WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUWA KARIBU NA WANANCHI, BALOZI MWINYI

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhani Mwinyi akitoa mwongozo kwa wajumbe w...

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhani Mwinyi akitoa mwongozo kwa wajumbe wa semina ya Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki inayoendelea kufanyika kisiwani Pemba. Pamoja na mambo mengine amewahimiza wananchi kuchangamkia fursa zinazopatikana kwenye mtangamano. 
 
Mbunge wa jimbo la Konga, Mhe. Mbarouk Ali akichangia jambo kwenye semina. 
Sehemu ya wajumbe wakiendelea kusikiliza mada mbalimbali zilizokuwa zikiendelea kutolewa kwenye semina. 
Afisa kutoka Ofisi za Uhamiaji Pemba Bw. Haji Kassim Haji akijibu hoja mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na wajumbe kwenye semina juu ya upatikanaji wa Hati ya Kusafiria ya Afrika Mashariki. 
Bw. Amedeusi Mzee akitoa mada kuhusu Soko la Pamoja na faida zinazopatikana kwenye soko hilo. 
Luteni wa JKU naye akitolea ufafanuzi kwenye maswala mbalimbali yenayohusiana na maswala ya magendo. 
Wajumbe wakisikiliza kwa makini mada na majibu ya hoja mbalimbali walizokuwa wakihitaji kufahamu kutoka kwa Bw. Amedeusi (hayupo pichani) na mjumbe kutoka JKU. 


Taasisi za Serikali zimehimizwa ziwe karibu na wananchi ili ziweze kuwahudumia na kuwaelimisha juu ya huduma inazozitoa. Wananchi wengi wamekuwa wakilalamika mara kwa mara kuhusu watumishi wa umma kutotumia weledi na ubunifu katika kuwahudumia wananchi jambo ambalo likiachwa liendelee, Tanzania itaachwa nyuma ndani ya Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na ulimwengu mzima kwa ujumla.

Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan Mwinyi katika semina kuhusu elimu ya mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na fursa zake inayotolewa na wataalamu wa Wizara yake kisiwani Pemba. Semina hiyo iliyoanza jana inafanyika kwenye uwanja wa Gombani, Pemba na itamalizika tarehe 18 Mei 2017.

"Kuna fursa nyingi za kiuchumi katika Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki lakini kama wananchi wetu hatutawasaidia na kuwaelimisha kuhusu nyaraka na masharti yanayokidhi vigezo wataachwa nyuma na kubaki kuwa watazamaji na walalamikaji" Balozi Mwinyi alisema.

Wajasiriamali walielezea masikitiko yao juu ya ugumu wa kupata hati za kusafiria kutokana na mlolongo wa masharti hususan, inapotokea kuwa safari ni ya ghafla. Aidha, wajasiriamali wamekuwa wakilalamika kuwa wanapata tabu kusajili bidhaa zao katika mamlaka zinazosimamia ubora wa viwango wa bidhaa, chakula na madawa kwa kuelezwa kwamba bidhaa zao ni duni, hivyo wameiomba Serikali iwawezeshe kupata teknolojia ya kisasa ikiwa ni pamoja na vifungashio.

Balozi Mwinyi alisisitiza umuhimu wa taasisi zote bila kukiuka Sheria, kanuni na vigezo vilivyowekwa kurahisisha taratibu zao ili wananchi wapate nyaraka zinazotakiwa kwa urahisi ili iwe wepesi kwao kuchangamkia fursa za kiuchumi na kibiashara katika soko la pamoja la Afrika Mashariki.

Akitoa ufafanuzi kuhusu upatikanaji wa hati za kusafiria, Afisa Uhamiaji, Bw. Haji Kassim Haji alisema kuwa taratibu zilizowekwa hazina lengo la kukwamisha shughuli ya mtu yeyote isipokuwa zimewekwa kwa kuzingatia maslahi mapana ya nchi. Katika ulimwengu wa leo ambao unakabiliwa na changamoto nyingi za kiusalama kama, ugaidi, uharamia, Biashara haramu ya binadamu, uhamiaji haramu, lazima masharti yazingatiwe ili kuepuka uwezekano wa kutokea uovu huo.

Aidha, Balozi Mwinyi alishauri wajasiriamali wajiunge katika vikundi ili masuala yao ikiwa ni pamoja na maombi ya hati za kusafiria yafanywe kwa pamoja wakidhaminiwa na taasisi zinazosimamia shughuli zao.


Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, 
Pemba, 16 Mei, 2017

COMMENTS

Name

analogia,2,Biashara,618,dijital,235,Jamii,3473,Magazeti,385,Michezo,334,Mikoani,1262,Moto,334,Sanaa,247,Siasa,369,Slide,10,tv,4,Uchumi,276,
ltr
item
Okandablogs: WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUWA KARIBU NA WANANCHI, BALOZI MWINYI
WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUWA KARIBU NA WANANCHI, BALOZI MWINYI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhJwotNroKUoP1qwIOVam02D9zmDBF5IZ_49xdeG5pVf9ncMudaIQqXSTy3Xf7hlgL1jMk49S3d6T1spr-9RdE_OSW308vsdN6-ct4Dv7Sxdd4r3MgXSe5EchrHDp543zfNTrPQDdAc1UzK/s640/719A6435.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhJwotNroKUoP1qwIOVam02D9zmDBF5IZ_49xdeG5pVf9ncMudaIQqXSTy3Xf7hlgL1jMk49S3d6T1spr-9RdE_OSW308vsdN6-ct4Dv7Sxdd4r3MgXSe5EchrHDp543zfNTrPQDdAc1UzK/s72-c/719A6435.JPG
Okandablogs
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/watumishi-wa-umma-watakiwa-kuwa-karibu.html
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/
http://robertokanda.blogspot.com/2017/05/watumishi-wa-umma-watakiwa-kuwa-karibu.html
true
7708052459372695991
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy