Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia) akisalimiana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya kikristo Tanzania, Askofu Dkt. Alex Mala...
Spika
wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia) akisalimiana na Mwenyekiti wa
Jumuiya ya kikristo Tanzania, Askofu Dkt. Alex Malasusa kabla ya kuanza
harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania,
katika tukio lililofanyika Mjini Dodoma Juni 18 2017, Spika Ndugai pia alikuwa mgeni
rasmi ambapo aliongoza Wabunge katika harambee hiyo.
Spika
wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kulia) akisalimiana na Waziri Mkuu
Mstaafu, Mheshimiwa Mizengo Pinda kabla ya kuanza harambee kwa
ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya Kikristo Tanzania, katika tukio
lililofanyika Mjini Dodoma June 18 2017. Katikati ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania, Askofu Dkt. Alex Malasusa.
Spika
wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kulia) akiongoza Wabunge Mbalimbali kucheza nyimbo ya injili kama njia moja wapo ya kuhamasisha
uchangiaji kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya Kikristo Tanzania,
tukio lililofanyika Mjini Dodoma.
Spika
wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza jambo kabla ya kuanza
harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania,
tukio lililofanyika Mjini Dodoma. Kushoto ni Waziri Mkuu Mstaafu,
Mhe. Mizengo Pinda na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania, Askofu Dkt. Alex Malasusa.
Spika
wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akiteta jambo na Katibu wa
Bunge, Dkt. Thomas Kashililah (kulia) baada ya kumalizika kwa harambee
kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania, tukio
lililofanyika Mjini Dodoma.
Waziri
Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda (kushoto) akisalimiana na Katibu
wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah baada ya kumalizika kwa
harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania,
katikati ni Ndg. Elton Mapesa Mwakilishi wa Harambee kutoka External,
Ubungo Jijini Dar es Salaam. Katika harambee hiyo, Spika wa Bunge,
Mhe. Ndugai aliwaongoza wa Bunge katika uchangiaji wa ujenzi
wa jengo hilo.
Waziri
Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda (wa pili kushoto) akizungumza
jambo baada ya kumalizika kwa harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la
Jumuiya ya kikristo Tanzania. Kulia ni Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas
Kashililah, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo,
Askofu Dkt. Alex Malasusa (kushoto) na Elton Mapesa
Mwakilishi wa Harambee kutoka External Ubungo Jijini Dar es Salaam.
COMMENTS