MARUFUKU KUFANYA SHUGHULI ZA KIBINADAMU NDANI YA MITA 60 YA VYANZO VYA MAJI-DC HANDENI

Wananchi wilayani Handeni wapigwa marufuku kufanya shughuli za kibinadamu ndani ya mita 60 kutoka katika vyanzo vya maji na kutakiwa...


Wananchi wilayani Handeni wapigwa marufuku kufanya shughuli za kibinadamu ndani ya mita 60 kutoka katika vyanzo vya maji na kutakiwa kutunza mazingira ili kuwezesha uendelevu wa maisha.

Marufuku hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Godwin Gondwe aliyekuwa mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya siku ya mazingira duniani yaliyofanyika ngazi ya wilaya katika Kata ya Mkata katika bwawa la Tulafimbo. 

Gondwe alisema kuwa wananchi lazima wazingatie sheria ya Mazingira inayozuia kufanya shughuli za kibinadamu pamoja na kujenga kwenye maeneo yote ya vyanzo vya maji ndani ya mita 60. “Kwa kuzingatia sheria hiyo, kupiga marufuku kwa wananchi kufanya shughuli zozote za kibinadamu zenye kuhatarisha usalama wa maji na uchafuzi wa mazingira kwenye maeneo yanayozunguka vyanzo vya maji wilayani Handeni” alisema Gondwe. 

Aidha, aliwataka maafisa Tarafa, maafisa watendaji wa Kata na wenyeviti wa Vijiji kuhakikisha wanatengeneza mipaka kwenye maeneo ya vyanzo vya maji vyote vilivyopo Wilayani Handeni msimu huu ambao mvua imenyesha ya kutosha na vyanzo vingi vimejaa maji. “Hii itasaidia kuzuia uvamizi wa maeneo hayo na kurahisisha kuchukua hatua kwa watu watakaokwenda kinyume na amri hiyo” alisema Gondwe.

Gondwe, aliwataka wananchi wote walionunua mashamba kwa lengo la kilimo kusafisha mashamba yao kwa kuacha asilimia 30 ya uoto wa asili badala ya kusafisha maeneo yote ambayo wamenunua. “Tusipotunza mazingira, itakuwa ni ubinafsi kwa kizazi chetu na kizazi kijacho. Tukitendee haki kizazi hiki na kijacho kwa kuondoa ubinafsi wa kuharibu mazingira” alisema Gondwe.

Wakati huohuo, aliwataka viongozi ngazi ya Wilaya, Tarafa, Kata na Vijiji kutunza kutunza mazingira kwa kusimamia uwiano wa ardhi uliyopo na idadi ya mifugo ili kutunza mazingira kwa kuwa na mifugo inayoendana na rasilimali ardhi iliyopo. Aliwataka kuweka mikakati ya kupiga chapa mifugo ili kurahisisha utambuzi wa mifugo hiyo wilayani Handeni.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni, William Makufwe aliwataka wananchi kutunza rasilimali maji kidogo inayopatikana kwa kipindi cha mvua kwa kupanda miti kwenye maeneo yanayozunguka vyanzo vya maji. Alisema kuwa Serikali inaendelea kushughulikia changamoto ya upatikanaji maji ya kudumu Wilayani Handeni. 

Aliwataka wakuu wa shule za msingi na sekondari kuhakikisha kila mwanafunzi anayeanza darasa la kwanza hadi la saba na kidato cha kwanza hadi cha nne anakuwa na mti wake anaoutunza ili anapomaliza shule akikabidhiwa cheti na yeye akabidhi mti alioutunza kwa kipindi chote alichokuwa shuleni. 

Maadhimisho ya wiki ya mazingira kiwilaya yalitanguliwa na upandaji miti 28,954 yakiongozwa na kaulimbiu isemayo “hifadhi ya mazingira muhimili kwa Tanzania ya viwanda”.
 Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh Godwin Gondwe akipanda mti kwenye maadhimisho.
 Mkurugenzi Mtendaji Bw William Makufwe iyeshika chepeo na mwenyekiti wa Halmashauri ya Handeni Mh Ramadhani Diliwa wakipanda mti.
 Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh Godwin Gondwe akizungumza na wananchi.
 Mkurugenzi Mtendaji Bw William Makufwe akizungumza na wananchi wakati wa maadhimisho.
 Mwenyekiti wa Halmashauri Mh Ramadhani Diliwa akizungumza na wananchi.
Wanafunzi wa shule ya sekondari Mkata  wkisherehesha kwa Ujumbe wa utunzaji mazingira.















Halila

Tongolanga amefariki jana usiku katika hospitali ya Muhimbili. Alikuwa

mwanamuziki wa siku nyingi na alifahamika kwanza  kwa wengi baada ya kuanza kusikika kibao chake cha lugha ya Kimakonde cha Kila munu ave na kwao, chenye

tafsiri ya ‘Kila mtu ana kwao’ ambacho alikirekodi akiwa bendi ya jeshi ya CTU

Monduli, iliyojulikana kama  Les

Mwenge. Kwa kifupi ni kuwa baada ya hapo aliitwa kujiunga na bendi iliyokuwa

mali ya Dr Alex Khalid, iliyokuwa ikiitwa Makondeko Six. Wakati huo Dr Khalid

alikuwa na sehemu kubwa ya burudani iliyokuwa pia na ukumbi na ilikuwa inaitwa

Makondeko ikawa na bendi ya watu sita hivyo bendi hiyo ikaitwa Makondeko Six.

Bendi hii awali ilikuwa ikipiga muziki kwa kufuata nyayo za bendi ya Tatu Nane,

lakini Dr Khalid baada ya kuona bendi haina umaarufu kutokana na aina ya muziki iliyokuwa ikipiga, ndipo alipomuita

Halila Tongolanga nae akaja na baadhi ya wanamuziki wakajiunga na kuanzisha kundi

lililoendelea kutumia jina la Makondeko Six japo wanamuziki walikuwa wengi zaidi

ya sita. Na ndipo katika kundi hili lilikuwa na wanamuziki wengine kama

Innocent Nganyagwa, Anna mwaole wakaweza kurekodi tena wimbo wa Kila Munu Ave

na kwao na kundi kupata umaarufu mkubwa mpaka baada ya kusambaratika kwa Makondeko baada ya kifo cha Dkt. Alex Khalid lakini Tongolanga aliendelea
kutumia jina la Makondeko. 

Baadhi ya wanamuziki waliowahi kufanya kazi na Tongolanga katika kundi la makondeko Six, wakiwa wanasubiri kusafirisha mwili wa mpendwa wao.Toka kushoto, Innocent Nganyagwa, Meneja wa bendi, mpiga solo, Waninga

                       Tongolanga amefanya kazi nyingi za muziki ikiwemo

kuwa mmoja wa kundi lililoundwa na wanamuziki wengine mahiri kama Moshi William, Muhidin Mwalim, Huluka Uvuruge, Kandaya na wengine lililojulikana

kama Bana mwambe, ambapo waliweza kutoka nyimbo nyingi nzuri sana wakati

biashara ya kuuza album ilipokuwa ina faida. Tongolanga ameagwa na wapenzi wa

muziki ndugu na marafiki, lakini kulikuwa na uhaba mkubwa wa wanamuziki wenzie katika

kundi lililokuja kumuaga mwanamuziki huyu. Waliojitokeza hasa ni wanamuziki wale tu

ambao waliwahi kupiga nae katika kundi la Makondeko na Bana Mwambe na wanamuziki wengine wachache wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Shirikisho la Muziki John Kitime, Katibu Mkuu wa Chamudara Hassan Msumari. Serikali iliwakilishwa na Katibu Mtendaji wa BASATA.  Katika jambo moja kubwa lililotokea

wakati wa kuaga mwili ni kujitokeza kwa balozi wa Msumbiiji Bi Monica Patricio

Clemente aliyefika Muhimbili kuaga mwili wa Tongolanga akiwa amesindikizwa na maafisa wengine, na pia Balozi huo alitoa

rambirambi zake kama Balozi na alitoa rambirambi kutoka kwa Waziri wa Ulinzi wa

Msumbiji. Hili lilikumbusha usemi wa wahenga ‘Nabii hathaminiwi kwao.’ Taarifa

zilizopatikana pale ni kuwa Tongolanga alikuwa mtu maarufu sana nchini

Msumbiji, na aliyekuwa ni msanii muhimu wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu nchini

humo.
Balozi wa Msumbiji Bi Monica Patricio Clemente akiaga sanduku lililokuwa na mwili wa Halila Tongolanga










Nilipokutana

nae kwa mara ya mwisho akiwa kitandani Tongolanda kwa sauti ya uchovu alinambia

alikuwa na mengi ya kunambia, wakati tunasubiri taratib kukamilika za kuanza

kusafirisha mwili, Innocent Nganyagwa ambaye alikuwa mmoja ya wanamuziki

waliotengeneza kundi la Makondeko Six alinambia Tongolanga alikuwa amepanga

kufanya onyesho la ‘Usiku wa Makondeko’ na alikuwa na mipango mingine mikubwa

ya kufanya kupitia kipaji chake. Pengine ndiyo hayo aliyotaka kunambia Mungu

pekee anajua. 



Shukrani za pekee zimfikie Mbunge wa Tandahimba Mheshimiwa Katani Ahmed Katani, kwani kwa juhudi zake Tongolanga alisafirishwa akiwa hai kutoka Ndanda hadi Dar es Salaam kwa matibabu, na pia ndie aliyeusafirisha mwili wa mwanamuziki huyu kwenda Mchichila kwa ajili ya mazishi.
Toka kushoto Rais wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi Nyangamale, Balozi wa Msumbiji nchini, Katibu Mtendaji wa BASATA, Mbunge wa Tandahimba Mhe Katani Katani, afisa wa Ubalozi wa Msumbiji










Tongolanga

anategemewa kuzikwa kijijini kwao Mchichila kesho Junanne 6 Juni 2017.









Mungu

Amlaze Pema Halila Tongolanga 

Mpiga Kinanda Geophrey Kumburu, Katibu Mtendaji wa BASATA Godfrey Mngereza, Katibu Mkuu wa CHAMUDATA Hassan Msumari

John Kitime, wanamuziki wa Makondeko Six, Mngereza, KumburuAdd caption




Sanduku alilolazwa Halila Tongolanga likitayarishwa kuingizwa kwenye gari la kusafirisha kuelekea Mcjichila





















Sanduku likiingizwa kwenye gari










Imetayarishwa na John Kitime wa www.tanzaniarhumba.blogspot.com

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MARUFUKU KUFANYA SHUGHULI ZA KIBINADAMU NDANI YA MITA 60 YA VYANZO VYA MAJI-DC HANDENI
MARUFUKU KUFANYA SHUGHULI ZA KIBINADAMU NDANI YA MITA 60 YA VYANZO VYA MAJI-DC HANDENI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg9Pd0yYyYKcVwTWwVrm4jBwAcgyxKsvLTUjaSw3je-ndP1RPJFFYgzASrc5CLp4iHpiG1Jcu5K1tHFDXiiNR5A4OVhx_xFP90YkFbu29RqMsEjUkDbxOzun_gxfvzOOLs4Kcarq1sbTBk/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg9Pd0yYyYKcVwTWwVrm4jBwAcgyxKsvLTUjaSw3je-ndP1RPJFFYgzASrc5CLp4iHpiG1Jcu5K1tHFDXiiNR5A4OVhx_xFP90YkFbu29RqMsEjUkDbxOzun_gxfvzOOLs4Kcarq1sbTBk/s72-c/1.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/marufuku-kufanya-shughuli-za-kibinadamu.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/marufuku-kufanya-shughuli-za-kibinadamu.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy