Na Shamimu Nyaki-WHUSM. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amepokea jumla ya shilingi ...
Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe
amepokea jumla ya shilingi 12,000,000 kutoka kwa Kampuni ya Multi
Choice, Taasisi
ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika Tawi la Tanzania (MISA TAN)
pamoja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa ajili
ya kuisaidia timu ya Serengeti Boys.
Dkt.
Mwakyembe amezipokea fedha hizo leo Jijini Dar es Salaam mbele ya
waandishi wa habari na kuahidi kutoa taarifa ya kiasi cha fedha
zilizochangwa na wadau mbalimbali mwishoni mwa mwezi huu.
“Nawashukuru
wadau wote wanaoendelea kuichangia timu yetu ya Serengeti Boys, leo
nimepokea shilingi 10,000,000 kutoka Kampuni ya Mult Choice, shilingi
1,000,000 kutoka MISA TAN pamoja na shilingi 1,000,000 kutoka TAKUKURU”,
alisema Dkt. Mwakyembe.
Ameongeza
kuwa timu imeanza mashindano hayo vizuri japokuwa wametoka bila
kufungana na timu ya Taifa ya Mali ambayo ndio mabingwa watetezi wa
kombe hilo.
Aidha,
ameahidi kuwa mchezo dhidi ya Timu ya Serengeti Boys na Timu ya Angola
itakayochezwa Mei 18 mwaka huu itarushwa moja kwa moja kupitia
Televisheni ya Taifa (TBC).
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa MISA TAN, Salome Kitomari amesema kuwa
waandishi wa habari wameamua kuisaidia timu hiyo sio kwa kutumia kalamu
zao kuwatangaza katika vyombo vya habari tu bali imeamua kuwasaidia kwa
kuwachangia fedha.
“Tumeamua
kuichangia timu yetu ili tuwape moyo zaidi wa kufanya vizuri kwani
wameonesha jitihada katika mchezo wa mpira wa miguu,” alisema Bi.
Salome.
COMMENTS