Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCMM), umem pongeza Mwenyekiti wa CCM na Rais wa ...
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCMM), umempongeza
Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John
Pombe Magufuli kwa kuonesha Uzalendo mkubwa alionao kwa nchi yake, baada
ya kuchukua maamuzi yenye maslahi ya nchi katika sakata la zima la
Makinikia.
Hayo yamesemwa leo na Kaimu Katibu mkuu wa UVCCM Shaka Hamdu Shaka (MNEC) alipokuwa akitoa salamu za pongezi za Vijana wote katika ukumbi wa CCM Vijana Kinondoni .
Shaka
amesema Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi unampongeza Mwenyekiti
wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa na uzalendo wa
hali ya juu alionao kwa Taifa mara baada ya kuchukua maamuzi yenye
masalhi ya nchi katika swala zima la Makinikia.
Amesema
Umoja wa Vijana wa CCM unaunga mkono maamuzi yote yaliyopitishwa au
kutolewa na Rais Dk John Magufuli mara baada ya kupokea ripoti ya Tume
ya Uchunguzi
“Umoja
wa Vijana wa CCM hatuko tayari na hatutakubali kushuhudia tena Tanzania
ikirejea katika zama ya kiza kinene cha ukwapuaji mali, ulaji,
kufilisi mashirika ya umma au wizi wa mali za umma.tunaishauri serikali
yetu iendelee na mikakati yake ya kuhakikisha ukwapuaji, ubabaishaji,
wizi na ufisadi wa mali za serikali vinavikomeshwa mara moja
Amesema
kuwa Umoja wa Vijana wa CCM unaiomba kwa dhati Serikali yetu ianze
kuipitia upya mikataba yote ya madini ili kubaini kama ni yenye manufaa
na maslahi mapana kwa umma na kumuomba Rais Dk John Magufuli kuwaweka
pembeni wasaidizi wake wote ambao bado wanaonekana kuwa na kigugumizi
katika kuwatumikia wananchi huku baadhi yao wakiona muhali kupambana na
ufisadi.
Ameweka
wazi kuwa UVCCM Inasisitiza kuwa Watendaji wote waliokuwa na dhamana na
ambao wamehusika kwa namna moja au nyingine kupoteza mapato na kulitia
hasara Taifa, hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao haraka .
Amesema
wao wanaishauri Serikali kuendelea kuwabaini na kuwachukulia hatua
Viongozi na watendaji wa serikali ambao watabainika kumiliki mali,
utajiri na vitega uchumi ambavyo havitokani na mapato yasiolingana na
vipato vyao wataifishwe kama ilivyofanyika mwaka 1967 baada ya
kutangazwa Azimio la Arusha .
“Vijana
wote tunaishauri serikali yetu isikubali na isiafiki mali za umma
zitumike kwa maslahi binafsi badala yake kila miliki ya serikali na mali
ya umma ifahamike kuwa kila mwananchi ana haki kufaidika nayo ambayo
ni sehemu ya matunda ya Uhuru na Mapinduzi matukufu ya Zanzibar”.
Alimaliza
kwa kusema kuwa Umoja wa Vijana wa CCM unawataka wana CCM na
Watanzania wote kwa ujumla kuendelea kumuunga mkono Mheshimiwa Rais na
Serikali yake katika mapambano dhidi ya vikundi vya rushwa, ufisadi na
uzembe kwa baadhi ya watendaji ili kuleta maendeleo endelevu katika
taifa letu.
Kaimu
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Shaka
Hamdu Shaka (MNEC) akizungumza na Vijana wa Mkoa wa Dar es Salaam wakati
wa mkutano wa kumpongeza Rais John Pombe Magufuli kwa maamuzi
aliyochukua.
Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akiwa na Viongozi wa ngazi za juu wa umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM)
Kaimu
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Shaka
Hamdu Shaka (MNEC) akicheza muziki na baadhi ya wanachama wa UVCCM
Kaimu
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Shaka
Hamdu Shaka (MNEC) Akiwa amebebwa juu na Vijana wa CCM
Sehemu
ya Vijana wa Hamasa wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi
wakifurahi juu ya mamuzi yaliyochukuliwa na Rais John Pombe Mgufuli
Kaimu
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Shaka
Hamdu Shaka (MNEC) akiwasili katika ukumbi wa Umoja wa Vijana Kinondoni
Kaimu
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Shaka
Hamdu Shaka (MNEC) akiwasili katika Ukumbi wa Umoja wa Vijana Kinondoni
smsehemu ya Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wakiwa na furaha kubwa sana
ehemu ya Vijana wa Hamasa wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi wakifurahi juu ya mamuzi yaliyochukuliwa na Rais John Pombe Mgufuli
Mabango ya kumpongeza Rais Magufuli
COMMENTS