DROO ya kwanza ya Sh Milioni 20 na ya kumi kufanywa na waendeshaji wa bahati Nasibu ya Biko hatimae imepata mwenyewe baada ya kutan...
DROO
ya kwanza ya Sh Milioni 20 na ya kumi kufanywa na waendeshaji wa bahati
Nasibu ya Biko hatimae imepata mwenyewe baada ya kutangazwa mshindi
wake ambaye ni Huruma Mkongwa wa jijini Arusha, akiibuka kidedea katika
droo iliyochezeshwa jana, jijini Dar es Salaam.
Droo
hiyo ni ongezeko la Sh Milioni 10 ambapo hapo awali droo zote zilikuwa
zikihusisha kiasi hicho cha pesa kabla ya kuongezwa katika droo ya
Jumatano ambapo waliongeza Milioni 10 nyingine hivyo kufikia Sh Milioni
20 na hivyo kutua kwa Mkongwa.
Akizungumza
jana jijini Dar es Salaam wakati wa kuchezesha droo hiyo, Meneja Masoko
wa Biko, Goodhope Heaven, alisema Jumatano ya Sh Milioni 20 imekuwa
tamu baada ya fedha hizo za zawadi ya juu kabisa kutoka kwenda kwa
Mkongwa ambapo anakuwa mshindi wa kwanza kuzoa kiasi hicho cha pesa
kutoka kwenye bahati nasibu yao inayotikisa nchini.
Balozi
wa Biko Kajala Masanja kulia akisalimiana na Mkaguzi kutoka Bodi ya
Michezo ya Kubahatisha Tanzania Bakari Maggid kabla ya kuanza kuchezesha
droo ya 10 ya Jumatano ya Sh Milioni 20 ambapo mkazi mwingine wa
Arusha, Huruma Mkongwa aliibuka kidedea.
Balozi
wa Biko Kajala Masanja akimtangaza mshindi wa Sh Milioni 20 Huruma
Mkongwa kutoka mkoani Arusha baada ya kumaliza kuchezeshwa droo hiyo ya
10 ya Biko. Kushoto ni Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha
Tanzania Bakari Maggid.
Balozi
wa Biko Tanzania Kajala Masanja akifurahia jambo baada ya kupatikana
mshindi wa Sh Milioni 20 katika droo iliyochezeshwa jana jijini Dar es
Salaam.
Alisema
ni imani yao ni kwamba kutoka kwa fedha hizo kutazidi kuibua fursa
sahihi kwa washindi wao katika kuhakikisha wanatumia vema fedha hizo ili
wanufaike kiuchumi kwa kutumia rasilimali fedha wanazopata kutoka Biko.
“Jumatano
ya leo imekuwa Jumatamu kwa mshindi wetu Huruma Mkongwa wa Arusha
kupata mkwanja kutoka kwetu, huku Biko tukiwa na lengo kubwa la kukuza
uchumi wa wananchi wote hususan wale wanaoamua kutuunga mkono kwa
kucheza Biko mara nyingi zaidi kwa kufanya miamala kwenye simu zao za
Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel Money ambapo watakapoingia kwenye lipa bili
au lipa kwa Mpesa wataweka namba ya kampuni ambayo ni 505050 na ile ya
kumbukumbu 2456.
“Huu
ni wakati wa kupata zawadi mbalimbali kutoka Biko kuanzia Sh 5,000,
10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni moja ambapo
hulipwa papo hapo kwa kupitia simu zao walizocheza muda mchache baada ya
kushinda, hivyo ili washinde lazima wacheze mara nyingi zaidi ili
wajiwekee mazingira mazuri ya ushindi,” Alisema Heaven.
Akizungumza
kwa simu wakati anafanya mahojiano na Balozi wa Biko Kajala Masanja,
Mkongwa alisema haamini kama ameshinda donge nono hilo kutoka Biko
ingawa alikiri kucheza Biko akiomba Mungu ashinde ili atimize malengo
yake,
“Nashukuru
dada Kajala kama mimi ndio mshindi hakika nimefurahi kwa kunitangaza
mimi, maana nina uhitaji wa fedha ukizingatia kwamba shughuli zangu kwa
sasa nashughulika na mambo ya magari yanayokwenda Namanga,” Alisema
Mkongwa.
Naye
Mkaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Bakari Maggid,
alisema wanafurahishwa na utaratibu mzima unaofanywa na Biko katika
kuwapata washindi wa papo kwa hapo na wale wa droo kubwa ya Sh Milioni
10 na hii ya Milioni 20 iliyofanyika Jumatano na kupatikana Mkongwa
kutoka mkoani Arusha.
“Ni
wakati wa Watanzania kujitokeza kwa wingi kucheza Biko kwasababu fedha
zipo nje nje na kila mtu anaweza kushinda, ukizingatia kuwa Biko
wanakidhi vigezo vyote na mchezo wao ni mzuri unaoweza kutoa fedha kwa
kila Mtanzania,” Alisema.
Mkongwa
anakuwa mtu wa kwanza kushinda donge nono la Sh Milioni 20 lililowekwa
katika droo ya Jumatano, huku akiwa mtu wa pili kushinda dau kubwa
likiwapo la Sh Milioni 10 ambapo zimetolewa kwa washindi tisa, huku yeye
pekee akitarajiwa kukabidhiwa fedha zake Sh Milioni 20 mapema
iwezekanavyo kama atakavyopewa utaratibu na Biko.
COMMENTS