WAZIRI MUHONGO AKUTANA NA RAIS WA KAMPUNI YA TBEA YA CHINA

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amekutana na Rais wa Kampuni ya TBEA ya China, Zhang Xin kwa ajili ya kujadil...




Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amekutana na Rais wa Kampuni ya TBEA ya China, Zhang Xin kwa ajili ya kujadili masuala ya uwekezaji kwenye Sekta ya Nishati nchini.

Mkutano huo wa Waziri Muhongo na Rais huyo ambaye ameongozana na Ujumbe wake umefanyika Mei 21, 2017 jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Wataalamu kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Waziri Muhongo aliuelezea ujumbe huo baadhi ya fursa za uwekezaji kwenye Sekta ya Nishati nchini na kuwashauri wachague eneo ambalo wanahitaji kuwekeza ili taratibu zianze mapema.

“Fursa ni nyingi sana, ni nyinyi kuamua wapi mmelenga ili taratibu ziendelee ikizingatiwa kwamba dhamira ya Serikali ni kuhakikisha tunakuwa na Tanzania ya Viwanda,” alisema Waziri Muhongo.

Aliagiza wataalamu wa Wizara ya Nishati na Madini kukutana na Ujumbe huo hapo kesho ili kujadili kwa undani dhamira yao ya uwekezaji ikiwemo kuchagua eneo ambalo wangependa kuwekeza.

Kwa upande wake Xin alisema kampuni yake inaridhishwa na kasi ya Serikali ya Tanzania chini ya Uongozi wa Rais John Pombe Magufuli na hivyo wanatarajia kuwekeza kiasi cha Dola za Marekani bilioni 10 kwenye sekta mbalimbali ikiwemo Nishati, Barabara, Uendelezaji wa Miji, na Usafirishaji.

Alisema uchumi wa Tanzania umezidi kuimarika na hivyo kuzidi kuvutia wawekezaji kwenye maeneo mbalimbali hususan ikizingatiwa kuwa Tanzania ni Taifa lenye amani linalokuwa kwa kasi kubwa.

Ujumbe huo upo nchini Tanzania na unatarajia kukutana na Wizara mbalimbali ili kubaini fursa zaidi za uwekezaji nchini

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WAZIRI MUHONGO AKUTANA NA RAIS WA KAMPUNI YA TBEA YA CHINA
WAZIRI MUHONGO AKUTANA NA RAIS WA KAMPUNI YA TBEA YA CHINA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhkU69RBb86Vqmn2fdLQ3WYNd9cLEOm05gu7UIVYGeuVpF9BZdOthaeOaX5jLkUTGGyLZBChpDWsADNPadutVKYZFyoDDvaSfJvvOUOqFiYvuep_GLRloG0d2kuzM1zoG9p4H3eBNdG5zo/s640/MUHO1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhkU69RBb86Vqmn2fdLQ3WYNd9cLEOm05gu7UIVYGeuVpF9BZdOthaeOaX5jLkUTGGyLZBChpDWsADNPadutVKYZFyoDDvaSfJvvOUOqFiYvuep_GLRloG0d2kuzM1zoG9p4H3eBNdG5zo/s72-c/MUHO1.jpg
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/waziri-muhongo-akutana-na-rais-wa.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/waziri-muhongo-akutana-na-rais-wa.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy