KITUO CHA UWEKEZAJI (TIC) CHAANDAA MAFUNZO YA SIKU SITA KWA WAJASIRIAMALI JIJINI DAR ES SALAAM

Bw. Godfrey Mwambe Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) akizungumza na waandishi wa habari wakati akielezea kuhusu kuhusu semin...



Bw. Godfrey Mwambe Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) akizungumza na waandishi wa habari wakati akielezea kuhusu kuhusu semina ya wajasiriamali inayotarajiwa kuanyika kwa kipindi cha siku sita kuanzia tarehe 26 Juni Mpaka tarehe 01 Julai katika Hoteli ya New Afrika hapa hapa jijini Dar-es-salaam, Mkutano huo umefanyika katika ofisi za kituo hicho jijini Dar es salaam leo.
Bw. Godfrey Mwambe Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye mkutano huo uliofanyika katika ofisi za kituo hichi jijini Dar es salaam.

………………………………………………………………………………….

Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kwa kushirikiana na Shirika la biashara na Maendeleo la Umoja wa Mataifa UNCTAD, limeandaa mafunzo maalumu ya kuwajengea uwezo wajasiriamali wadogo mafunzo ambayo yatafanyika kwa kipindi cha siku sita kuanzia tarehe 26 Juni Mpaka tarehe 01 Julai katika Hoteli ya New Afrika hapa hapa jijini Dar-es-salaam.

Lengo la program hii muhimu na endelevu kwa Wajasiriamali wa Kati (SMEs) na makampuni makubwa ni kuwajengea uwezo wafanyabiashara hao wadogo ili waweze kufanyabiashara na kutoa huduma kiufanisi na tija zaidi baina yao na hayo makampuni makubwa ya kigeni yaliyopo hapa nchini. Semina hii itawasaidia pia katika kuongeza mbinu na ujuzi katika kuibua fursa mpya, kudumisha biashara baina ya makampuni madogo na makubwa, kuwafundisha namna ya kupata taarifa sahihi za kibiashara, kuongeza ubora na viwango vya bidhaa na huduma wanazotoa na kuongeza ujasiri katika kuendesha biashara zao.

Vilevile lengo lingine muhimu la programu hii ni kuwaunganisha wafanyabiashara hao na wadau mbalimbali yaani BDSPs kama vile taasisi za fedha, wataalam mbalimbali wa huduma za biashara, masoko, biashara na tafiti mbalimbali ili kuwapa ujuzi wa kisekta mbalimbali zinazolenga katika kuboresha bidhaa na huduma zao.

TIC inategemea kuwa baada ya mafunzo hayo wafanyabiashara hao watakuwa wamejengewa uwezo na mitizamo chanya ili baadae waweze kutoa bidhaa na hudumu zinazokidhi ubora na viwango.

Kama Serikali tumekuwa tukihimiza na kutunga sheria na miongozo mbalimbali kuwafanya wawekezaji wakubwa wa nje na wa ndani kutoa fursa kwa makampuni madogo madogo kufanya biashara nao. Lakini mtakubaliana nami kwamba changamoto kubwa ya utekelezaji wa jambo hili ni kushidwa kuwa na uwezo kwa wajasiliamali wetu kufanya biashara na makampuni haya kiufanisi. Mafunzo haya yanalenga katika kusadia kuondoa changamoto hizo.

Mwisho kabisa, napenda kutoa rai kwa wafanyabiashara watakaopata fursa ya kuweza kujengewa uwezo waweze kuzingatia sana mada zitakazotolewa na wawezeshaji hawa. Nina hakika kwa kufanya hivyo tutaweza kuondokana na changamoto za kutokuwa wadau endelevu katika mfumo wa uchumi wetu.

IMETOLEWA NA MKURUGENZI MTENDAJI TIC,

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: KITUO CHA UWEKEZAJI (TIC) CHAANDAA MAFUNZO YA SIKU SITA KWA WAJASIRIAMALI JIJINI DAR ES SALAAM
KITUO CHA UWEKEZAJI (TIC) CHAANDAA MAFUNZO YA SIKU SITA KWA WAJASIRIAMALI JIJINI DAR ES SALAAM
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh18-nKRwnxAAI9e1LjQHSYfz0wHSKpUTUfmODKAQeVldlh_qIQcbqH8u0MJzYPrd675cwA4DowncaJE-qXHupsyKayayN7ZaidC6QibQBVS8FpW8quejXqg-b7puD-CS_1klipR5cv2JU/s640/god01.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh18-nKRwnxAAI9e1LjQHSYfz0wHSKpUTUfmODKAQeVldlh_qIQcbqH8u0MJzYPrd675cwA4DowncaJE-qXHupsyKayayN7ZaidC6QibQBVS8FpW8quejXqg-b7puD-CS_1klipR5cv2JU/s72-c/god01.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/kituo-cha-uwekezaji-tic-chaandaa.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/kituo-cha-uwekezaji-tic-chaandaa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy