Ditha Nyoni - RUVUMA Raia nane kutoka nchi ya Ethiopia wamekutwa wamefariki katika kijiji cha Amani makolo taarafa ya kingonser...
Ditha Nyoni - RUVUMA
Raia
nane kutoka nchi ya Ethiopia wamekutwa wamefariki katika kijiji cha
Amani makolo taarafa ya kingonsera wilayani mbinga mkoani wa ruvuma huku
wengine 25 wakiwa hai wanashikiriwa na jeshi la polisi.
Habari
kutoka jeshi la polisi mkoa wa ruvuma kupitia kaimu kamanda wa polisi
ACP Dismas Kisusi zinasema raia hao wa Ethiopia walikuwa
wanasafirishwa kwenda nchi ya Afrika ya Kusini kupitia Upande wa Malawi mwa
katika ziwa Nyasa.
Vifo
vya Waithiopia hao vinatokana na kubebwa kwenye kontena la lori
wakitokea Namanga, Arusha hivyo kutokana na hali mbaya ya hewa hali zao
zilianza kubadilika na kupelekea kufariki. Huku miili ya marehemu hao
ikiwa imehifadhiwa katika hospitali ya wilaya Mbinga.
Jeshi
la polisi mkoa wa Ruvuma kwa kushirikiana na jeshi la uhamiaji
linaendelea na uchunguzi kubaini walioleta miili ya marehemu na wale
wasiliokamatwa hatua za kisheria zitafuatwa.
COMMENTS