Kaimu Mkurugenzi mkuu wa VETA nchini ,Bwire Ndazi akizungumza wakati wa uzinduzi wa programu mpya ya mafunzo ya ufundi stadi kupita...
Kaimu
Mkurugenzi mkuu wa VETA nchini ,Bwire Ndazi akizungumza wakati wa
uzinduzi wa programu mpya ya mafunzo ya ufundi stadi kupita mtandao wa
airtel kwa watu waliopo mbali na vyuo inayokwenda kwa jina la VSOMO
|
Mkurugezni
wa Mawasiliano wa kampuni ya Airtel Tanzania ,Betrice Singano
akizungumza na waandishi wa habaari waati wa uzinduzi wa programu ya
VSOMO inayoendeshwa na kampuni ya Airtel kwa kushirikiana na Mamlaka ya
Ufundi Stadi nchini VETA
|
Mkurugezni
wa Mawasiliano wa kampuni ya Airtel Tanzania ,Betrice Singano
akizungumza na waandishi wa habaari waati wa uzinduzi wa programu ya
VSOMO inayoendeshwa na kampuni ya Airtel kwa kushirikiana na Mamlaka ya
Ufundi Stadi nchini VETA
|
Kaimu
Mkurugenzi mkuu wa VETA nchini ,Bwire Ndazi Akionyesha Application
iliyopo kwenye simu ya Airtel ambayo itasaidia mtu anayyetumia mtandao
huo kujiunga na mafunzo y ufundi Stadi Popote pale alipo kushoto ni
Mkurugezni wa Mawasiliano wa kampuni ya Airtel Tanzania ,Betrice Singano
na kulia ni Mkurugenzi wa VETA kanda ya Dar es Salaam Habibu Burko
akishuhudia
|
Mkuu
wa Chuo cha Veta Kipawa ,Mhandisi Luuciius ,luteganya akizungumza
wakati wa uzinduzi wa programu ya VSOMO Katika chuo cha VETA Kipawa.
Sehemu ya wanafunzi wa chuo cha VETA kipawa walio shuhudia tukio hilo la uzinduzi
Picha ya pamoja kati ya watendaji wa VETA,AIRTEL na Wanafunzi mara baada ya kumalizika kwa uzinduuzi wa programu ya VSOMO
Kampuni
ya simu za Mkononi ya Airtel Tanzania imeboresha huduma yake ya kutoa
elimu kwa njia ya mtandao inayokwenda kwa jina la VSOMO kwa kushirikiana
na mamlaka ya ufundi stadi nchini VETA kupitia chuo cha Kipawa.
Akizungumza
wakati wa kutangaza uongezwaji wa programu zingine 5 na kufanya kozi
zinazofundishwa kuwa 11 Mkurugenzi wa mahusiano wa kampuni ya Airtel
Tanzania , Beatrice Singano amesema mpango huo ni sehemu ya programu ya
Airtel Fursa inayoendeshwa na kampuni hiyo.
“Airtel
fursa imeendelea kuwa na mchango mkubwa katika kuelekea Tanzania ya
Viwanda kwa kuwawezesha watanzania kupata elimu ya ufundi stadi popote
pale walipo ili waweze kuajiriwa au kujiajiri katika mashirika
mabalimbali”alisema Singano.
Ametaja
kuwa Airtel Tanzania iimefaanya tafiti na kubaini kuwa vijaana wengi
wamekuwa waoga wa kujiunga na shule au kujiendeleza katika ufundi stadi
kwa hofu ya kupoteza wateja wao katika biashara wanazofanya pindi
wanapokwenda shule kutwa nzima.
Amesema
kuwa mpango huu wa elimu kwa njia ya mtandao ni moja ya fursa ambayo
itasaidia vijana wengi hivyo mtu anaehitaji kupata mpango huu anatakiwa
kujiunga na Airtel Tanzania hili aweze kunufaika na mpango huu.
Kwa
upande wake Kaimu mkurugenzi wa Veta,Bwire Ndazi ametaja kuwa mpango
huu ni muhimu sasa kwani utawezesha VETA kufikia malengo yake
iliyojiwekea ya kutoa elimu ya ufundi mpaka vijijini hili kuwawezesha
watanzania kupata elimu pale walipo.
Ametoa
wito kwa makampuni mengine kuiga mfano wa Airtel fursa kwa kuwezesha
tasisi za elimu kutoa mafunzo kwa njia ya kisasa zaidi.
COMMENTS