Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dkt, Harrison Mwakyembe (kushoto) akikaribishwa na Mkuu wa kitengo cha Masoko na Ma...
Waziri
wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dkt, Harrison Mwakyembe (kushoto)
akikaribishwa na Mkuu wa kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom
Tanzania PLC, Nandi Mwiyombella alipowasili kwenye hafla ya utoaji wa
tuzo za washindi wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara, iliyoandaliwa na
wadhamni hao na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani city
jijini Dar es Salaam jana.
Waziri
wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dkt, Harrison Mwakyembe akimsikiliza
jambo kwa makini Mkurugenzi wa biashara wa Vodacom Tanzania, Hisham
Hendi (katikati) wakati wa hafla ya utoaji wa tuzo za washindi wa Ligi
kuu ya Vodacom Tanzania bara, iliyoandaliwa na kampuni hiyo ikiwa ndiyo
wadhamini wakuu wa ligi na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa
Mlimani city jijini Dar es Salaam jana, kulia ni Mkuu wa kitengo cha
Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania PLC, Nandi Mwiyombella.
Mkurugenzi
wa biashara wa Vodacom Tanzania,Hisham Hendi,akiongea wakati wa hafla
ya utoaji wa tuzo za washindi mbalimbali wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania
bara, iliyoandaliwa na kampuni hiyo ikiwa ndiyo wadhamini wakuu wa ligi
na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani city jijini Dar es
Salaam jana.
Waziri
wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dkt, Harrison Mwakyembe, akiongea na
wadau mbalimbali waliohudhuria hafla ya utoaji wa tuzo mbalimbali za
washindi wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara, iliyoandaliwa na
wadhamini wakuu wa ligi Vodacom Tanzania na kufanyika katika ukumbi wa
mikutano wa Mlimani city jijini Dar es Salaam.
Waziri
wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dkt, Harrison Mwakyembe, akipewa hongera
na Mkurugenzi wa biashara wa Vodacom Tanzania,Hisham Hendi baada ya
kuongea na wadau walioshiriki katika hafla ya utoaji tuzo mbalimbali za
washindi wa Ligi kuu bara, iliyoandaliwa na wadhamini wakuu wa ligi
Vodacom Tanzania na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani city
jijini Dar es Salaam, katikati ni Mkuu wa kitengo cha Masoko na
Mawasiliano wa Vodacom Tanzania PLC, Nandi Mwiyombella.
Mkuu
wa kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania PLC, Nandi
Mwiyombella akimkabidhi hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 84/-
Katibu mkuu wa Yanga, Boniface Mkwasa baada ya timu yao kuibika mabingwa
wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara 2016/2017 wakati wa halfa ya
utoaji tuzo mbalimbali jana katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es
Salaam.
Mkurugenzi
wa masoko wa Vodacom Tanzania, Ashutosh Tiwary (kushoto) akimkabidhi
tuzo ya heshima, Kitwana Manara wakati wa halfa ya utoaji tuzo
mbalimbali za ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara iliyoandaliwa na
wadhamini wakuu wa ligi na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa
Mlimani city jijini Dar es Salaam.
Waziri
wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dkt, Harrison Mwakyembe (katikati)
Mkurugenzi mkuu wa biashara wa Vodacom Tanzania, Hisham Hendi(kushoto)
wakimkabidhi tuzo ya mchezaji bora wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara
2016/2017 baba mzazi wa mchezaji wa Simba, Mohamed Hussein ”Tshabalala”
baada ya mtoto wake kuchukua tuzo hiyo hapo jana wakati wa halfa ya
utoaji tuzo mbalimbali za ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara
iliyoandaliwa na wadhamini wakuu wa ligi na kufanyika katika ukumbi wa
mikutano wa Mlimani city jijini Dar es Salaam.
Waziri
wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dkt, Harrison Mwakyembe (katikati)
akimshuhudia Mkurugenzi mkuu wa biashara wa Vodacom Tanzania, Hisham
Hendi(kushoto)akimpongeza baba mzazi wa mchezaji wa Simba, Mohamed
Hussein ”Tshabalala” baada ya mtoto wake kuibuka mshindi wa tuzo ya
mchezaji bora wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara 2016/2017 wakati wa
halfa ya utoaji tuzo mbalimbali za ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara
iliyoandaliwa na wadhamini wakuu wa ligi na kufanyika katika ukumbi wa
mikutano wa Mlimani city jijini Dar es Salaam.
Wadhamini
wakuu wa Ligi ya Mpira wa miguu Tanzania Bara kampuni ya Mawasiliano ya
Vodacom Tanzania PLC, jana ilitoa zawadi zenye thamani ya shilingi
232,974,660 kwa washindi mbali mbali wa ligi.
Akizungumza
wakati wa hafla ya utoaji zawadi iliyofanyika jijini Dar es Salaama
jana, Mkurugenzi Mkuu wa biashara na Masoko wa kampuni hiyo, Hisham Hendi
alisema Vodacom imeongeza kiasi cha fedha zaidi mwaka huu.
Mwaka
jana tulitoa shilingi 219,502,500. Kwa ajili ya zawadi lakini mwaka huu
fedha hizi zimeongezeka na kufikia shilingi 232,974,660,” alisema
Hendi
alisema, Vodacom Tanzania inavutiwa na jinsi ambavyo umaarufu wa ligi
unavyokuwa ukiongezeka siku hadi siku huku ukiwavutia na kuwaburudisha
Watanzania walio wengi wanaoishi mijini na vijijini bila kujali kama
timu za maeneo wanayoishi zinashiriki ligi hii.
“Pamoja
na umaarufu wa ligi hii kuongezeka na mafanikio yanayozidi kupatikana,
sisi kama wadhamini tunajua kuwa bado kuna changamoto mbalimbali za
kuboresha ligi yetu iwe na viwango vya hali ya juu na ili kuondokana na
changamoto hizi unahitajika ushirikiano mkubwa baina ya wadau wote wa
mchezo wa soka nchini japo mabadiliko hayawezi kuja kwa siku moja,”
alieleza.
Mkurugenzi
huyo alitoa wito kwa wadau wote kushiriki kubuni mikakati ya kuboresha
ligi hii na ikiwezekana wajitokeze wafadhili wengine zaidi ili wachezaji
wazidi kunufaika.
“Kama
sote tunavyoelewa hivi sasa michezo sio burudani tu kama ilivyokuwa
miaka ya zamani bali inasaidia kupunguza tatizo la ajira na kuinua
uchumi wa nchi kwani wanamichezo wakiwezeshwa wanaweza kupitia mapato
yao kuboresha pato la taifa kama tunavyosikia katika nchi za wenzetu
ambako wachezaji na wasanii ni kundi la mamilionea wanaotambulika na
hapa tukiamua yote haya yanawezekana na dalili zimeanza kuonekana.
Alisema
Vodacom itaendelea kuunga mkono na kufadhili mchezo wa soka na michezo
mingine kwa kuwa inaamini wanamichezo ni mabalozi wazuri katika
kutangaza Taifa na pia michezo huchangia kuibua na kukuza vipaji vya
wanamichezo.
“Kwa
niaba ya Vodacom Tanzania naipongeza timu bingwa ya ligi ya Soka ya
Vodacom msimu uliomalizika Yanga African bila kusahau timu zote
zilizofanya vizuri na wote waliokabidhiwa zawadi zao leo.
Ni
matumaini yetu maandalizi ya msimu ujao wa ligi yamekwishaanza
kuandaliwa vizuri na wadau wote tutashirikiana tena kuhakikisha ubora wa
ligi unazidi kuwa bora zaidi,” alisema Hisham.
COMMENTS