MAGRETH SINYANGWA WA KILOSA MOROGORO AKABIDHIWA MILIONI 20 ZA BIKO

Na Mwandishi Wetu, Morogoro MJASIRIAMALI mwanamke mwenye umri wa miaka 26, Magreth Sinyangwa amekabidhiwa jumla ya Sh Milioni 20 ...

Na Mwandishi Wetu, Morogoro
MJASIRIAMALI mwanamke mwenye umri wa miaka 26, Magreth Sinyangwa amekabidhiwa jumla ya Sh Milioni 20 za ushindi wa bahati nasibu ya Biko, aliyoupata katika droo kubwa iliyochezeshwa juzi Jumatano, jijini Dar es Salaam, huku akiwa mwanamke wa kwanza kuibuka na ushindi huo.

Sinyangwa amekabidhiwa fedha hizo Kilosa katika benki ya NMB, mkoani Morogoro na Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven, ambaye pamoja na mambo mengine, alimpongeza mshindi huyo na kumtaka azitumie fedha zake kwa uangalifu pamoja na kuboresha maisha yake ya kila siku.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Heaven alisema ni wakati wa kutajirika kwa kutumia vyema bahati nasibu ya Biko, ‘Ijue Nguvu ya Buku’ iliyozidi kuchanja mbuga na kutoa mamilioni ya Sh kwa washindi wa droo kubwa zinazofanyika Jumatano na Jumapili, sanjari na zawadi za papo kwa hapo.

“Tunajivunia kumpata mshindi mwanamke ambaye leo (jana) tumemkabidhi zawadi yake ya Sh Milioni 20, tukiamini kuwa atazitumia vizuri katika kuhakikisha kwamba anakuza biashara zake, ukizingatia kuwa tayari yupo kwenye tasnia ya biashara kabla ya kupata donge nono la Biko.

“Kucheza ni rahisi kwa sababu Biko inachezwa kwenye simu za Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel Money, ambapo mtu atafanya muamala kuanzia Sh 1,000 na kuendelea ambapo ataweka namba ya kampuni ambayo ni 505050 na ile ya kumbukumbu ni 2456, huku mbali na donge nono la Sh Milioni 20 linatoka kila Jumatano na Jumapili, pia zipo zawadi za papo hapo kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni,” Alisema Heaven.

Naye Sinyangwa alishindwa kuzuia furaha yake baada ya kukabidhiwa fedha zake, akisema kuwa ameshukuru ushindi wake huo akisema maisha yake yatabadilika kwa sababu atatumia biashara zake zipanuke kwa kutumia vyema ushindi huo wa Biko uliompatia mamilioni ya fedha.

“Huu ni wakati wa kusonga mbele kiuchumi kwa kutumia fedha hizi ambazo nimezipata bila kutarajia, hivyo nawaomba akina mama wenzangu pamoja na Watanzania wote kucheza Biko kwa sababu kila mtu anaweza kushinda bila kuangalia yupo wapi na anaishi vipi.

“Mimi nipo Kilosa Morogoro, lakini nilishangaa nilipopigiwa simu na mtu anayeitwa Kajala Masanja na kuniambia kuwa nimeshinda Biko, lakini nzuri zaidi leo (jana) wameniletea fedha zangu hadi ninapoishi jambo ambalo naona si la kawaida na ni la pekee kwa hawa Biko,” Alisema.

Mbali na kukabidhiwa fedha hizo jumla ya Sh Milioni 20, Biko pia tayari wametoa zaidi ya Sh Milioni 500 kwa washindi wake walioshinda katika mwezi Mei pekee, ikiwa ni siku chache tangu kuanzishwa kwa bahati nasibu hiyo inayotikisa katika kona mbalimbali hapa nchini..
Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven kulia akiwa katika makabidhiano ya Sh Milioni 20 kwa mshindi wao wa Kilosa, mkoani Morogoro, Magreth Senyangwa aliyeibuka kidedea katika droo kubwa iliyofanyika Jumatano iliyopita. Kushoto ni mume wa Magreth, Bahati Ramadhani na mwingine ni Ofisa wa NMB Tawi la Kilosa, akiwa kwenye makabidhiano hayo.
Mshindi wa donge nono la Sh Milioni 20 kutoka Kilosa, mkoani Morogoro, Magreth Senyangwa akiwa ameshika fedha zake baada ya kukabidhiwa kutoka kwa waendeshaji wa bahati nasibu ya Biko.
Meneja Masoko wa Biko Goodhope Heaven kushoto akiwa ameshika hundi tayari kwa kumkabidhi mshindi wao wa Sh Milioni 20 wa Kilosa Morogoro, Magreth Senyangwa, wa pili kutoka kushoto akifuatiwa na mumewe Bahati Ramadhan pamoja na familia yao.
Mshindi wa Sh Milioni 20 kutoka Biko, Magreth Senyangwa, akiwa amebeba fedha zake mara baada ya kukabidhiwa na waendeshaji wa bahati nasibu hiyo.
Meneja Masoko wa Biko, Goodhope Heaven kulia akiwa katika makabidhiano ya Sh Milioni 20 kwa mshindi wao wa Kilosa, mkoani Morogoro, Magreth Senyangwa aliyeibuka kidedea katika droo kubwa iliyofanyika Jumatano iliyopita. Kushoto ni Ofisa wa NMB Tawi la Kilosa, akiwa kwenye makabidhiano hayo.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: MAGRETH SINYANGWA WA KILOSA MOROGORO AKABIDHIWA MILIONI 20 ZA BIKO
MAGRETH SINYANGWA WA KILOSA MOROGORO AKABIDHIWA MILIONI 20 ZA BIKO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiFpV01TkgusFpmDfO9kNn74ia_iIUAYqEKyo8S9h9RU2gMh6FLpOS3rxRFo-FRzX5tyoFI17uL0e1Dv24rP4AklKW_H541s0m84F5ruKqM7_SrAdWeLFviLkBxxAZwgpnPLb_ysb5izcw/s640/_H4A9800.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiFpV01TkgusFpmDfO9kNn74ia_iIUAYqEKyo8S9h9RU2gMh6FLpOS3rxRFo-FRzX5tyoFI17uL0e1Dv24rP4AklKW_H541s0m84F5ruKqM7_SrAdWeLFviLkBxxAZwgpnPLb_ysb5izcw/s72-c/_H4A9800.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/magreth-sinyangwa-wa-kilosa-morogoro.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/magreth-sinyangwa-wa-kilosa-morogoro.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy