KAMPUNI YA TRUMARK YATOA ZAWADI YA EID EL-FITR KWA WATOTO YATIMA JIJINI DAR ES SALAAM

  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Trumark, Agnes Mgongo akizungumza na wanahabari wakati wa kutoa zawadi kwa watoto Yatima wa Kituo...





 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Trumark, Agnes Mgongo akizungumza na wanahabari wakati wa kutoa zawadi kwa watoto Yatima wa Kituo cha Mtoto Wetu Tanzania jijini Dar es Salaam leo.


 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Trumark, Agnes Mgongo akiwa amekaa na watoto wa kituo hicho.
 Mratibu wa Miradi wa Kampuni hiyo, Gasparino Haule akiongoza kucheza katika hafla hiyo.
 Ofisa  Rasilimali Watu wa Kampuni hiyo, Grace Zikwaze, akizungumza na watoto hao.
 Keki maalumu ya hafla hiyo ikikatwa kwa pamoja. Kushoto ni Makamu Mkurugenzi wa Kituo hicho, Theobald Truphone na katikati ni  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Trumark, Agnes Mgongo. Wengine ni maofisa wa Kampuni ya Trumark.
 Zawadi zikitolewa.
 Mwanafunzi Shafii Hassan wa kituo hicho akizungumza 
kwenye hafla hiyo.
 Mwanafunzi Wanswekula Zacharia akizungumza na wanahabari kuhusu changamoto walizonazo.
 Nguo zikiandaliwa tayari kukabidhiwa watoto hao.
 Keki maalumu kwa ajili hayo iliyotolewa na Kampuni hiyo.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Trumark, Agnes Mgongo akiwalisha keki watoto hao.
 Watoto wakiserebuka.
 Ofisa Utawala wa Kampuni hiyo, Azavery Phares akimkabidhi keki hiyo maalumu, mtoto Godwin Steven.
 Picha ya pamoja kabla ya kuicharanga keki hiyo tayari kwa kuila.




 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Trumark, Agnes Mgongo akiwa na watoto wake kwenye hafla hiyo.





Na Dotto Mwaibale

JAMII imetakiwa kujenga moyo wa kusaidia watu waliopo katika makundi yenye uhitaji ili nao wajisikie kama watu wengine waliopo katika familia.

Mwito huo umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Trumark inayojishughulisha na uwezeshaji  jamii, Agnes Mgongo wakati kampuni hiyo  ilipokuwa ikitoa zawadi ya Sikukuu ya Eid El-Fitr katika Kituo cha watoto Yatima  cha Mtoto Wetu Tanzania kilichopo Kimara Suca jijini Dar es Salaam leo hii.

"Ni vizuri jamii ikajenga tabia ya kuwakumbuka watoto na watu wengine waliopo  katika makundi maalumu kwa kuwafariji badala ya kuiachia serikali ambayo ina mambo mengi ya kufanya" alisema Mgongo.

Alisema kampuni yake iliguswa na changamoto walizonazo watoto waishio katika kituo hicho ikaona ni vizuri katika kipindi hiki cha sikukuu ya Eid El-Fitr wakajumuike nao kwa kula na kucheza pamoja na kuwapa zawadi mbalimbali.

Mgongo alitaja zawadi walizotoa kupitia wadau wengine marafiki wa taasisi hiyo kuwa ni nguo, vinywaji na chakula ambacho kilipikwa katika kituo hicho.

Akizungumzia changamoto wanazokumbana nazo watoto waliopo katika makundi yenye  uhitaji, Wanswekula Zacharia alisema ni pamoja na vitabu, karo, sare za shule na  mahitaji mengine.

Alisema pamoja na kuwepo kwa changamoto hizo mwanafunzi anapaswa kujua wajibu wake akiwa shuleni ni kusoma na si vinginevyo.

Alisema kupokea misaada ni jambo moja lakini hata mtu kufika tu kituoni hapo na  kuwajulia hali bila ya kuwa na kitu chochote ni jambo la heri kwani wanachohitaji  zaidi ni kujumuika na jamii na kupata faraja.

Mwanafunzi wa kidato cha sita, Shafii Hassan ambaye analelewa katika kituo hicho  tangu akiwa mdogo anasema misaada wanayoipata imekuwa ikiwafanya wapate faraja  ukizingatia ukubwa wa changamoto walizonazo.

Makamu Mkurugenzi wa Kituo hicho,Theobald Tryphone aliishukuru kampuni hiyo kwa  msaada huo na kueleza changamoto kubwa walizonazo ni ada za wanafunzi, chakula,  ulipaji wa umeme na kuwa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroad) wameweka alama za x  katika majengo yao waondoke lakini suala hilo linashughulikiwa na Manispaa ya  Ubungo kuona jinsi itakavyowasaidia kuwasaidia kupata eneo jingine kwa ajili ya 
kujenga kituo hicho.

Mtoto analelewa katika kituo hicho, Godwin Steven alitoa shukurani kwa kampuni  hiyo kwa niaba ya wenzake kwa msaada huo.

(Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712727062)

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: KAMPUNI YA TRUMARK YATOA ZAWADI YA EID EL-FITR KWA WATOTO YATIMA JIJINI DAR ES SALAAM
KAMPUNI YA TRUMARK YATOA ZAWADI YA EID EL-FITR KWA WATOTO YATIMA JIJINI DAR ES SALAAM
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj-QGRb1hUsKeKL6N04EK7loqslLvYr2Ad0VfZfHSj1FDd4s9V8zBKVeHYVi8ZjoaXcry49uSb-ZWxLwWZxHXHb4pzYpsOnHWIPnzKoc1xg8iC_T97u9D9cA0X_2oWwEjQy4WMZ5JoTXoyb/s640/1.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj-QGRb1hUsKeKL6N04EK7loqslLvYr2Ad0VfZfHSj1FDd4s9V8zBKVeHYVi8ZjoaXcry49uSb-ZWxLwWZxHXHb4pzYpsOnHWIPnzKoc1xg8iC_T97u9D9cA0X_2oWwEjQy4WMZ5JoTXoyb/s72-c/1.JPG
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/kampuni-ya-trumark-yatoa-zawadi-ya-eid.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/06/kampuni-ya-trumark-yatoa-zawadi-ya-eid.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy