WAZIRI MWAKYEMBE APOKEA MILIONI 12 MCHANGO WA SERENGETI BOYS

Na Shamimu Nyaki-WHUSM. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amepokea jumla ya shilingi ...


Na Shamimu Nyaki-WHUSM.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amepokea jumla ya shilingi 12,000,000 kutoka kwa Kampuni ya Multi Choice, Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika Tawi la Tanzania (MISA TAN) pamoja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa ajili ya kuisaidia timu ya Serengeti Boys.

Dkt. Mwakyembe amezipokea fedha hizo leo Jijini Dar es Salaam mbele ya waandishi wa habari na kuahidi kutoa taarifa ya kiasi cha fedha zilizochangwa na wadau mbalimbali mwishoni mwa mwezi huu.

“Nawashukuru wadau wote wanaoendelea kuichangia timu yetu ya Serengeti Boys, leo nimepokea shilingi 10,000,000 kutoka Kampuni ya Mult Choice, shilingi 1,000,000 kutoka MISA TAN pamoja na shilingi 1,000,000 kutoka TAKUKURU”, alisema Dkt. Mwakyembe.

Ameongeza kuwa timu imeanza mashindano hayo vizuri japokuwa wametoka bila kufungana na timu ya Taifa ya Mali ambayo ndio mabingwa watetezi wa kombe hilo.

Aidha, ameahidi kuwa mchezo dhidi ya Timu ya Serengeti Boys na Timu ya Angola itakayochezwa Mei 18 mwaka huu itarushwa moja kwa moja kupitia Televisheni ya Taifa (TBC).

Kwa upande wake Mwenyekiti wa MISA TAN, Salome Kitomari amesema kuwa waandishi wa habari wameamua kuisaidia timu hiyo sio kwa kutumia kalamu zao kuwatangaza katika vyombo vya habari tu bali imeamua kuwasaidia kwa kuwachangia fedha.

“Tumeamua kuichangia timu yetu ili tuwape moyo zaidi wa kufanya vizuri kwani wameonesha jitihada katika mchezo wa mpira wa miguu,” alisema Bi. Salome.

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAZIRI MWAKYEMBE APOKEA MILIONI 12 MCHANGO WA SERENGETI BOYS
WAZIRI MWAKYEMBE APOKEA MILIONI 12 MCHANGO WA SERENGETI BOYS
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi2k7FGzrT5u41DHvX0vrjU1_Al4EIuAf6M0hGuxky5HAp3k9RdyjiwJy5vQ1bqUvALWA47TWsY9d32CFFgQvJ9LwVOO1lOFK7Z2wTYuPIk1BSICLa9Nw_DflkJmy98oIETx0Dy7IHbfEU/s400/pic%252Bindependent%252Bcandidacy.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi2k7FGzrT5u41DHvX0vrjU1_Al4EIuAf6M0hGuxky5HAp3k9RdyjiwJy5vQ1bqUvALWA47TWsY9d32CFFgQvJ9LwVOO1lOFK7Z2wTYuPIk1BSICLa9Nw_DflkJmy98oIETx0Dy7IHbfEU/s72-c/pic%252Bindependent%252Bcandidacy.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/waziri-mwakyembe-apokea-milioni-12.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/waziri-mwakyembe-apokea-milioni-12.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy