Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela akizungumza na blog hii juu ya kitu kinachiendelea kwenye mgodi wa nyakavangala. N...
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela akizungumza na blog hii juu ya kitu kinachiendelea kwenye mgodi wa nyakavangala.
Na Fredy Mgunda, Iringa
Wachimbaji
wa madini katika mgodi wa nyakavangala wamefukiwa na mchanga kutokana
na wachimbaji hao kuingia kinyume cha makubaliano yaliyowekwa baina ya
wachimbaji na Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela.
Akizungumza
na blog hii Kasesela alisema kuwa Jana mida ya saa 1 jioni Duara la
mgodi mmoja ulioko Nyakavangala uliporomoka na kufukia wachimbaji 4 .
"Inasemekana
wachimbaji hao walikuwa wameingia kuiba kwani duara hilo ni kati ya
maduara ambayo Mkuu Wa wilaya ya Iringa Mhe Richard Kasesela aliifungia
ili ijengwe nguzo na ngao" alisema Kasesela
Kasesela
alisema kuwa Watu 4 waliingia mgodini baada ya mafundi Wa ujenzi Wa
ngao kupumzika kwa vile ni usiku ndipo wachimbaji nao wakaingia mgodini
bila ruhusa
"Hadi
sasa tumefanikiwa kuokoa 3 mpaka sasa huyo mmoja hajaokolewa bado yupo
ndani ya mgodi kutokana na changamoto za uokoaji ili Juhudi zinaendelea
za kumuokoa huyo mmoja" alisema Kasesela
Kasesela
alisema kuwa changamoto ilikuwa ni namna ya kumuokoa kwani sehemu
iliyokuwa imejifukia juu mwamba mwingine ulionekana kuwa na dalili za
kushuka.ikawapasa kujengea kwanza eneo hilo kazi iliyochukua mda mrefu
na ndipo waaze kuokoa.kwahiyo tunasubiri hatua nyingine sasa.
"Naendelea
kuwaonya wachimbaji wasiendelee na uchimbaji eneo la chini maarufu kama
kwenye "vein" mpaka wajenge ngao ili wasihatarishe maisha yao.
Wakiendelea na kiburi tutaamua tufunge mgodi" alisema Kasesela
COMMENTS