Na MWANDISHI WETU Wananchi wa Arumeru wameanza kunufaika na mradi wa Kuimarisha upatikanaji wa taarifa za hali ya hewa na Mfumo...
Na MWANDISHI
WETU
Wananchi wa Arumeru wameanza
kunufaika na mradi wa Kuimarisha upatikanaji wa taarifa za hali ya hewa na
Mfumo wa Tahadhari unaoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kufungiwa mitambo
ya kisasa ya kutoa taarifa za hali ya hewa na tahadhari.
Zaidi ya mitambo 40
imefungwa nchi nzima ikiwa Arumeru na Liwale ni moja ya wilaya za mfano
ambazo mitambo hiyo imekuwa ikisaidia
Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini kutoa taarifa za
utabili wa hali ya hewa zenye
uhakika na uharaka.
Mradi huo mpaka sasa
umefanikiwa kufunga Mitambo katika maeneo ya Mbuguni, Hifadhi ya Taifa Arusha,
Lyamungo, Manyara, Babati Longido, maeneo ya Bonde la Mto Pangani,Lushoto
pamoja na Mombo.
Wakizungumza na Watumishi wa
Ofisi ya Waziri Mkuu waliofanya tathimini ya utekelezaji wa mradi huo,wakazi wa
Arumeru wamesema tangu mitambo hiyo
ilipofungwa wamekuwa wanufaika wakubwa.
“Sisi wakulima na wafugaji
wa Mbuguni tumefaidika sana na uwepo wa mitambo ya kisasa ya utoaji wa taarifa
za hali ya hewa katika maeneo yetu kwani kumesaidia wakulima kulima mazao
yanayoendana na hali ya hewa na kuondokana na athari za mafuriko kwa kuzingatia
taarifa za utabiri zinazotokana na mitambo iliyofungwa” alibaini Bi.Pepetua
Mafia
Pamoja na hilo walikiri
ongezeko la tahadhari kwa kuwa Mamlaka ya Hali ya Hewa imekuwa ikituma jumbe
fupi za taarifa za utabiri wa hali ya hewa kwa maeneo yao katika simu za
mkononi walizopewa na mradi huo.
“Tunafarijika na tunaona umuhimu
wa taarifa za utabiri zinazotumwa katika simu hizi tulizopewa na mradi huu
kwani imekuwa rahisi kujua vipindi mbalimbali vya hali ya hewa na kutusaidia
kuweza kupanga shughuli za uzalishaji ikiwemo kilimo na ufugaji wenye tija
ambapo kila baada ya siku kumi tunapokea jumbe kutoka Mamlaka ya hali ya
hewa”alisisitiza mkazi wa Shambarai Bi.Elizabeth Laiza
Aidha pamoja na mafanikio
hayo wakazi wa Arumeru waliomba Serikali kuongeza vituo na kujengewa uwezo
zaidi ili kuepuka changamoto za uelewa mdogo wa taarifa za hali ya hewa.
“Tunaiomba Serikali
itujengee uwezo zaidi juu ya umuhimu wa taarifa za hali ya hewa na tahadhari
ili kutatua changamoto za kutojali taarifa hizo na kusaidia kuyakabili majanga
ya mafuriko na ukame yanapotokea.” alisema Bw. Elibokea Lukio mkazi wa
Maloloni.
Kwa upande wake, Mkurugenzi
Msaidizi masuala ya Bajeti Ofisi ya Waziri Mkuu Bi. Grace Mosha alipongeza
jitihada zilizopo za waratibu wa Ofisi
yake kwa kushirikiana na wadau ikiwemo Wizara na Maji na Umwagiliaji Bodi ya
Bonde la Mto Pangani, Wizara ya Kilimo na Mifugo na Mamlaka ya Hali ya Hewa
Nchini na kuwaomba kuendelea kutekeleza mradi huu ikiwezekana kuongeza mitambo
hiyo kulingana na uhitaji.
“Niwapongeze wadau wote wa
mradi kwani mradi umekuwa na matokeo chanya kwakuwa wananchi wamekiri na kuomba
Serikali ifunge mitambo mingi zaidi ili kuifikia nchi nzima badala ya mitambo
iliyopo sasa”.Alisisitiza Bi.Mosha
AWALI:Mradi
wa Kuimarisha Taarifa za Hali ya Hewa na Mfumo wa Tahadhari ni mradi wa mfano
na utekelezaji wake ni katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale mkoani Lindi na
Arumeru mkoani Arusha ambapo umelenga kuwajengea uwezo wananchi katika kupata
taarifa za tahadhari zitazosaidia kujiandaa, kukabili hali pindi
unapotokea Ukame na Mafuriko ikiwa ni
maeneo yanayoathiriwa zaidi. Mradi huu ulianza kutekelezwa rasmi mwaka 2015
Ukiwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa ufadhiri wa Shirika la Maendeleo la
Umoja wa Mataifa (United Nations Development Programme)
COMMENTS