbalimbali vya kukuzia
vipaji vya soka Osman amewataka kujituma zaidi ili waweze kufikia
malengo yao.
Osman amewapatia zawadi ya mipira vijana hao waliokuja na kuonyeshwa kufurahia namna wanavyojituma na kuonyesha vipaji vyao.
Waziri
wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo Harrison Mwakyembe akiwa
ameongozana na mchezaji wa zaman wa Everton Leon Osman (wa pili kulia)
sambamba na Mkurugenzi wa Michezo wa Wizara Yusuph Singo (kulia) na
Mkurugenzi wa Timu ya Everton Robert Elstone leo Jijini Dar es salaam.
Waziri
wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo Harrison Mwakyembe akiwa
ameongozana na mchezaji wa zamani wa Everton Leon Osman (anayewasalimia
vijana ) sambamba na Mkurugenzi wa Timu ya Everton Robert Elstone leo
Jijini Dar es salaam.
Mchezaji wa zamani wa Everton Leon Osman akiwa uwanjani na baadhi ya vijana akiwapa maelekezo mbalimbali.
Mchezaji
wa zamani wa Everton Leon Osman akitoa zawadi ya mipira kwa vijana
waliojitokeza katika uzinduzi wa programu hiyo itakayokuw aendelelevu
chini ya Timu ya Everton.
Mchezaji
wa zamani wa Everton Leon Osman akiwa katika picha ya pamoja na vijana
kutoka vituo mbalimbali pamoja na Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na
Michezo Harrison Mwakyembe na Mkurugenzi wa Timu ya Everton Robert
Elstone.
Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo Harrison Mwakyembe
akiwa na mchezaji wa zaman wa Everton leon Osman (wa kwanza kushoto)
sambamba na Mkurugenzi wa Michezo wa Wizara Yusuph Singo (kulia) na
Mkurugenzi wa Timu ya Everton Robert Elstone (wa nne kulia) na Mkurugenzi
wa SportPesa Pavel Slavkov na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Sportpesa
Tanzani Abbas Tarimba.
COMMENTS