Kulia ni daktari feki ambaye amekuwa akijitambulisha kwamba ni Dk Abdallah Juma ambaye amekuwa akifanya ka...
Kulia
ni daktari feki ambaye amekuwa akijitambulisha kwamba ni Dk Abdallah
Juma ambaye amekuwa akifanya kazi katika Maabara Kuu, katika Hospitali
ya Taifa Muhimbili (MNH). Kulia ni mmoja wa askari wa Muhimbili
aliyemkamata daktari huyo.
………………………………………………………………………
Hospitali
ya Taifa Muhimbili (MNH) imemtia mbaroni kijana mmoja aliyekuwa
akijifanya daktari na alikuwa akijitambulisha kwa wagonjwa kwamba
anaitwa Dk Abdallah Juma.
Mtu
huyo alikuwa akijifanya kutoa huduma katika Maabara Kuu. Uongozi wa
hospitali hiyo umesema kuwa kijana huyo ni daktari feki na si daktari
kama alivyokuwa akijitambulisha na kwamba amekamatwa baada ya kuwekewa
mtego na askari wa hospitali hiyo.
Uongozi wa hospitali hiyo umesema kuwa walinzi walikuwa wakimtilia shaka na kuanza kumfuatilia hadi walipofanikiwa kumkamata.
Mkuu
wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Wateja wa Hospitali hiyo,
Aminiel Aligaesha amesema hospitali imeweka mikakati mbalimbali ya
kupambana na wahalifu wakiwamo watu wanaojiita ni madaktari kama huyo
ambaye amekamatwa leo Juni 19, 2017.
COMMENTS