Kaimu Katibu Tawala upande wa Uchumi na Uzalisha Mkoa wa Dar es salaam Ndg Edward Otieno akizungumza wakati wa ufunguzi wa UMISSET...
Kaimu
Katibu Tawala upande wa Uchumi na Uzalisha Mkoa wa Dar es salaam Ndg
Edward Otieno akizungumza wakati wa ufunguzi wa UMISSETA Mkoa wa Dar es
salaam Leo Mei 28, 2017 katika Uwanja wa Uhuru.
Mkurugenzi
wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akiwasalimu wanamichezo
wakati wa ufunguzi wa UMISSETA Mkoa wa Dar es salaam Leo Mei 28, 2017
katika Uwanja wa Uhuru.
Baadhi
ya wanamichezo kutoka Manispaa za Mkoa wa Dar es salaam wakifatilia
mchezo kati ya Ilala na Ubungo wakati wa ufunguzi wa UMISSETA Mkoa wa
Dar es salaam Leo Mei 28, 2017 katika Uwanja wa Uhuru.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akisalimiana na mchezaji
wa Mpira wa Miguu Manispaa ya Ubungo wakati wa ufunguzi wa UMISSETA
Mkoa wa Dar es salaam Leo Mei 28, 2017 katika Uwanja wa Uhuru.
Mkurugenzi
wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo (Kushoto), Kaimu Katibu
Tawala upande wa Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Dar es salaam Ndg Edward
Otieno (Katikati) na Afisa Elimu Mkoa wa Dar es salaam Khamisi Lissu
wakati wa ufunguzi wa UMISSETA Mkoa wa Dar es salaam Leo Mei 28, 2017
katika Uwanja Uhuru.
Mkurugenzi
wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akitoa hamasa kwa timu ya
UMISSETA Wilaya ya Ubungo wakati wa ufunguzi wa UMISSETA Mkoa wa Dar
es salaam Leo Mei 28, 2017 katika Uwanja wa Uhuru.
Mkurugenzi
wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akiimba wimbo maalumu wa
Michezo ya UMISSETA wakati wa ufunguzi wa UMISSETA Mkoa wa Dar es
salaam Leo Mei 28, 2017 katika Uwanja wa Uhuru.
Na Mathias Canal, Dar es salaam
Maandalizi
ya ngazi ya Mkoa wa Dar es salaam Kwa Mashindano ya Umoja wa Michezo
Shule za Sekondari Tanzania yamezidi kupamba Moto katika Uwanja wa Uhuru
na Uwanja wa Taifa Jjijini Dar es salaam.
Maandalizi
hayo kwa ngazi ya Mkoa kwa ajili ya kupata timu ya Mkoa Wa Dar es
salaam yameanza Leo Mei 28, 2017 Kwa kuhusisha Manispaa za Mkoa wa Dar
es salaam ikiwemo Manispaa ya Ilala, Temeke, Kinondoni, Kgamboni na
Ubungo.
Akizungumza
katika ufunguzi wa mashindano hayo Kwa ngazi ya Wilaya za Mkoa wa Dar
es salaam Kaimu Katibu Tawala katika upande wa Uchumi na Uzalisha Mkoa
wa Dar es salaam Ndg Edward Otieno amewasihi washiriki kutumia weledi
wao wa mafunzo waliyoyapata kuhusu michezo na kuonyesha umahiri wao ili
kuchaguliwa katika timu ya Mkoa.
Wanafunzi
hao ambao wameweka kambi katika Shule ya Sekondari Jitegemee mpaka Mei
31, 2017 wataanza safari ya kuelekea Jijini Mwanza kwa ajili ya
mashindano hayo ngazi ya Taifa yanayotaraji kuanza kufanyika katika
uwanja wa CCM Kirumba June 6, 2017.
Otieno
alisema kuwa vijana hao wanapaswa kutambua kuwa michezo ndio ajira
inayolipa zaidi Duniani hivyo wanapaswa kudumisha nidhamu kwa kipindi
chote Cha mashindano.
Aliongeza
kuwa wanapaswa kutambua kuwa timu zote za Mkoa wa Dar es salaam
zitakwenda Mwanza kushindana katika michezo hiyo ngazi ya Taifa na si
kushiriki pekee.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo
aliyezuru katika Uwanja wa Uhuru kujionea Timu ya Vijana wake kutoka
Manispaa ya Ubungo ikichuana vikali na timu ya Manispaa ya Ilala
amepongeza juhudi za washiriki wote ambao wameonyesha nidhamu ya Hali ya
juu.
"Ukiona
vijana Wana nidhamu Kama hivi ni vyena kuwapongeza na kuwatia moyo
maana Bado Wana safari ndefu kimichezo na kimaisha" Alisema MD Kayombo
Mkurugenzi
Kayombo ametilia msisitizo zaidi kutumia weledi wao ili kurejesha
heshima ya michezo katika Manispaa ya Ubungo na Mkoa wa Dar es salaam
Kwa ujumla.
COMMENTS