Mshambulaji wa kitanzania Jerome Nturukundo (kushoto) anayekipiga katika timu ya Nakuru Stars ya nchini Kenya. Na Zainab N...
Mshambulaji wa kitanzania Jerome Nturukundo (kushoto) anayekipiga katika timu ya Nakuru Stars ya nchini Kenya.
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
Mshambulaji
wa timu ya Nakuru All Stars Mtanzania Jerome Nturukundo amesema kuwa
mechi yao dhidi ya Simba itakuwa ni ngumu sana ila watahakikisha
wanafanya vizuri ili kuingia hatua ya nusu fainali.
Nakuru
wanatakutana na mabingwa wa kombe la FA Simba katika mchezo wa mtoano
utkaoafanyika leo saa 10:15 alasiri kwenye dimba la uwanja wa Uhuru.
Nturukundo
amesema kuwa wanajua Simba ni timu nzuri sana lakinina wao wamekuja
kupambana na kuhakikisha wanapata ushindi na kuingia hatua inayofuata.
"Tutajua
simba ni team nzuri lakini na sisi pia tunekuja kiushindani na
wafahamu timu yetu imekamilika na leo wapo katika wakati mgumu kwa
sababu sisi pia tumekuja kushinda,"amsema Jerome
Kwa upande wa beki wa kati James sadicky mukhwana yeye
amesema kuwa ujio wao Tanzania ni kwa ajili ya kuhakikisha wanapat
ushindi katika michezo yao na malengo yao ni kuona kombe la Sportpesa
Super Cup likienda nchini Kenya.
"Simba
wasifikiri itakua rahisi kuweza kuoata ushindi katika mchezo wetu wa
leo kwani tunataka kombe liiende nyumbani Nchini Kenya na mimi kama
mlinzi nitahakikisha hakuna makosa yatakayofanyika katika eneo
langui,"amesema mukhwana.
Timu ya Nakuru inanolewa na kocha mzawa George Maina imekuja nchini katika michuano ya Sportpesa Super Cup iliyoandaliwa na kampuni ya michezo ya kubahatisha ya Sportpesa.
COMMENTS