NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR. NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar , Abdulla Juma Saadalla “ Mabodi” amesema CCM itaendelea kufanya...
NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.
NAIBU
Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar , Abdulla Juma Saadalla “ Mabodi” amesema
CCM itaendelea kufanya ushindani wa sera za maendeleo zitakazowanufaisha
wananchi wa makundi yote mijini na vijijini.
Kauli
hiyo ameitoa wakati akifungua Mafunzo ya Wanawake na Uongozi kwa
wanachama na viongozi wa UWT Mkoa wa Mjini huko Amani Zanzibar, Dkt.
Mabodi alisema wananchi wa visiwa vya Zanzibar kwa sasa wanachohitaji ni
siasa za ushindani wa kisera katika kukuza kipato cha mwananchi mmoja
mmoja hadi taifa kwa ujumla.
Dkt.
Mabodi alisema taifa lolote linalotamani kuendelea kiuchumi ni lazima
wananchi wake wakubali kwa vitendo dhana ya siasa za ustaarabu katika
kudumisha amani na utulivu wa nchi ili kufanya kazi za kujiongezea
kipato na kukuza uchumi wa nchi.
Aidha
Naibu Katibu Mkuu huyo alisema ushindi wa CCM katika chaguzi mbali mbali
za dola unatokana na nguvu za Wanawake wa UWT katika kuunga mkono
harakati mbali mbali za kisiasa hadi kuhakikisha chama kinaingia
madarakani.
“ kila
mtu ndani ya Chama Chetu anajua na kutambua mchango wa Wanawake katika
medali za kisiasa, wao ndio wamekuwa mstari wa mbele kwa kila kitu
ikiwemo kujitokeza kwa wingi kupiga kura halali za kuiletea ushindi CCM.
Pia
nakuahidini kwamba nitaendelea kuwa nanyi bega kwa bega kwa lengo la
kuimarisha chama na jumuiza zake sambamba na kuwaletea wananchi
maendeleo ya kudumu.”, alisema Dkt. Mabodi.
Kupitia
Mkutano huo Dkt. Mabodi aliwasihi viongozi na watendaji wa Umoja wa
Wanawake Tanzania kushuka ngazi za chini za uongozi hasa matawi na
mashina kwa lengo la kuratibu changamoto zinazowakabili wananchi ili
zitafutiwe ufumbuzi wa kudumu na serikali.
Aliwapongeza
viongozi wa UWT waliojitolea kuanzisha mafunzo ya uongozi kwa wanawake
wenzao ili wapate ujuzi wa kufanya siasa za maendeleo zitakazowajengea
ujasiri wa kujenga hoja imara zinazokubalika katika ulimwengu wa siasa
za ushindani.
Sambamba
na hayo alimpongeza Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa
Zanzibar Dkt. John Pombe Magufuli kwa juhudi zake za kulinda rasilimali
za nchi hasa kuthibiti mianya ya usafirishaji wa Mchanga wa Madini
unaosababisha upotevu wa fedha nyingi za umma.
Akizungumzia
Uchaguzi wa ngazi ya Wadi unaoendelea hivi sasa katika Chama na Jumuiya
aliagiza kwamba kamati zinazosimamia zoezi hilo zifanye kazi ya ziada
ya kuhakikisha wanapatikana viongozi safi wasiokuwa na sifa za usaliti.
Mapema
akizungumza katika Mkutano huo Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Mjini, Bi.
Waridi Juma Othman aliahidi kuwa wanawake hao watatumia vizuri mafunzo
ya uongozi katika siasa kama muongozo wa kufanya kazi za kisiasa kwa
ufanisi mkubwa.
Akitoa
neno la shukrani Mbunge wa Viti Maalum wanawake( MNEC), Khadija Hassan
Aboud alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo wanawake wa CCM
ili waweze kuzitumika vizuri fursa za uongozi zinazopatikana ndani ya
chama na serikali kwa ujumla.
Mafunzo
hayo ya siku moja yameandaliwa na Mbunge wa Viti Maalum wanawake(
MNEC), Khadija Hassan Aboud kwa kushirikiana na Mbunge wa Viti Maalum
Mkoa wa Mjini, Faharia Shomari Shomari Khamis.
COMMENTS