MAJARIBIO YA UTAFITI WA HALI YA UMASIKINI UNAENDELEA KUFANYIKA MKOANI DODOMA NA KILIMANJARO

Benny Mwaipaja, WFM - Dodoma 29 Juni, 2017. Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo y...


Benny Mwaipaja, WFM - Dodoma

29 Juni, 2017.

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee, na Watoto pamoja na Shirika la Afya Duniani (WHO), inakamilisha majaribio ya utafiti wa hali ya umasikini katika mikoa ya Dodoma na Kilimanjaro kabla ya kuanza utafiti huo nchi nzima mwezi Agosti, mwaka huu.

Hayo yamesemwa mjini Dodoma na Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa wakati Ujumbe kutoka Benki ya Dunia ulipotembelea na kukagua ujenzi wa Jengo Jipya la Makao Makuu ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu mjini humo.

Amesema kuwa ana matarajio kwamba mchakato wa taarifa za utafiti huo zitafanywa mjini Dodoma baada ya kukamilika kwa ujenzi wa Ofisi hiyo inayojengwa kwa gharama ya shilingi 11.6 bilioni, zikiwa ni fedha za mkopo wenye masharti nafuu kutoka Benki ya Dunia.

Dkt. Chuwa ametoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa wakusanya taarifa za utafiti huo ili Serikali iweze kupata takwimu sahihi za hali ya umasikini nchini kwa ajili ya kutathmini programu mbalimbali na kupanga mipango ya maendeleo ya wananchi wake.

Nae Mshauri wa Masuala ya Kitakwimu kutoka Benki ya Dunia nchini Tanzania, Elizabeth Talbert amesema kuwa Benki yake imetoa mkopo huo kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania Bara na Zanzibar kutokana na Benki hiyo kuona mchango mkubwa wa takwimu katika maendeleo ya nchi yoyote ile duniani.

“Tumefurahishwa na kasi ya ujenzi wa Ofisi hii hapa mjini Dodoma na tunaamini ujenzi wake utakamilika kwa wakati ili kazi za kitakwimu ziweze kufanyika katika mazingira mazuri na tunaamini hatua hii italeta mchango mkubwa katika masuala ya kitakwimu hapa nchini” alisema Bibi Talbert.

Amesema kuwa Jengo la Ofisi ya Takwimu kwa upande wa Zanzibar limekamilika na huenda likaanza kutumika mapema Julai mwaka huu hatua ambayo inaleta mageuzi makubwa katika tasnia hiyo ya ukusanyaji wa takwimu mbalimbali zinazoisaidia nchi kupanga mipango ya maendeleo ya watu wake.
Kwa upande wake Mkandarasi Msanifu Majengo Mhandisi Ramadhani Shomvi anayesimamia ujenzi wa jengo hilo litakalo kuwa na ghorofa 6, amesema kuwa kampuni yake itakamilisha ujenzi huo mwezi Februari, 2018.

Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina chuwa (wa pili kushoto) akingalia kitofali kinachotengezwa na mkandarasi anayejenga jengo la Taasisi hiyo wakati Ujumbe kutoka Benki ya Dunia ulipotembelea na kukagua ujenzi wa Jengo Jipya la Makao Makuu ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu linalojengwa mkoani Dodoma.
Mshauri wa Masuala ya Kitakwimu kutoka Benki ya Dunia nchini Tanzania, Elizabeth Talbert (kushoto) akisisitiza jambo wakati Ujumbe kutoka Benki hiyo ulipotembelea na kukagua ujenzi wa Jengo Jipya la Makao Makuu ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu linalojengwa mkoani Dodoma.
Mkandarasi Msanifu Majengo, Mhandisi Shomvi (aliyevaa sweta kulia) anayesimamia ujenzi wa jengo la ofisi ya Taifa ya Takwimu linalojengwa Mkoani Dodoma akitoa maelezo kuhusu maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo wakati Ujumbe kutoka Benki ya Dunia ulipotembelea na kukagua ujenzi wa Jengo hilo mjini Dodoma.
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina chuwa (wa pili kushoto) akifurahia jambo na timu ya wataalamu wa ujenzi na ujumbe kutoka Benki ya Dunia ulipotembelea na kukagua ujenzi wa Jengo Jipya la Makao Makuu ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu linalojengwa mkoani Dodoma.

(Picha: Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-WFM)

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MAJARIBIO YA UTAFITI WA HALI YA UMASIKINI UNAENDELEA KUFANYIKA MKOANI DODOMA NA KILIMANJARO
MAJARIBIO YA UTAFITI WA HALI YA UMASIKINI UNAENDELEA KUFANYIKA MKOANI DODOMA NA KILIMANJARO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhFcd32qY7nsHRmk3HgKNnxK8NFW3Y2bxvr37uAk1fNEDG9Ie3z74P7H7Fp3U6YBje9CUekoKBp7dyGlKK-qHd7ywyD12dpaR3ZksTP_CIFwO_wG6V1T3xkvJpnSF32u5Srn6jB9BQIvRY/s640/PICHA+1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhFcd32qY7nsHRmk3HgKNnxK8NFW3Y2bxvr37uAk1fNEDG9Ie3z74P7H7Fp3U6YBje9CUekoKBp7dyGlKK-qHd7ywyD12dpaR3ZksTP_CIFwO_wG6V1T3xkvJpnSF32u5Srn6jB9BQIvRY/s72-c/PICHA+1.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/majaribio-ya-utafiti-wa-hali-ya.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/majaribio-ya-utafiti-wa-hali-ya.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy